< Amosi 5 >

1 Sikia neno hili, ee nyumba ya Israeli, ombolezo hili ninalifanya kuwahusu ninyi:
Hear ye this word which I take up for a lamentation over you, O house of Israel:
2 “Bikira Israeli ameanguka, kamwe hatainuka tena, ameachwa pweke katika nchi yake, hakuna yeyote wa kumwinua.”
The virgin of Israel is fallen, she shall no more rise; she is cast down upon her land, there is none to raise her up.
3 Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “Wakati mmoja wa miji yako utakapopeleka watu elfu moja vitani kwa ajili ya Israeli, mia moja tu watarudi; wakati mji utakapopeleka mia moja, kumi tu ndio watarudi hai.”
For thus saith the Lord GOD: The city that went forth a thousand shall have a hundred left, and that which went forth a hundred shall have ten left, of the house of Israel.
4 Hili ndilo Bwana asemalo kwa nyumba ya Israeli: “Nitafuteni mpate kuishi;
For thus saith the LORD unto the house of Israel: Seek ye Me, and live;
5 msitafute Betheli, msiende Gilgali, msisafiri kwenda Beer-Sheba. Kwa maana kwa hakika Gilgali itakwenda uhamishoni, na Betheli itafanywa kuwa si kitu.”
But seek not Beth-el, nor enter into Gilgal, and pass not to Beer-sheba; for Gilgal shall surely go into captivity, and Beth-el shall come to nought.
6 Mtafuteni Bwana mpate kuishi, au atafagia nyumba ya Yosefu kama moto; utawateketeza, nayo Betheli haitakuwa na yeyote wa kuuzima.
Seek the LORD, and live — lest He break out like fire in the house of Joseph, and it devour, and there be none to quench it in Bethel —
7 Ninyi ambao mnageuza haki kuwa uchungu na kuiangusha haki chini
Ye who turn judgment to wormwood, and cast righteousness to the ground;
8 (yeye ambaye alifanya Kilimia na Orioni, ambaye hugeuza giza kuwa mapambazuko na mchana kuwa usiku, ambaye huyaita maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake;
Him that maketh the Pleiades and Orion, and bringeth on the shadow of death in the morning, and darkeneth the day into night; that calleth for the waters of the sea, and poureth them out upon the face of the earth; the LORD is His name;
9 yeye hufanya maangamizo kwenye ngome na kufanya mji uliozungushiwa ngome kuwa ukiwa),
That causeth destruction to flash upon the strong, so that destruction cometh upon the fortress.
10 mnamchukia yule akemeaye mahakamani, na kumdharau yule ambaye husema kweli.
They hate him that reproveth in the gate, and they abhor him that speaketh uprightly.
11 Mnamgandamiza maskini na kumlazimisha awape nafaka. Kwa hiyo, ingawa mmejenga majumba ya mawe ya fahari, hamtaishi ndani yake; ingawa mmepanda mashamba mazuri ya mizabibu, hamtakunywa divai yake.
Therefore, because ye trample upon the poor, and take from him exactions of wheat; ye have built houses of hewn stone, but ye shall not dwell in them, ye have planted pleasant vineyards, but ye shall not drink wine thereof.
12 Kwa kuwa ninajua hesabu ya makosa yenu na ukubwa wa dhambi zenu. Mmewaonea wenye haki na kupokea rushwa na kuzuia haki ya maskini mahakamani.
For I know how manifold are your transgressions, and how mighty are your sins; ye that afflict the just, that take a ransom, and that turn aside the needy in the gate.
13 Kwa hiyo mtu mwenye busara hunyamaza kimya nyakati kama hizo, kwa kuwa nyakati ni mbaya.
Therefore the prudent doth keep silence in such a time; for it is an evil time.
14 Tafuteni mema, wala si mabaya, ili mpate kuishi. Ndipo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote atakuwa pamoja nanyi, kama msemavyo yupo nanyi.
Seek good, and not evil, that ye may live; and so the LORD, the God of hosts, will be with you, as ye say.
15 Yachukieni maovu, yapendeni mema; dumisheni haki mahakamani. Yamkini Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote atawahurumia mabaki ya Yosefu.
Hate the evil, and love the good, and establish justice in the gate; it may be that the LORD, the God of hosts, will be gracious unto the remnant of Joseph.
16 Kwa hiyo hili ndilo Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Kutakuwepo maombolezo katika barabara zote na vilio vya uchungu katika njia kuu zote. Wakulima wataitwa kuja kulia, na waombolezaji waje kuomboleza.
Therefore thus saith the LORD, the God of hosts, the Lord: Lamentation shall be in all the broad places, and they shall say in all the streets: 'Alas! alas!' and they shall call the husbandman to mourning, and proclaim lamentation to such as are skilful of wailing.
17 Kutakuwepo kuomboleza katika mashamba yote ya mizabibu, kwa kuwa nitapita katikati yenu,” asema Bwana.
And in all vineyards shall be lamentation; for I will pass through the midst of thee, saith the LORD.
18 Ole wenu ninyi mnaoitamani siku ya Bwana! Kwa nini mnaitamani siku ya Bwana? Siku hiyo itakuwa giza, si nuru.
Woe unto you that desire the day of the LORD! Wherefore would ye have the day of the LORD? It is darkness, and not light.
19 Itakuwa kama vile mtu aliyemkimbia simba kumbe akakutana na dubu, kama vile mtu aliyeingia nyumbani mwake na kuupumzisha mkono wake kwenye ukuta, kumbe akaumwa na nyoka.
As if a man did flee from a lion, and a bear met him; and went into the house and leaned his hand on the wall, and a serpent bit him.
20 Je, siku ya Bwana haitakuwa giza, na si nuru: giza nene, bila mwonzi wa mwanga?
Shall not the day of the LORD be darkness, and not light? Even very dark, and no brightness in it?
21 “Ninachukia, ninazidharau sikukuu zenu za dini; siwezi kuvumilia makusanyiko yenu.
I hate, I despise your feasts, and I will take no delight in your solemn assemblies.
22 Hata ingawa mnaniletea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za nafaka, sitazikubali. Ingawa mnaniletea sadaka nzuri za amani, sitazitambua.
Yea, though ye offer me burnt-offerings and your meal-offerings, I will not accept them; neither will I regard the peace-offerings of your fat beasts.
23 Niondoleeni kelele za nyimbo zenu! Sitasikiliza sauti za vinubi vyenu.
Take thou away from Me the noise of thy songs; and let Me not hear the melody of thy psalteries.
24 Lakini acheni haki itiririke kama mto, na uadilifu uwe kama kijito kisichokauka!
But let justice well up as waters, and righteousness as a mighty stream.
25 “Je, mliniletea dhabihu na sadaka kwa miaka arobaini kule jangwani, ee nyumba ya Israeli?
Did ye bring unto Me sacrifices and offerings in the wilderness forty years, O house of Israel?
26 Mmeyainua madhabahu ya mfalme wenu, Sikuthi mungu wenu mtawala, na Kiuni mungu wenu wa nyota, ambao mliwatengeneza wenyewe.
So shall ye take up Siccuth your king and Chiun your images, the star of your god, which ye made to yourselves.
27 Kwa sababu hiyo nitawapeleka uhamishoni mbali kupita Dameski,” asema Bwana, ambaye jina lake ni Mungu Mwenye Nguvu Zote.
Therefore will I cause you to go into captivity beyond Damascus, saith He, whose name is the LORD God of hosts.

< Amosi 5 >