< Kutoka 37 >

1 Bezaleli akatengeneza Sanduku la mbao za mshita: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja na nusu.
I Besalel zrobił arkę z drewna akacjowego, [a] jej długość [była] na dwa i pół łokcia, a jej szerokość – na półtora łokcia, także jej wysokość to półtora łokcia.
2 Akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulizungushia ukingo wa dhahabu.
I pokrył ją szczerym złotem wewnątrz i na zewnątrz i zrobił wokół niej złotą listwę.
3 Akasubu pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
Odlał też do niej cztery złote pierścienie do czterech jej narożników: dwa pierścienie po jednej jej stronie, a dwa pierścienie po drugiej jej stronie.
4 Kisha akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
Zrobił również drążki z drewna akacjowego i pokrył je złotem.
5 Akaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
I włożył drążki w pierścienie po obu stronach arki, aby arka była na nich noszona.
6 Akatengeneza kifuniko cha upatanisho kwa dhahabu safi: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu.
Zrobił też przebłagalnię ze szczerego złota: jej długość [była] na dwa i pół łokcia, a jej szerokość – na półtora łokcia.
7 Kisha akatengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
Zrobił dwa cherubiny wykute ze złota na obu końcach przebłagalni.
8 Akatengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; akawatengeneza kuwa kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
Jednego cherubina na jednym końcu, a drugiego cherubina na drugim końcu. Zrobił cherubiny z przebłagalni wystające na obu jej końcach.
9 Makerubi hao walikuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao walielekeana, wakitazama hicho kifuniko.
A cherubiny miały rozpostarte skrzydła, z wierzchu zakrywały swymi skrzydłami przebłagalnię, a ich twarze były zwrócone ku sobie, twarze cherubinów były zwrócone ku przebłagalni.
10 Akatengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
Zrobił też stół z drewna akacjowego, jego długość [była] na dwa łokcie, jego szerokość – na [jeden] łokieć, a wysokość – na półtora łokcia.
11 Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
I pokrył go szczerym złotem, i zrobił wokół niego złotą listwę.
12 Pia akatengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na kuufanyia ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
Zrobił wokół niego też listwę o szerokości dłoni; zrobił również złote obramowanie wokoło tej listwy.
13 Akasubu pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na kuzifungia kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
I odlał do niego cztery złote pierścienie, i przyprawił je do czterech narożników u jego czterech nóg.
14 Pete hizo ziliwekwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko iliyotumika kuibebea hiyo meza.
Naprzeciwko tej listwy były pierścienie, przez które przewleczono drążki do noszenia stołu.
15 Mipiko hiyo ya kubebea meza ilitengenezwa kwa mti wa mshita, na ilikuwa imefunikwa kwa dhahabu.
Porobił drążki z drewna akacjowego do noszenia stołu i powlókł je złotem.
16 Vyombo vyote vya mezani vilitengenezwa kwa dhahabu safi: yaani sahani zake, masinia, na bakuli na bilauri zake kwa ajili ya kumiminia sadaka za vinywaji.
Zrobił też ze szczerego złota naczynia do stołu, misy do niego, czasze, przykrycia i kubki do nalewania.
17 Akatengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vilivyofanana na ua, matovu na maua vilikuwa kitu kimoja.
Zrobił także świecznik ze szczerego złota. Wykuł [ze złota ten] świecznik. Jego podstawa, ramiona, kielichy, gałki i kwiaty były z tej samej [bryły].
18 Matawi sita yalitokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
Sześć ramion wychodziło z obu boków: trzy ramiona z jednego boku świecznika i trzy ramiona z drugiego boku świecznika.
19 Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vilikuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yaliyotokeza kwenye kile kinara cha taa.
Trzy kielichy na kształt migdała na jednym ramieniu, [także] gałka i kwiat; i trzy kielichy na kształt migdała na drugim ramieniu, [także] gałka i kwiat. Tak [było] na wszystkich sześciu ramionach wychodzących ze świecznika.
20 Juu ya kinara chenyewe kulikuwepo na vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
Ale na samym świeczniku [były] cztery kielichy na kształt migdała, jego gałki i jego kwiaty.
21 Tovu moja lilikuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani, matawi sita kwa jumla.
I była gałka pod dwoma jego ramionami, także gałka [pod następnymi] dwoma jego ramionami, i znów gałka pod dwoma [innymi] jego ramionami. [Tak było] pod sześcioma ramionami wychodzącymi z niego.
22 Matovu na matawi yote yalikuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakiwa yamefuliwa kwa dhahabu safi.
Ich gałki i ramiona były z tej samej [bryły]. Wszystko to w całości było wykute ze szczerego złota.
23 Akatengeneza taa zake saba, na pia mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote kwa dhahabu safi.
Zrobił też do niego siedem lamp oraz szczypce i naczynia na popiół ze szczerego złota.
24 Akatengeneza kinara hicho cha taa pamoja na vifaa vyake vyote kutumia talanta moja ya dhahabu safi.
Zrobił go i wszystkie naczynia do niego z talentu szczerego złota.
25 Akatengeneza madhabahu ya kufukizia uvumba kwa mbao za mshita. Ilikuwa ya mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zilikuwa kitu kimoja nayo.
Zrobił także ołtarz do kadzenia z drewna akacjowego, na łokieć długi i na łokieć szeroki, kwadratowy, na dwa łokcie wysoki, a z niego wychodziły rogi.
26 Akafunika hayo madhabahu juu na pande zote na pia zile pembe zake kwa dhahabu safi, na akayafanyizia ukingo wa dhahabu kuizunguka.
I pokrył go szczerym złotem – jego wierzch, jego ściany wokoło i jego rogi. Zrobił też dokoła niego złotą listwę.
27 Akatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, zikiwa mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko iliyotumika kuyabebea madhabahu.
Zrobił dwa złote pierścienie do niego, pod jego listwą, na dwóch jego narożnikach, po obu bokach, przez które przewleczono drążki, aby był na nich noszony.
28 Akatengeneza mipiko kwa miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
Zrobił także drążki z drewna akacjowego i pokrył je złotem.
29 Pia akatengeneza mafuta matakatifu ya upako, na uvumba safi wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato.
Sporządził też olejek do świętego namaszczenia i wonne kadzidło, tak jak się robi wonności.

< Kutoka 37 >