< Kutoka 1 >

1 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli ambao walikwenda Misri na Yakobo, kila mmoja akiwa pamoja na jamaa yake:
Oto imiona synów Izraela, którzy przybyli z Jakubem do Egiptu; każdy przybył ze swoją rodziną:
2 Reubeni, Simeoni, Lawi na Yuda;
Ruben, Symeon, Lewi i Juda;
3 Isakari, Zabuloni na Benyamini;
Issachar, Zebulon i Beniamin;
4 Dani na Naftali, Gadi na Asheri.
Dan, Neftali, Gad i Aszer.
5 Wazao wote wa Yakobo walikuwa watu sabini; Yosefu alikuwa tayari yuko Misri.
A wszystkich dusz, które wyszły z bioder Jakuba, było siedemdziesiąt. Józef zaś [już] był w Egipcie.
6 Basi Yosefu na kaka zake wote na kizazi kile chote walikufa,
Potem umarli Józef, wszyscy jego bracia i całe to pokolenie.
7 lakini Waisraeli walikuwa wamezaana na kuongezeka sana, idadi yao ikawa kubwa mno, kwa hiyo wakaijaza nchi.
A synowie Izraela byli płodni, rozrodzili się, rozmnożyli i bardzo umacniali, a ziemia była ich pełna.
8 Kisha mfalme mpya ambaye hakufahamu habari za Yosefu akatawala Misri.
Wówczas nastał nad Egiptem nowy król, który nie znał Józefa.
9 Akawaambia watu wake, “Tazameni, Waisraeli wamekuwa wengi mno kwa idadi kutuliko sisi.
I powiedział do swego ludu: Oto lud synów Izraela stał się liczniejszy i potężniejszy od nas.
10 Njooni, ni lazima tuwashughulikie kwa uangalifu, la sivyo watazidi kuwa wengi zaidi, na ikiwa patatokea vita, watajiunga na adui zetu kupigana dhidi yetu na kuondoka katika nchi hii.”
Postąpmy więc z nimi mądrze, by się nie rozmnożyli, bo gdyby przyszła wojna, mogliby przyłączyć się do naszych wrogów i walczyć przeciwko nam, i opuścić ziemię.
11 Basi Wamisri wakaweka wasimamizi wa kuwasimamia na kuwatesa Waisraeli kwa kazi ngumu, nao wakajenga miji ya Pithomu na Ramesesi ya kuweka akiba ya Farao.
Ustanowiono więc nad nimi nadzorców, aby ich gnębili ciężarami. I [lud Izraela] zbudował dla faraona miasta na składy: Pitom i Ramzes.
12 Lakini walivyozidi kuteswa ndivyo walivyozidi kuongezeka na kuenea katika nchi; Wamisri wakawaogopa Waisraeli,
Ale im bardziej ich gnębili, tym bardziej się rozmnażali i rośli, tak że zatrwożyli się z powodu synów Izraela.
13 kwa hiyo wakawatumikisha kwa ukatili.
I Egipcjanie zmuszali synów Izraela do ciężkiej pracy.
14 Wakafanya maisha ya Waisraeli kuwa machungu kwa kufanya kazi ngumu ya kutengeneza lami na kufyatua matofali, na kazi zote za mashambani; katika kazi zao zote ngumu, Wamisri waliwatumia Waisraeli kwa ukatili.
I uprzykrzali [im] życie uciążliwą pracą przy glinie i przy cegłach, i przy każdej robocie na polu. Do wszelkiej pracy zmuszali ich bez litości.
15 Mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kimisri waliowazalisha wanawake wa Kiebrania, ambao majina yao ni Shifra na Pua,
I król Egiptu rozkazał hebrajskim położnym, z których jedna miała na imię Szifra, a druga Pua;
16 “Mtakapowazalisha wanawake wa Kiebrania, chunguzeni wanapojifungua. Ikiwa ni mtoto wa kiume, muueni, lakini ikiwa ni msichana, mwacheni aishi.”
Powiedział: Gdy będziecie przy porodach hebrajskich [kobiet] i zobaczycie, że urodził się syn, zabijcie go, a jeśli córka, niech zostanie przy życiu.
17 Lakini hao wakunga walimcha Mungu na hawakufanya kile mfalme wa Misri alichowaambia kufanya, bali wakawaacha watoto wa kiume waishi.
Lecz położne bały się Boga i nie robiły tak, jak im rozkazał król Egiptu, ale pozostawiały chłopców przy życiu.
18 Ndipo mfalme wa Misri akawaita hao wakunga, akawauliza, “Kwa nini mmefanya hivi? Mbona mmeacha watoto wa kiume waishi?”
Wtedy król Egiptu wezwał położne i powiedział do nich: Dlaczego tak postąpiłyście, że pozostawiłyście chłopców przy życiu?
19 Wakunga wakamjibu Farao, “Wanawake wa Kiebrania ni tofauti na wanawake wa Kimisri; wao wana nguvu, nao hujifungua watoto kabla wakunga hawajafika.”
Położne odpowiedziały faraonowi: Hebrajskie kobiety nie [są] takie jak egipskie [kobiety]. Są bowiem żywotne, rodzą wcześniej, zanim przyjdzie do nich położna.
20 Kwa hiyo Mungu akawatendea mema wakunga hao. Waisraeli wakaongezeka na kuendelea kuwa wengi zaidi.
I Bóg dobrze czynił tym położnym, a lud się mnożył i bardzo się wzmocnił.
21 Kwa vile hao wakunga walimcha Mungu, Mungu akawajalia kuwa na jamaa zao wenyewe.
A ponieważ położne bały się Boga, zbudował im domy.
22 Kisha Farao akatoa agizo hili kwa watu wake wote: “Kila mtoto wa kiume atakayezaliwa kwa Waebrania lazima atupwe katika Mto Naili, bali kila mtoto wa kike aachwe aishi.”
Wtedy faraon rozkazał całemu swemu ludowi: Każdego syna, który się urodzi, wrzućcie do rzeki, a każdą córkę pozostawcie przy życiu.

< Kutoka 1 >