< Isaya 22 >

1 Neno kuhusu Bonde la Maono: Nini kinachokutaabisha sasa, kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?
Brzemię Doliny Widzenia. Co ci się stało, że cała wystąpiłaś na dachy?
2 Ewe mji uliojaa ghasia, ewe mji wa makelele na sherehe! Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.
Miasto pełne wrzasku i zgiełku, miasto wesołe! Twoi zabici nie padli od miecza ani nie zginęli w bitwie.
3 Viongozi wako wote wamekimbia pamoja, wamekamatwa bila kutumia upinde. Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja, mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.
Wszyscy twoi dowódcy pierzchli razem, związani przez łuczników. Zostali związani razem ci, których znaleziono u ciebie, ci, którzy uciekli z daleka.
4 Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami, niache nilie kwa uchungu. Usijaribu kunifariji juu ya maangamizi ya watu wangu.”
Dlatego powiedziałem: Odwróćcie swój wzrok ode mnie, abym gorzko zapłakał; nie próbujcie mnie pocieszać z powodu spustoszenia córki mojego ludu.
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya katika Bonde la Maono, siku ya kuangusha kuta na ya kupiga kelele mpaka milimani.
To jest bowiem dzień ucisku, deptania i zamieszania od Pana, BOGA zastępów, w Dolinie Widzenia, [dzień] burzenia murów i wołania na góry.
6 Elamu analichukua podo, pamoja na waendesha magari ya vita na farasi. Kiri anaifungua ngao.
Elam wziął kołczan z rydwanami ludu wojennego, a Kir odsłonił swoją tarczę.
7 Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita, nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;
I stało się tak, że najpiękniejsze doliny były pełne rydwanów, a jeźdźcy ustawili się potężnie przy bramie.
8 ulinzi wa Yuda umeondolewa. Nawe ulitazama siku ile silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,
I odkryto osłonę Judy, i w tym dniu spoglądałeś na zbrojownię w Domu Lasu.
9 mkaona kuwa Mji wa Daudi una matundu mengi katika ulinzi wake, mkaweka akiba ya maji kwenye Bwawa la Chini.
I spoglądaliście na wyłomy miasta Dawida – na to, że były liczne, i zgromadziliście wody Dolnej Sadzawki.
10 Mlihesabu majengo katika Yerusalemu nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.
Policzyliście domy w Jerozolimie i burzyliście domy, aby wzmocnić mur.
11 Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani, lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza, au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.
Zrobiliście też zbiornik między dwoma murami na wodę Starej Sadzawki, ale nie spoglądaliście na jej twórcę ani nie widzieliście tego, który od dawna ją ukształtował.
12 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliwaita siku ile ili kulia na kuomboleza, kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.
W tym dniu Pan, BÓG zastępów, wzywał do płaczu i do żałoby, do ostrzyżenia się i do przepasania się worem.
13 Lakini tazama, kuna furaha na sherehe, kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa mvinyo! Mnasema, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa!”
A oto radość i wesele, zabijanie wołów i owiec, spożywanie mięsa i picie wina: Jedzmy, pijmy, bo jutro umrzemy.
14 Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”
Ale PAN zastępów objawił mi to, [mówiąc] do [mych] uszu: Na pewno ta nieprawość nie będzie wam przebaczona aż do śmierci, mówi Pan, BÓG zastępów.
15 Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna, ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:
Tak mówi Pan, BÓG zastępów: Idź, udaj się do tego skarbnika, do Szebny, przełożonego domu, i powiedz:
16 Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa kujikatia kaburi lako mwenyewe, ukichonga kaburi lako mahali palipo juu, na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?
Co ty tu masz i kogo tu masz, że wykułeś sobie w tym miejscu grób? Wykułeś sobie grób wysoko, wydrążyłeś sobie w skale swoje mieszkanie.
17 “Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti, na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.
Oto PAN, który cię przykrył jak zacnego człowieka i który cię kosztownie przyoblekł;
18 Atakuvingirisha uwe kama mpira na kukutupa katika nchi kubwa. Huko ndiko utakakofia, na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia, wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!
Tocząc cię, zwinie i rzuci jak kulę w przestronną ziemię. Tam umrzesz, tam też rydwany twojej chwały będą hańbą domu twego pana.
19 Nitakuondoa kutoka kazi yako, nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.
Wypędzę cię z twego stanowiska, z twego urzędu ściągnę cię.
20 “Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia.
W tym dniu powołam swego sługę Eliakima, syna Chilkiasza.
21 Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
I ubiorę go w twoją szatę, i przepaszę go twoim pasem, i oddam w jego ręce twoją władzę; i będzie on ojcem dla mieszkańców Jerozolimy i domu Judy.
22 Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua.
I położę klucz domu Dawida na jego ramieniu; gdy on otworzy, nikt nie zamknie, a gdy zamknie, nikt nie otworzy.
23 Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake.
I wbiję go jak gwóźdź na miejscu pewnym, a będzie tronem chwały dla domu swego ojca.
24 Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”
I zawieszą na nim całą chwałę domu jego ojca, synowie i córki, wszelkie drobne naczynia, od kubków do wszelkich dzbanów.
25 Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.
W tym dniu, mówi PAN zastępów, gwóźdź, który był wbity w miejscu pewnym, zostanie wyjęty i przycięty, i spadnie; a brzemię, które wisiało na nim, zostanie odcięte. Tak bowiem PAN to powiedział.

< Isaya 22 >