< Isaya 18 >

1 Ole kwa nchi ya mvumo wa mabawa, kando ya mito ya Kushi,
Biada ziemi, którą zacieniają skrzydła, [ziemi] leżącej za rzekami Etiopii;
2 iwapelekayo wajumbe wake kwa njia ya bahari kwa mashua za mafunjo juu ya maji. Nendeni, wajumbe wepesi, kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo, kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu, taifa gomvi lenye lugha ngeni, ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito.
Która wysyła posłów przez morze w łodziach z sitowia po wodach, mówiąc: Idźcie, prędcy posłańcy, do narodu rozszarpanego i splądrowanego, do ludu, który budzi grozę, odkąd istnieje, do narodu zdeptanego do szczętu, którego ziemię rozrywają rzeki.
3 Enyi mataifa yote ya ulimwengu, ninyi mnaoishi duniani wakati bendera itakapoinuliwa milimani, mtaiona, nayo tarumbeta itakapolia, mtaisikia.
Wszyscy mieszkańcy świata i osiedleńcy ziemi, zobaczycie, jak sztandar zostanie wzniesiony na górach, i usłyszycie, gdy zadmą w trąby.
4 Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nitatulia kimya na kutazama kutoka maskani yangu, kama joto linalometameta katika mwanga wa jua, kama wingu la umande katika joto la wakati wa mavuno.”
Tak bowiem mówi PAN do mnie: Będę spokojny i będę przypatrywać się z mojego przybytku – jak pogodne ciepło po deszczu, jak obłok rosy w upalne żniwo.
5 Kwa maana, kabla ya mavuno, wakati wa kuchanua ukishapita na maua yakawa zabibu zinazoiva, atayakata machipukizi kwa mundu wa kupogolea matawi, naye atakata na kuyaondoa matawi yaliyopanuka.
Bo przed żniwem, gdy puszczą pączki, a kwiat wyda dojrzewające cierpkie grono, wtedy obetnie gałązki nożami i gałęzie usunie i obetnie.
6 Yote yataachwa kwa ajili ya ndege wawindao wa mlimani na wanyama pori, ndege watajilisha juu yake wakati wote wa kiangazi, nao wanyama pori wakati wote wa masika.
I będą pozostawione wszystkie razem ptakom górskim i zwierzętom polnym. Ptaki spędzą na nich lato, a wszystkie zwierzęta polne na nich przezimują.
7 Wakati huo matoleo yataletwa kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote kutoka kwa taifa la watu warefu wenye ngozi nyororo, kutoka kwa taifa linaloogopwa mbali na karibu, kutoka taifa gomvi lenye lugha ngeni, ambalo nchi yao imegawanywa kwa mito, matoleo yataletwa katika Mlima Sayuni, mahali pa Jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
W tym czasie będzie przyniesiony dar PANU zastępów od ludu rozszarpanego i splądrowanego, od ludu budzącego grozę, odkąd istnieje aż do dziś, od narodu do szczętu zdeptanego, którego ziemię rozrywały rzeki, na miejsce imienia PANA zastępów, na górę Syjon.

< Isaya 18 >