< Mwanzo 49 >

1 Ndipo Yakobo akawaita wanawe na kusema: “Kusanyikeni kunizunguka ili niweze kuwaambia lile litakalowatokea siku zijazo.
Potem Jakub wezwał swoich synów i powiedział: Zbierzcie się, a oznajmię wam, co was spotka w [waszych] ostatnich dniach.
2 “Kusanyikeni na msikilize, enyi wana wa Yakobo, msikilizeni baba yenu Israeli.
Zbierzcie się i słuchajcie, synowie Jakuba, a słuchajcie waszego ojca Izraela.
3 “Reubeni, wewe ni mzaliwa wangu wa kwanza, nguvu zangu, tunda la kwanza la nguvu zangu, umepita kwa heshima, umepita kwa uwezo.
Rubenie, mój pierworodny, ty jesteś moją mocą i początkiem mojej siły, pierwszy dostojeństwem i pierwszy męstwem.
4 Usiyezuiwa kama maji, basi hutakuwa mkuu tena, kwa kuwa ulipanda kwenye kitanda cha baba yako, kwenye kitanda changu na kukinajisi.
Niestabilny jak woda, nie będziesz przodować, bo wstąpiłeś do łoża twego ojca; wstępując do mojego posłania, zbezcześciłeś je.
5 “Simeoni na Lawi ni wana ndugu: panga zao ni silaha za jeuri.
Symeon i Lewi, bracia, ich miecze to narzędzia przemocy.
6 Mimi na nisiingie katika baraza lao, nami nisiunganike katika kusanyiko lao, kwa kuwa wamewaua watu katika hasira yao, walikata mishipa ya miguu ya mafahali kama walivyopenda.
Niech moja dusza nie wchodzi w ich radę, niech moja sława nie jednoczy się z ich zgromadzeniem, bo w swej zapalczywości zabili człowieka, a w samowoli wywrócili mur.
7 Hasira yao na ilaaniwe, kwa kuwa ni kali mno, nayo ghadhabu yao ni ya ukatili! Nitawatawanya katika Yakobo Na kuwasambaza katika Israeli.
Przeklęta ich zapalczywość, bo uparta, i ich gniew, bo zatwardziały. Rozdzielę ich w Jakubie, a rozproszę ich w Izraelu.
8 “Yuda, ndugu zako watakusifu; mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako; wana wa baba yako watakusujudia.
Judo, to ciebie będą chwalić twoi bracia, twoja ręka będzie na karku twoich nieprzyjaciół, synowie twego ojca będą ci się kłaniać.
9 Ee Yuda, wewe ni mwana simba; unarudi toka mawindoni, mwanangu. Kama simba hunyemelea na kulala chini, kama simba jike: nani athubutuye kumwamsha?
Judo, szczenię lwie, wróciłeś od łupu, mój synu. Skłonił się i położył się jak lew i jak lwica. Któż go obudzi?
10 Fimbo ya ufalme haitaondoka kwa Yuda, wala fimbo ya mtawala kati ya miguu yake, hadi aje yeye ambaye milki ni yake, ambaye utii wa mataifa ni wake.
Nie będzie odjęte berło od Judy ani prawodawca spomiędzy jego nóg, aż przyjdzie Szylo i jemu będą posłuszne narody.
11 Atamfunga punda wake katika mzabibu, naye mwana-punda wake kwenye tawi lililo bora zaidi; atafua mavazi yake katika divai, majoho yake katika damu ya mizabibu.
Przywiąże do winorośli swoje oślę, a do wybornej winorośli – oślątko swojej oślicy. Wypierze w winie swoją szatę, a we krwi winogron – swoje odzienie.
12 Macho yake yatakuwa mekundu kwa divai, meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa.
Jego oczy czerwone od wina, a zęby białe od mleka.
13 “Zabuloni ataishi pwani ya bahari na kuwa bandari za kuegesha meli; mpaka wake utapanuka kuelekea Sidoni.
Zebulon [będzie] mieszkać na morskim brzegu, przy porcie okrętów, a jego granice [będą] aż do Sydonu.
14 “Isakari ni punda mwenye nguvu ambaye amelala kati ya mizigo yake.
Issachar [jak] osioł kościsty leżący między dwoma brzemionami.
15 Aonapo palivyo pazuri mahali pake pa kupumzika na jinsi nchi yake inavyopendeza, atainamisha bega lake kwenye mzigo na kujitolea kwa ajili ya kazi ngumu.
Zobaczył, że spoczynek jest dobry i ziemię, że [jest] urocza, nachylił swe ramię, by dźwigać, i stał się sługą składającym daninę.
16 “Dani atahukumu watu wake kwa haki kama mmoja wa makabila ya Israeli.
Dan będzie sądzić swój lud jako jedno z pokoleń Izraela.
17 Dani atakuwa nyoka kando ya barabara, nyoka mwenye sumu kando ya njia, yule aumaye visigino vya farasi ili yule ampandaye aanguke chali.
Dan będzie wężem na drodze, żmiją na ścieżce kąsającą końskie pięty, tak że jeździec spadnie do tyłu.
18 “Ee Bwana, nautafuta wokovu wako.
Oczekuję twego zbawienia, PANIE!
19 “Gadi atashambuliwa ghafula na kundi la washambuliaji, lakini yeye atawageukia na kuwashinda kabisa.
Gad będzie zwyciężony przez wojsko, ale on na koniec zwycięży.
20 “Chakula cha Asheri kitakuwa kinono, naye atatoa chakula kitamu kimfaacho mfalme.
Od Aszera [będzie] tłusty chleb, a on dostarczy przysmaków królewskich.
21 “Naftali ni kulungu jike aliyeachiwa huru azaaye watoto wazuri.
Neftali [jak] wypuszczona łania, mówiący piękne słowa.
22 “Yosefu ni mzabibu uzaao, mzabibu uzaao ulio kando ya chemchemi, ambao matawi yake hutanda ukutani.
Józef, latorośl płodna, latorośl płodna przy źródle, a [jej] szczepy rozchodzą się po murze.
23 Kwa uchungu wapiga mshale walimshambulia, wakampiga mshale kwa ukatili.
Choć napoili go goryczą i strzelali do niego, i nienawidzili go strzelcy;
24 Lakini upinde wake ulibaki imara, mikono yake ikatiwa nguvu, na mkono wa Mwenye Nguvu wa Yakobo, kwa sababu ya Mchungaji, Mwamba wa Israeli,
Jednak jego łuk został potężny i wzmocniły się ramiona jego rąk dzięki rękom mocnego [Boga] Jakuba, stamtąd pasterz i opoka Izraela.
25 kwa sababu ya Mungu wa baba yako, anayekusaidia, kwa sababu ya Mwenyezi, yeye anayekubariki kwa baraka za mbinguni juu, baraka za kilindi kilichoko chini, baraka za matitini na za tumbo la uzazi.
Od Boga twego ojca, który [będzie] cię wspomagał, i od Wszechmogącego, który ci pobłogosławi błogosławieństwami nieba z wysoka [i] błogosławieństwami głębin leżących na dole, [i] błogosławieństwami piersi i łona.
26 Baraka za baba yako ni kubwa kuliko baraka za milima ya kale, nyingi kuliko vilima vya kale. Baraka hizo zote na zikae juu ya kichwa cha Yosefu, juu ya paji la yule mkuu miongoni mwa ndugu zake.
Błogosławieństwa twego ojca będą mocniejsze niż błogosławieństwa moich przodków aż do granic pagórków wiecznych. Będą nad głową Józefa i nad wierzchem głowy odłączonego od swych braci.
27 “Benyamini ni mbwa mwitu mlafi mwenye njaa kuu; asubuhi hurarua mawindo yake, jioni hugawa nyara.”
Beniamin [jak] drapieżny wilk, rano będzie jeść zdobycz, a wieczorem będzie dzielił łupy.
28 Haya yote ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hivi ndivyo baba yao alivyowaambia alipowabariki, akimpa kila mmoja baraka inayomfaa.
Oto wszystkich dwanaście pokoleń Izraela i to, co im powiedział ich ojciec, gdy im błogosławił. Każdemu według jego błogosławieństwa błogosławił.
29 Ndipo alipowapa maelekezo haya: “Mimi niko karibu kukusanywa kwa watu wangu. Mnizike pamoja na baba zangu kwenye pango katika shamba la Efroni, Mhiti,
Potem im nakazał: Ja będę przyłączony do mojego ludu. Pogrzebcie mnie z moimi ojcami w jaskini, która jest na polu Efrona Chetyty;
30 pango lililoko katika shamba la Makpela, karibu na Mamre huko Kanaani, ambalo Abrahamu alinunua kwa ajili ya mahali pa kuzikia kutoka kwa Efroni, Mhiti, pamoja na shamba.
W jaskini, która [jest] na polu Makpela naprzeciwko Mamre w ziemi Kanaan. Kupił ją wraz z polem Abraham od Efrona Chetyty jako grób na własność.
31 Huko ndiko Abrahamu na Sara mkewe walikozikwa, huko akazikwa Isaki na Rebeka mkewe, na huko nilimzika Lea.
Tam pogrzebano Abrahama i jego żonę Sarę, tam pogrzebano Izaaka i jego żonę Rebekę. Tam też pogrzebałem Leę.
32 Shamba hilo na pango lililoko ndani yake lilinunuliwa kutoka kwa Wahiti.”
Pole to i jaskinię na nim kupiono od synów Cheta.
33 Baada ya Yakobo kumaliza kutoa maelekezo hayo kwa wanawe, akarudisha miguu yake kitandani, akapumua pumzi ya mwisho, na akakusanywa kwa watu wake.
A gdy Jakub przestał mówić do swoich synów, złożył swoje nogi na łoże i umarł, i został przyłączony do swego ludu.

< Mwanzo 49 >