< Yeremia 36 >

1 Katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia nabii Yeremia kutoka kwa Bwana, kusema:
W czwartym roku Joakima, syna Jozjasza, króla Judy, doszło do Jeremiasza słowo od PANA mówiące:
2 “Chukua kitabu uandike ndani yake maneno yote niliyonena nawe kuhusu Israeli, Yuda na mataifa mengine yote, tangu nilipoanza kunena nawe wakati wa utawala wa Yosia hadi sasa.
Weź sobie zwój księgi i napisz na nim wszystkie słowa, które wypowiadałem do ciebie przeciw Izraelowi, przeciw Judzie i przeciw wszystkim narodom od dnia, kiedy [zacząłem] mówić do ciebie, od dni Jozjasza aż do dziś.
3 Labda watu wa Yuda watakaposikia juu ya kila maafa ninayokusudia kuwapiga nayo, kila mmoja wao atageuka kutoka njia zake mbaya, kisha nitasamehe uovu wao na dhambi yao.”
Może [gdy] dom Judy usłyszy o całym tym nieszczęściu, które zamierzam im uczynić, odwróci się każdy od swojej złej drogi, abym przebaczył ich nieprawość i grzech.
4 Hivyo Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria, naye Yeremia alipokuwa akiyakariri maneno yote aliyoyasema Bwana, Baruku akayaandika katika kitabu.
Jeremiasz więc wezwał Barucha, syna Neriasza, a Baruch spisał z ust Jeremiasza na zwoju księgi wszystkie słowa PANA, które mówił do niego.
5 Kisha Yeremia akamwambia Baruku, “Nimezuiliwa, mimi siwezi kuingia katika Hekalu la Bwana.
Potem Jeremiasz nakazał Baruchowi: Jestem powstrzymany i nie mogę wejść do domu PANA;
6 Basi wewe nenda katika nyumba ya Bwana siku ya kufunga, uwasomee watu maneno ya Bwana kutoka kitabu hiki yale uliyoyaandika kutoka kinywani mwangu. Wasomee watu wote wa Yuda waliofika kutoka miji yao.
Dlatego ty idź i odczytaj z tego zwoju, co napisałeś z moich ust – słowa PANA – do uszu ludu w domu PANA, w dzień postu. Odczytaj [to] także do uszu wszystkich z Judy, którzy przychodzą ze swoich miast.
7 Labda wataomba na kusihi mbele za Bwana na kila mmoja akageuka kutoka njia zake mbaya, kwa sababu hasira na ghadhabu zilizotamkwa dhidi ya watu hawa na Bwana ni kubwa.”
Może skierują swoje błaganie przed oblicze PANA i każdy odwróci się od swojej złej drogi. Wielkie są bowiem gniew i zapalczywość, które PAN wypowiedział przeciwko temu ludowi.
8 Baruku mwana wa Neria akafanya kila kitu nabii Yeremia alichomwambia kufanya. Alisoma maneno ya Bwana katika Hekalu la Bwana kutoka kile kitabu.
I postąpił Baruch, syn Neriasza, zgodnie ze wszystkim, co prorok Jeremiasz mu nakazał, odczytując z księgi słowa PANA w domu PANA.
9 Katika mwezi wa tisa, mnamo mwaka wa tano wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati wa kufunga mbele za Bwana, ilitangazwa kwa watu wote walioko Yerusalemu, na wale wote waliokuwa wamekuja kutoka miji ya Yuda.
W piątym roku Joakima, syna Jozjasza, króla Judy, w dziewiątym miesiącu, zapowiedziano post przed PANEM całemu ludowi w Jerozolimie i całemu ludowi, który przybył z miast Judy do Jerozolimy.
10 Kutoka chumba cha Gemaria mwana wa Shafani mwandishi, kilichokuwa katika ua wa juu kwenye ingilio la Lango Jipya la Hekalu, Baruku akawasomea watu wote waliokuwa katika Hekalu la Bwana maneno ya Yeremia kutoka kwenye kile kitabu.
I Baruch odczytał z księgi słowa Jeremiasza w domu PANA, w komnacie Gemariasza, syna Szafana, pisarza, na górnym dziedzińcu, u wejścia do Bramy Nowej domu PANA, do uszu całego ludu.
11 Basi Mikaya mwana wa Gemaria, mwana wa Shafani, aliposikia maneno yote ya Bwana kutoka kwenye kile kitabu,
A [gdy] Micheasz, syn Gemariasza, syna Szafana, usłyszał wszystkie słowa PANA z księgi;
12 alishuka hadi kwenye chumba cha mwandishi kwenye jumba la kifalme, mahali walipokuwa wameketi maafisa wote: yaani Elishama mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnathani mwana wa Akbori, Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania, na maafisa wengine wote.
Zszedł do domu króla, do komnaty pisarza, a oto siedzieli tam wszyscy książęta: Eliszama, pisarz, Delajasz, syn Szemajasza, Elnatan, syn Akbora, Gemariasz, syn Szafana, Sedekiasz, syn Chananiasza, i pozostali książęta.
13 Baada ya Mikaya kuwaambia kila kitu ambacho alikuwa amesikia Baruku akiwasomea watu kutoka kwenye kile kitabu,
I Micheasz powiedział im wszystkie słowa, które usłyszał, gdy Baruch czytał z księgi do uszu ludu.
14 maafisa wote wakamtuma Yehudi mwana wa Nethania, mwana wa Shelemia, mwana wa Kushi, kumwambia Baruku, “Leta hicho kitabu ambacho umewasomea watu, nawe mwenyewe uje.” Ndipo Baruku mwana wa Neria akawaendea akiwa na hicho kitabu mkononi mwake.
Wtedy wszyscy książęta posłali do Barucha Jehudiego, syna Netaniasza, syna Szelemiasza, syna Kusziego, z poleceniem: Weź do ręki zwój, z którego czytałeś do uszu ludu, i przyjdź. Baruch więc, syn Neriasza, wziął zwój do ręki i przyszedł do nich.
15 Wakamwambia, “Tafadhali, keti na utusomee hicho kitabu.” Ndipo Baruku akawasomea kile kitabu.
I powiedzieli do niego: Usiądź proszę i odczytaj to do naszych uszu. Czytał więc Baruch do ich uszu.
16 Walipoyasikia maneno hayo yote, wakatazamana wao kwa wao kwa woga na kumwambia Baruku, “Lazima tutoe taarifa ya maneno haya yote kwa mfalme.”
A gdy usłyszeli wszystkie te słowa, [spojrzeli] przerażeni jeden na drugiego i powiedzieli do Barucha: Musimy powiadomić króla o tych wszystkich słowach.
17 Kisha wakamuuliza Baruku, “Tuambie, uliandikaje haya yote? Je, yalitoka kinywani mwa Yeremia?”
I zapytali Barucha: Powiedz nam teraz, jak spisywałeś wszystkie te słowa z jego ust?
18 Baruku akajibu, “Ndiyo, maneno haya yote yalitoka kinywani mwa Yeremia, nami nikayaandika kwa wino katika hiki kitabu.”
Baruch odpowiedział: Ustnie podawał mi wszystkie te słowa, a ja spisałem [je] atramentem w księdze.
19 Ndipo wale maafisa wakamwambia Baruku, “Wewe na Yeremia nendeni mkajifiche. Mtu yeyote asijue mahali mlipo.”
Wtedy książęta powiedzieli do Barucha: Idź, ukryj się, ty i Jeremiasz, a niech nikt nie wie, gdzie jesteście.
20 Baada ya kuhifadhi kile kitabu ndani ya chumba cha Elishama mwandishi, wakamwendea mfalme katika ua wa nje na kumwarifu kila kitu.
Potem weszli do króla na dziedziniec, ale księgę ukryli w komnacie Eliszamy, pisarza, i opowiedzieli do uszu króla wszystkie [te] słowa.
21 Mfalme akamtuma Yehudi akachukue kile kitabu. Yehudi akakileta hicho kitabu kutoka kwenye chumba cha Elishama mwandishi, na akakisoma mbele ya mfalme na maafisa wakiwa wamesimama kando ya mfalme.
Król więc posłał Jehudiego, aby wziął zwój, a ten zabrał go z komnaty Eliszamy, pisarza. I Jehudi odczytał go do uszu króla i wszystkich książąt, którzy stali przed królem.
22 Ulikuwa mwezi wa tisa, na mfalme alikuwa ameketi chumba cha wakati wa baridi akiota moto.
A król siedział w domu zimowym, w dziewiątym miesiącu, i [ogień] płonął na palenisku przed nim.
23 Hata ikawa kila wakati Yehudi alipomaliza kusoma kurasa tatu au nne za hicho kitabu, mfalme alizikata kwa kisu cha mwandishi na kuzitupia motoni, hadi kitabu chote kikateketea.
Gdy Jehudi przeczytał trzy lub cztery karty, odcinał je nożem pisarskim i wrzucał do ognia, który [rozpalony był] na palenisku, aż cały zwój spłonął w ogniu na palenisku.
24 Mfalme na watumishi wake wote waliosikia yote yaliyosomwa hawakuonyesha hofu yoyote, wala hawakuyararua mavazi yao.
Ale nie przerazili się i nie rozdarli swoich szat ani król, ani jego słudzy, którzy słyszeli wszystkie te słowa.
25 Hata ingawa Elnathani, Delaya na Gemaria walimsihi mfalme asikichome kile kitabu, yeye hakuwasikiliza.
Elnatan jednak, Delajasz i Gemariasz nalegali na króla, aby nie palił tego zwoju, ale ich nie usłuchał.
26 Badala yake, mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli kuwakamata mwandishi Baruku na nabii Yeremia. Lakini Bwana alikuwa amewaficha.
I król rozkazał Jerachmeelowi, synowi Meleka, Serajaszowi, synowi Azriela, i Szelemiaszowi, synowi Abdeela, aby pojmali Barucha, pisarza, i proroka Jeremiasza. Ale PAN ich ukrył.
27 Baada ya mfalme kuchoma kile kitabu kilichokuwa na yale maneno Baruku aliyokuwa ameyaandika kutoka kinywani mwa Yeremia, neno la Bwana lilimjia Yeremia likisema:
I do Jeremiasza doszło słowo PANA po spaleniu przez króla zwoju i słowa, które Baruch spisał z ust Jeremiasza, mówiące:
28 “Chukua kitabu kingine na uandike juu yake maneno yote yaliyokuwa katika kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda amekiteketeza kwa moto.
Weź sobie jeszcze inny zwój i zapisz na nim wszystkie poprzednie słowa, które były na pierwszym zwoju, spalonym przez Joakima, króla Judy.
29 Mwambie pia Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ulikiteketeza kile kitabu ukasema, “Kwa nini uliandika kwenye kitabu kwamba kwa hakika mfalme wa Babeli angekuja na kuangamiza nchi hii, na kuwakatilia mbali watu na wanyama kutoka humo?”
A do Joakima, króla Judy, powiedz: Tak mówi PAN: Ty spaliłeś ten zwój, mówiąc: Czemu napisałeś na nim: Na pewno król Babilonu nadciągnie, zniszczy tę ziemię i wytępi w niej człowieka i zwierzęta.
30 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana kuhusu Yehoyakimu mfalme wa Yuda: Hatakuwa na mtu yeyote atakayekalia kiti cha enzi cha Daudi; maiti yake itatupwa nje kwenye joto wakati wa mchana na kupigwa na baridi wakati wa usiku.
Dlatego tak mówi PAN o Joakimie, królu Judy: Nie będzie miał nikogo, kto zasiadłby na tronie Dawida, a jego zwłoki będą rzucone na upał we dnie i na mróz w nocy.
31 Nitamwadhibu yeye, watoto wake na watumishi wake kwa ajili ya uovu wao. Nitaleta juu yao na wote waishio Yerusalemu na watu wa Yuda kila maafa niliyoyasema dhidi yao, kwa sababu hawajasikiliza.’”
Nawiedzę go bowiem, jego potomstwo i jego sługi za ich nieprawość i sprowadzę na nich, na mieszkańców Jerozolimy i na Judejczyków całe to nieszczęście, które im zapowiedziałem, ale nie słuchali.
32 Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine na kumpa mwandishi Baruku mwana wa Neria, naye kama Yeremia alivyosema, Baruku akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa amekichoma moto, na maneno mengine mengi yaliyofanana na hayo yaliyoongezewa humo.
Wtedy Jeremiasz wziął inny zwój i dał go Baruchowi, synowi Neriasza, pisarzowi, a ten spisał na nim z ust Jeremiasza wszystkie słowa [tamtego] zwoju, który spalił w ogniu Joakim, król Judy. Nadto zostało dodane do nich wiele podobnych słów.

< Yeremia 36 >