< Mwanzo 14 >

1 Wakati huu Amrafeli mfalme wa Shinari, Arioko mfalme wa Elasari, Kedorlaoma mfalme wa Elamu, na Tidali mfalme wa Goimu
Za dni Amrafela, króla Szinearu, Arioka, króla Ellasaru, Kedorlaomera, króla Elamu i Tidala, króla narodów;
2 kwa pamoja walikwenda kupigana vita dhidi ya Bera mfalme wa Sodoma, Birsha mfalme wa Gomora, Shinabu mfalme wa Adma, Shemeberi mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari).
Prowadzili wojnę z Berą, królem Sodomy, z Birszą, królem Gomory, z Szinabem, królem Admy, z Szemeberem, królem Seboim, i z królem miasta Beli, czyli Soaru.
3 Hawa wote waliotajwa mwishoni waliunganisha majeshi yao kutoka Bonde la Sidimu (yaani Bahari ya Chumvi).
Wszyscy oni połączyli się w dolinie Siddim, gdzie [dziś jest] Morze Słone.
4 Walikuwa wametawaliwa na Mfalme Kedorlaoma kwa miaka kumi na miwili, lakini mwaka wa kumi na tatu waliasi.
Dwanaście lat służyli Kedorlaomerowi, a w trzynastym roku zbuntowali się.
5 Mnamo mwaka wa kumi na nne, Mfalme Kedorlaoma na wafalme waliojiunga naye walikwenda kupigana na kuwashinda Warefai katika Ashtaroth-Kanaimu, Wazuzi katika Hamu, Waemi katika Shawe-Kiriathaimu,
I tak w roku czternastym nadciągnął Kedorlaomer z królami, którzy z nim [byli], i pobił Rafaitów w Asztarot-Karnaim, Zuzytów w Ham, Emitów w Szawe-Kiriataim;
6 na Wahori katika nchi ya kilima cha Seiri, hadi El-Parani karibu na jangwa.
I Chorytów na ich górze Seir aż do równiny Paran, która [jest] przy pustyni.
7 Kisha wakarudi wakaenda En-Misfati (yaani Kadeshi), wakashinda nchi yote ya Waamaleki, pamoja na Waamori waliokuwa wakiishi Hasason-Tamari.
Potem zawrócili i przybyli do En-Miszpat, czyli Kadesz, i wybili całą krainę Amalekitów, a także Amorytów mieszkających w Chasason-Tamar.
8 Ndipo mfalme wa Sodoma, mfalme wa Gomora, mfalme wa Adma, mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari) wakatoka kupanga majeshi yao kwenye Bonde la Sidimu
Wtedy wyruszyli król Sodomy oraz król Gomory, król Admy, król Seboim i król Beli, czyli Soaru, i ustawili się do bitwy z nimi w dolinie Siddim.
9 dhidi ya Kedorlaoma, mfalme wa Elamu, Tidali mfalme wa Goimu, Amrafeli mfalme wa Shinari, na Arioko mfalme wa Elasari, yaani wafalme wanne dhidi ya wafalme watano.
Z Kedorlaomerem, królem Elamu, Tidalem, królem narodów, Amrafelem, królem Szinearu i Ariokiem, królem Ellasaru – czterech królów przeciw pięciu.
10 Basi Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami, nao wafalme wa Sodoma na wa Gomora walipokimbia, baadhi ya watu walitumbukia huko na wengine wakakimbilia vilimani.
A dolina Siddim [była] pełna dołów ze smołą. Gdy uciekali królowie Sodomy i Gomory, wpadli tam, a pozostali uciekli na górę.
11 Wale wafalme wanne wakateka mali yote ya Sodoma na Gomora pamoja na vyakula vyao vyote, kisha wakaenda zao.
A [tamci] zabrali wszelkie mienie Sodomy i Gomory oraz całą ich żywność i odeszli.
12 Pia walimteka Loti mwana wa ndugu yake Abramu pamoja na mali zake, kwa kuwa alikuwa akiishi Sodoma.
Zabrali też Lota, bratanka Abrama, wraz z jego mieniem i odeszli. Mieszkał on bowiem w Sodomie.
13 Mtu mmoja aliyekuwa ametoroka akaja kumpa Abramu Mwebrania taarifa. Wakati huu Abramu alikuwa anaishi karibu na mialoni ya Mamre Mwamori, aliyekuwa ndugu yake Eshkoli na Aneri, ambao wote walikuwa wameungana na Abramu.
I przyszedł jeden zbieg, i oznajmił [to] Abramowi Hebrajczykowi, który mieszkał na równinach Mamrego Amoryty, brata Eszkola i Anera. Oni bowiem byli sprzymierzeni z Abramem.
14 Abramu alipopata habari kwamba jamaa yake amechukuliwa mateka, akawaita watu 318 wa nyumbani mwake waliokuwa wamefunzwa kupigana vita, wakawafuatilia hadi Dani.
Gdy Abram usłyszał, że jego brat został pojmany, wyprawił swoich trzystu osiemnastu wyszkolonych sług, urodzonych w jego domu, i ścigał [ich] aż do Dan.
15 Wakati wa usiku Abramu aliwagawa watu wake katika vikosi ili awashambulie, na akawafuatilia, akawafukuza hadi Hoba, kaskazini ya Dameski.
W nocy podzielili się, on i jego słudzy, [napadli] na nich i pobili ich. Potem ścigali ich aż do Choby, która [leży] po lewej stronie Damaszku.
16 Akarudisha mali zote, na akamrudisha Loti jamaa yake na mali zake, pamoja na wanawake na watu wengine.
Odzyskał całe mienie i odbił swego brata Lota wraz z jego mieniem, a także kobiety i ludzi.
17 Abramu aliporudi baada ya kumshinda Mfalme Kedorlaoma na wale wafalme waliojiunga naye, mfalme wa Sodoma akatoka kwenda kumlaki katika Bonde la Shawe (yaani Bonde la Mfalme).
Gdy wracał po pobiciu Kedorlaomera i królów, którzy z nim [byli], król Sodomy wyszedł mu na spotkanie w dolinie Szawe, czyli w dolinie królewskiej.
18 Ndipo Melkizedeki mfalme wa Salemu alipoleta mkate na divai. Alikuwa kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana.
A Melchisedek, król Salemu, wyniósł chleb i wino. [Był] on kapłanem Boga Najwyższego.
19 Naye akambariki Abramu, akisema, “Abarikiwe Abramu na Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na nchi.
I błogosławił mu, mówiąc: [Niech będzie] błogosławiony Abram [przez] Boga Najwyższego, właściciela nieba i ziemi.
20 Abarikiwe Mungu Aliye Juu Sana, ambaye amewaweka adui zako mkononi mwako.” Ndipo Abramu akampa Melkizedeki sehemu ya kumi ya kila kitu.
I [niech będzie] błogosławiony Bóg Najwyższy, który wydał twoich wrogów w twoje ręce. I [Abram] dał mu dziesięcinę ze wszystkiego.
21 Mfalme wa Sodoma akamwambia Abramu, “Nipe hao watu na hizo mali uchukue wewe mwenyewe.”
A król Sodomy powiedział do Abrama: Oddaj mi ludzi, a mienie weź dla siebie.
22 Lakini Abramu akamwambia mfalme wa Sodoma, “Nimeinua mkono wangu kwa Bwana, Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na dunia, na nimeapa
Lecz Abram odpowiedział królowi Sodomy: Podniosłem swą rękę do PANA Boga Najwyższego, właściciela nieba i ziemi;
23 kwamba sitapokea kitu chochote kilicho chako, hata kama ni uzi au gidamu ya kiatu, ili kamwe usije ukasema, ‘Nimemtajirisha Abramu.’
Że nie wezmę najmniejszej nitki ani rzemyka od obuwia, ani niczego, co należy do ciebie, abyś nie powiedział: Ja wzbogaciłem Abrama.
24 Sitapokea chochote, ila kile tu watu wangu walichokula na sehemu ambayo ni fungu la watu waliokwenda pamoja nami, ambao ni Aneri, Eshkoli na Mamre. Wao na wapewe fungu lao.”
Tylko to, co moi słudzy zjedli, oraz przydział mężczyzn, którzy poszli ze mną: Anera, Eszkola i Mamrego; niech oni wezmą swój przydział.

< Mwanzo 14 >