< Mwanzo 36 >

1 Hivi ndivyo vizazi vya Esau (yaani Edomu).
To są dzieje rodu Ezawa, czyli Edomu.
2 Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti wa Eloni Mhiti, Oholibama binti wa Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi,
Ezaw pojął swoje żony z córek Kanaanu: Adę, córkę Elona Chetyty, Oholibamę, córkę Any, córki Sibeona Chiwwity;
3 pia akaoa Basemathi binti wa Ishmaeli, dada yake Nebayothi.
I Basmat, córkę Izmaela, siostrę Nebajota.
4 Ada akamzalia Esau Elifazi, Basemathi akamzaa Reueli,
I Ada urodziła Ezawowi Elifaza, a Basmat urodziła Rehuela.
5 Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wana wa Esau waliozaliwa kwake huko Kanaani.
Oholibama urodziła Jeusza, Jalama i Koracha. To [są] synowie Ezawa, którzy mu się urodzili w ziemi Kanaan.
6 Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike na wote wa nyumbani mwake, mifugo yake pamoja na wanyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata akiwa Kanaani, akahamia katika nchi iliyo mbali na Yakobo ndugu yake.
I Ezaw wziął swoje żony, synów, córki i wszystkich domowników, swoje stada, wszystkie bydła i całe swoje mienie, które zdobył w ziemi Kanaan, i odszedł od swego brata Jakuba do [innej] ziemi;
7 Mali zao zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba haikuwa rahisi wao kuishi pamoja, nchi waliyokuwa wakiishi isingewatosha wote kwa ajili ya mifugo yao.
Bo ich majątek był tak wielki, że nie mogli mieszkać razem, i ziemia, na której przebywali, nie mogła ich utrzymać z powodu [mnóstwa] ich stad.
8 Kwa hiyo Esau (ambaye ni Edomu) aliishi katika nchi ya kilima huko Seiri.
I Ezaw zamieszkał na górze Seir. Ezaw to Edom.
9 Hawa ndio wazao wa Esau, baba wa Waedomu, katika nchi ya kilima cha Seiri.
A to są dzieje rodu Ezawa, ojca Edomitów, na górze Seir.
10 Haya ndiyo majina ya wana wa Esau: Elifazi, mwana wa Esau ambaye mkewe Ada alimzalia; na Reueli, mwana wa Esau ambaye mkewe Basemathi alimzalia.
I to są imiona synów Ezawa: Elifaz, syn Ady, żony Ezawa, Rehuel, syn Basmat, żony Ezawa.
11 Wana wa Elifazi ni: Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.
Synami zaś Elifaza byli: Teman, Omar, Sefo, Gatam i Kenaz.
12 Elifazi mwana wa Esau alikuwa pia na suria aliyeitwa Timna, ambaye alimzalia Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Ada mke wa Esau.
A Timna była nałożnicą Elifaza, syna Ezawa, i urodziła Elifazowi Amaleka. To [są] synowie Ady, żony Ezawa.
13 Wana wa Reueli ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Basemathi mkewe Esau.
To [są] synowie Rehuela: Nachat, Zerach, Szamma i Mizza. Byli oni synami Basmat, żony Ezawa.
14 Wana wa Oholibama binti Ana, mkewe Esau, aliyekuwa mjukuu wa Sibeoni, aliomzalia Esau ni: Yeushi, Yalamu na Kora.
A ci byli synami żony Ezawa Oholibamy, córki Any, córki Sibeona. Urodziła ona Ezawowi Jeusza, Jalama i Koracha.
15 Hawa ndio waliokuwa wakuu miongoni mwa wazao wa Esau: Wakuu wa wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau ni: Temani, Omari, Sefo, Kenazi,
To [są] książęta spośród synów Ezawa, synowie Elifaza, pierworodnego Ezawa: książę Teman, książę Omar, książę Sefo, książę Kenaz.
16 Kora, Gatamu na Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wakuu waliotoka kwa Elifazi huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Ada.
Książę Korach, książę Gatam, książę Amalek. Ci książęta [pochodzą] z Elifaza, w ziemi Edom, to [są] synowie Ady.
17 Wakuu wa wana wa Reueli, mwana wa Esau ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa Reueli huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Basemathi mkewe Esau.
To [są] synowie Rehuela, syna Ezawa: książę Nachat, książę Zerach, książę Szamma, książę Mizza. Ci książęta [pochodzą] z Rehuela, w ziemi Edom. Oni [są] synami Basmat, żony Ezawa.
18 Wakuu wa wana wa Esau ambao mkewe Oholibama alimzalia ni: Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa mke wa Esau, Oholibama binti Ana.
A to [są] synowie Oholibamy, żony Ezawa: książę Jeusz, książę Jalam, książę Korach. Ci książęta [pochodzą] z Oholibamy, córki Any, żony Ezawa.
19 Hawa ndio waliokuwa wana wa Esau (ndiye Edomu), na hawa ndio waliokuwa wakuu wao.
To [są] synowie Ezawa, czyli Edom, i to [są] ich książęta.
20 Hawa ndio walikuwa wana wa Seiri, Mhori, waliokuwa wakiishi katika nchi ile: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
A to [są] synowie Seira, Choryty, mieszkańcy tej ziemi: Lotan, Szobal, Sibeon i Ana;
21 Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio wana wa Seiri huko Edomu waliokuwa wakuu kwa Wahori.
Diszon, Eser i Diszan. To [są] książęta Chorytów, synowie Seira w ziemi Edom.
22 Wana wa Lotani walikuwa: Hori na Homamu. Timna alikuwa dada yake Lotani.
Synami Lotana byli: Chori i Hemam; a siostrą Lotana była Tamna.
23 Wana wa Shobali walikuwa: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.
Synowie zaś Szobala: Alwan, Manachat, Ebal, Szefo i Onam.
24 Wana wa Sibeoni walikuwa: Aiya na Ana. Huyu Ana ndiye aligundua chemchemi ya maji moto jangwani alipokuwa akichunga punda za Sibeoni baba yake.
Synami Sibeona [są] Ajja i Ana. To ten Ana, który znalazł muły na pustyni, gdy pasł osły swego ojca Sibeona.
25 Watoto wa Ana walikuwa: Dishoni na Oholibama binti wa Ana.
A to [są] dzieci Any: Diszon i Oholibama, córka Any.
26 Wana wa Dishoni walikuwa: Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.
I synowie Diszona: Chemdan, Eszban, Jitran i Keran.
27 Wana wa Eseri walikuwa: Bilhani, Zaavani na Akani.
To są synowie Esera: Bilhan, Zaawan i Akan.
28 Wana wa Dishani walikuwa: Usi na Arani.
I synowie Diszana: Us i Aran.
29 Hawa ndio waliokuwa wakuu wa Wahori: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
To są książęta Chorytów: książę Lotan, książę Szobal, książę Sibeon, książę Ana.
30 Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Wahori, kufuatana na makundi yao, katika nchi ya Seiri.
Książę Diszon, książę Eser, książę Diszan. [Są] to książęta Chorytów, według ich księstw, w ziemi Seir.
31 Wafuatao ni wafalme waliotawala Edomu kabla ya mfalme yeyote wa Israeli kutawala:
To [są] królowie, którzy panowali w ziemi Edom, zanim panował król nad synami Izraela.
32 Bela mwana wa Beori alikuwa mfalme wa Edomu. Mji wake uliitwa Dinhaba.
W Edomie panował Bela, syn Beora, a nazwa jego miasta – Dinhaba.
33 Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.
I Bela umarł, a w jego miejsce panował Jobab, syn Zeracha z Bosry.
34 Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akawa mfalme baada yake.
Jobab umarł, a w jego miejsce panował Chuszam z ziemi Temanitów.
35 Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Avithi.
Chuszam umarł, a w jego miejsce panował Hadad, syn Bedada, który pokonał Midianitów na polu Moab, a nazwa jego miasta – Awit.
36 Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akawa mfalme baada yake.
Hadad umarł, a w jego miejsce panował Samla z Masreki.
37 Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ngʼambo ya Mto Frati akawa mfalme baada yake.
Samla umarł, a w jego miejsce panował Saul z Rechobot nad Rzeką.
38 Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akawa mfalme baada yake.
Saul umarł, a w jego miejsce panował Baalchanan, syn Akbora.
39 Baal-Hanani mwana wa Akbori alipofariki, Hadadi akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu.
Baalchanan, syn Akbora, umarł, a w jego miejsce panował Hadar, a nazwa jego miasta – Pahu, a imię jego żony [to] Mehetabel, [była to] córka Matredy, córki Mezahaba.
40 Hawa ndio wakuu waliotokana na Esau, kwa majina, kufuatana na koo zao na nchi zao: Timna, Alva, Yethethi,
To [są] imiona książąt Ezawa, według ich rodów i miejscowości i według ich imion: książę Timna, książę Alwa, książę Jetet.
41 Oholibama, Ela, Pinoni,
Książę Oholibama, książę Ela, książę Pinon.
42 Kenazi, Temani, Mibsari,
Książę Kenaz, książę Teman, książę Mibsar.
43 Magdieli na Iramu. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Edomu, kufuatana na makazi yao katika nchi waliyoimiliki. Huyu ndiye alikuwa Esau, baba wa Waedomu.
Książę Magdiel, książę Iram. To [są] książęta Edomu według miejsca ich zamieszkania w ziemi ich posiadłości. To [jest] Ezaw, ojciec Edomitów.

< Mwanzo 36 >