< Joeli 3 >

1 “Katika siku hizo na wakati huo, nitakaporejesha neema ya Yuda na Yerusalemu,
For, behold, in those days, and in that time, when I shall bring back the captivity of Judah and Jerusalem,
2 nitayakusanya mataifa yote na kuyaleta katika Bonde la Yehoshafati Hapo nitaingia kwenye hukumu dhidi yao kuhusu urithi wangu, watu wangu Israeli, kwa kuwa waliwatawanya watu wangu miongoni mwa mataifa na kuigawa nchi yangu.
I will gather all nations, and will bring them down into the valley of Jehoshaphat; and I will enter into judgment with them there for My people and for My heritage Israel, whom they have scattered among the nations, and divided My land.
3 Wanawapigia kura watu wangu na kuwauza wavulana ili kupata makahaba; waliwauza wasichana ili wapate kunywa mvinyo.
And they have cast lots for My people; and have given a boy for an harlot, and sold a girl for wine, and have drunk.
4 “Sasa una nini dhidi yangu, ee Tiro na Sidoni, nanyi nchi zote za Ufilisti? Je, mnanilipiza kwa yale niliyoyafanya? Kama mnalipa, mimi nitalipiza juu ya vichwa vyenu kwa kasi na kwa haraka yale mliyoyatenda.
And also what are ye to Me, O Tyre, and Zidon, and all the regions of Philistia? will ye render retribution on My behalf? and if ye render retribution on My behalf, swiftly, speedily will I return your retribution upon your own head.
5 Kwa kuwa mlichukua fedha na dhahabu yangu pia mkabeba hazina zangu nzuri sana mkapeleka kwenye mahekalu yenu.
Forasmuch as ye have taken My silver and My gold, and have carried into your temples My goodly treasures;
6 Mliwauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kwamba mpate kuwapeleka mbali na nchi yao.
the children also of Judah and the children of Jerusalem have ye sold unto the sons of Jevanim, that ye might remove them far from their border;
7 “Tazama nitawaamsha kutoka zile sehemu mlizowauza, nami nitawalipiza juu ya vichwa vyenu kile mlichofanya.
behold, I will stir them up out of the place whither ye have sold them, and will return your retribution upon your own head;
8 Nitawauza wana wenu na binti zenu kwa watu wa Yuda, nao watawauza kwa Waseba, taifa lililo mbali.” Bwana amesema.
and I will sell your sons and your daughters into the hand of the children of Judah, and they shall sell them to the men of Sheba, to a nation far off; for the LORD hath spoken.
9 Tangazeni hili miongoni mwa mataifa: Jiandaeni kwa vita! Amsha askari! Wanaume wote wapiganaji wasogee karibu na kushambulia.
Proclaim ye this among the nations, prepare war; stir up the mighty men; let all the men of war draw near, let them come up.
10 Majembe yenu yafueni yawe panga na miundu yenu ya kukatia iwe mikuki. Aliye dhaifu na aseme, “Mimi nina nguvu!”
Beat your plowshares into swords, and your pruning-hooks into spears; let the weak say: 'I am strong.'
11 Njooni haraka, ninyi mataifa yote kutoka pande zote, kusanyikeni huko. Shusha wapiganaji wako, Ee Bwana!
Haste ye, and come, all ye nations round about, and gather yourselves together; thither cause Thy mighty ones to come down, O LORD!
12 “Mataifa na yaamshwe; na yasonge mbele kuelekea Bonde la Yehoshafati, kwa kuwa nitaketi mahali pale kuhukumu mataifa yote yaliyoko kila upande.
Let the nations be stirred up, and come up to the valley of Jehoshaphat; for there will I sit to judge all the nations round about.
13 Tia mundu, kwa kuwa mavuno yamekomaa. Njooni, mkanyage zabibu, kwa kuwa shinikizo la kukamua zabibu limejaa na mapipa yanafurika: kwa kuwa uovu wao ni mkubwa!”
Put ye in the sickle, for the harvest is ripe; come, tread ye, for the winepress is full, the vats overflow; for their wickedness is great.
14 Umati mkubwa, umati mkubwa katika bonde la uamuzi! Kwa kuwa siku ya Bwana ni karibu katika bonde la uamuzi.
Multitudes, multitudes in the valley of decision! For the day of the LORD is near in the valley of decision.
15 Jua na mwezi vitatiwa giza, na nyota hazitatoa mwanga wake tena.
The sun and the moon are become black, and the stars withdraw their shining.
16 Bwana atanguruma kutoka Sayuni na mshindo wa ngurumo kutoka Yerusalemu; dunia na mbingu vitatikisika. Lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, ngome imara kwa ajili ya watu wa Israeli.
And the LORD shall roar from Zion, and utter His voice from Jerusalem, and the heavens and the earth shall shake; but the LORD will be a refuge unto His people, and a stronghold to the children of Israel.
17 “Ndipo mtakapojua kwamba Mimi, Bwana Mungu wenu, nakaa Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Yerusalemu utakuwa mtakatifu; kamwe wageni hawatavamia tena.
So shall ye know that I am the LORD your God, dwelling in Zion My holy mountain; then shall Jerusalem be holy, and there shall no strangers pass through her any more.
18 “Katika siku hiyo milima itadondosha divai mpya, na vilima vitatiririka maziwa; mabonde yote ya Yuda yatatiririka maji. Chemchemi itatiririka kutoka kwenye nyumba ya Bwana na kunywesha Bonde la Shitimu.
And it shall come to pass in that day, that the mountains shall drop down sweet wine, and the hills shall flow with milk, and all the brooks of Judah shall flow with waters; and a fountain shall come forth of the house of the LORD, and shall water the valley of Shittim.
19 Lakini Misri itakuwa ukiwa, Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya jeuri waliofanya kwa watu wa Yuda, ambao katika nchi yao walimwaga damu isiyo na hatia.
Egypt shall be a desolation, and Edom shall be a desolate wilderness, for the violence against the children of Judah, because they have shed innocent blood in their land.
20 Yuda itakaliwa na watu milele na Yerusalemu itadumu vizazi vyote.
But Judah shall be inhabited for ever, and Jerusalem from generation to generation.
21 Hatia yao ya damu, ambayo sijasamehe, nitasamehe.”
And I will hold as innocent their blood that I have not held as innocent; and the LORD dwelleth in Zion.

< Joeli 3 >