< Danieli 11 >

1 Nami katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario Mmedi, nilisimama kumsaidia na kumlinda.)
ایستاده بودم تا او را استوار سازم وقوت دهم.۱
2 “Sasa basi, ninakuambia kweli: Wafalme watatu zaidi watatokea Uajemi, kisha atatokea mfalme wa nne, ambaye atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Wakati atakapokuwa amekwisha kujipatia nguvu kwa utajiri wake, atamchochea kila mmoja dhidi ya ufalme wa Uyunani.
«و الان تو را به راستی اعلام می‌نمایم. اینک سه پادشاه بعد از این در فارس خواهند برخاست و چهارمین از همه دولتمندتر خواهد بود و چون به‌سبب توانگری خویش قوی گردد همه را به ضد مملکت یونان برخواهد انگیخت.۲
3 Ndipo mfalme mwenye nguvu atatokea, ambaye atatawala kwa nguvu nyingi na kufanya anavyopenda.
وپادشاهی جبار خواهد برخاست و بر مملکت عظیمی سلطنت خواهد نمود و برحسب اراده خود عمل خواهد کرد.۳
4 Baada ya kujitokeza, milki yake itavunjwa na kugawanyika katika pande nne za mbinguni. Hautakwenda kwa wazao wake, wala hautakuwa na nguvu alizotumia, kwa sababu milki yake itangʼolewa na kupewa wengine.
و چون برخیزد سلطنت او شکسته خواهد شد و بسوی بادهای اربعه آسمان تقسیم خواهد گردید. اما نه به ذریت او ونه موافق استقلالی که او می‌داشت، زیرا که سلطنت او از ریشه‌کنده شده و به دیگران غیر ازایشان داده خواهد شد.۴
5 “Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja wa majemadari wake atakuwa na nguvu zaidi kuliko mfalme, naye atatawala ufalme wake mwenyewe kwa nguvu nyingi.
و پادشاه جنوب با یکی از سرداران خود قوی شده، بر او غلبه خواهدیافت و سلطنت خواهد نمود و سلطنت اوسلطنت عظیمی خواهد بود.۵
6 Baada ya miaka kadha, wataungana. Binti wa mfalme wa Kusini ataolewa kwa mfalme wa Kaskazini ili kuimarisha mapatano, lakini huyo binti nguvu zake hazitadumu; hata mfalme hatadumu wala nguvu zake. Katika siku hizo atafukuzwa, pamoja na hao wasindikizaji wake wa kifalme, watoto wake, na yeyote aliyemuunga mkono.
و بعد از انقضای سالها ایشان همداستان خواهند شد و دختر پادشاه جنوب نزد پادشاه شمال آمده، با اومصالحه خواهد نمود. لیکن قوت بازوی خود رانگاه نخواهد داشت و او و بازویش برقرار نخواهدماند و آن دختر و آنانی که او را خواهند‌آورد وپدرش و آنکه او را تقویت خواهد نمود در آن زمان تسلیم خواهند شد.۶
7 “Mmoja kutoka jamaa ya huyo binti atainuka na kuchukua nafasi yake. Atashambulia majeshi ya mfalme wa Kaskazini na kuingia katika ngome yake; atapigana dhidi yao naye atashinda.
«و کسی از رمونه های ریشه هایش در جای او خواهد برخاست و با لشکری آمده، به قلعه پادشاه شمال داخل خواهد شد و با ایشان (جنگ ) نموده، غلبه خواهد یافت.۷
8 Tena ataitwaa miungu yao, vinyago vyao vya chuma, na vitu vyao vya thamani vya fedha na dhahabu, na kuvichukua hadi Misri. Kwa miaka kadha atamwacha mfalme wa Kaskazini bila kumsumbua.
و خدایان وبتهای ریخته شده ایشان را نیز با ظروف گرانبهای ایشان از طلا و نقره به مصر به اسیری خواهد برد وسالهایی چند از پادشاه شمال دست خواهدبرداشت.۸
9 Kisha mfalme wa Kaskazini atashambulia nchi ya mfalme wa Kusini, lakini atarudi nyuma hadi kwenye nchi yake.
و به مملکت پادشاه جنوب داخل شده، باز به ولایت خود مراجعت خواهد نمود.۹
10 Wana wa mfalme wa Kaskazini watajiandaa kwa vita na kukusanya jeshi kubwa, ambalo litafagia nchi kama mafuriko yasiyozuilika na kuendelea na vita hadi kwenye ngome ya mfalme wa Kusini.
و پسرانش محاربه خواهند نمود و گروهی ازلشکرهای عظیم را جمع خواهند کرد و ایشان داخل شده، مثل سیل خواهند آمد و عبورخواهند نمود و برگشته، تا به قلعه او جنگ خواهند کرد.۱۰
11 “Kisha mfalme wa Kusini atatoka kwa ghadhabu na kupigana dhidi ya mfalme wa Kaskazini, ambaye ataunda jeshi kubwa, lakini litashindwa.
و پادشاه جنوب خشمناک شده، بیرون خواهد آمد و با وی یعنی با پادشاه شمال جنگ خواهد نمود و وی گروه عظیمی برپاخواهد کرد و آن گروه به‌دست وی تسلیم خواهند شد.۱۱
12 Wakati jeshi litakapokuwa limechukuliwa, mfalme wa Kusini atajawa na kiburi na atachinja maelfu mengi, hata hivyo hatabaki na ushindi.
و چون آن گروه برداشته شود، دلش مغرور خواهد شد و کرورها را هلاک خواهد ساخت اما قوت نخواهد یافت.۱۲
13 Kwa maana mfalme wa Kaskazini atakusanya jeshi jingine kubwa kuliko lile la kwanza; na baada ya miaka kadha, atasonga mbele na jeshi kubwa mno lililoandaliwa vizuri.
پس پادشاه شمال مراجعت کرده، لشکری عظیم تر ازاول برپا خواهد نمود و بعد از انقضای مدت سالهابا لشکر عظیمی و دولت فراوانی خواهد آمد.۱۳
14 “Katika nyakati hizo wengi watainuka dhidi ya mfalme wa Kusini. Watu wenye ghasia miongoni mwa watu wako mwenyewe wataasi ili kutimiza maono, lakini bila mafanikio.
و در آنوقت بسیاری با پادشاه جنوب مقاومت خواهند نمود و بعضی از ستمکیشان قوم توخویشتن را خواهند برافراشت تا رویا را ثابت نمایند اما ایشان خواهند افتاد.۱۴
15 Ndipo mfalme wa Kaskazini atakuja na kuuzunguka mji kwa majeshi, na kuuteka mji wa ngome. Majeshi ya Kusini yatakosa nguvu za kuyazuia; naam, hata vikosi vyao vya askari vilivyo bora zaidi, havitakuwa na nguvu ya kuwakabili.
«پس پادشاه شمال خواهد آمد و سنگرهابرپا نموده، شهر حصاردار را خواهد گرفت و نه افواج جنوب و نه برگزیدگان او یارای مقاومت خواهند داشت بلکه وی را هیچ یارای مقاومت نخواهد بود.۱۵
16 Huyo mvamia nchi atafanya apendavyo; hakuna yeyote atakayeweza kumpinga. Atajiimarisha katika Nchi ya Kupendeza, na atakuwa na uwezo wa kuiangamiza.
و آنکس که به ضد وی می‌آیدبرحسب رضامندی خود عمل خواهد نمود وکسی نخواهد بود که با وی مقاومت تواند نمودپس در فخر زمینها توقف خواهد نمود و آن به‌دست وی تلف خواهد شد.۱۶
17 Ataamua kuja na nguvu za ufalme wake wote na kufanya mapatano ya amani na mfalme wa Kusini. Naye atamtoa binti yake aolewe naye ili kuuangusha ufalme, lakini mipango yake haitafanikiwa wala kumsaidia.
و عزیمت خواهدنمود که با قوت تمامی مملکت خویش داخل بشود و با وی مصالحه خواهد کرد و او دختر زنان را به وی خواهد داد تا آن را هلاک کند. اما او ثابت نخواهد ماند و از آن او نخواهد بود.۱۷
18 Ndipo atabadili nia yake kupigana na nchi za pwani na ataziteka nyingi, lakini jemadari mmoja atakomesha ufidhuli wake na kurudisha ufidhuli wake juu yake.
پس بسوی جزیره‌ها توجه خواهد نمود و بسیاری ازآنها را خواهد گرفت. لیکن سرداری سرزنش او راباطل خواهد کرد، بلکه انتقام سرزنش او را از اوخواهد گرفت.۱۸
19 Baada ya hili atazigeukia ngome za nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena.
پس بسوی قلعه های زمین خویش توجه خواهد نمود اما لغزش خواهدخورد و افتاده، ناپدید خواهد شد.۱۹
20 “Atakayetawala baada yake atamtuma mtoza ushuru ili kudumisha fahari ya kifalme. Hata hivyo, baada ya miaka michache ataangamizwa, lakini si katika hasira wala katika vita.
«پس در جای او عاملی خواهد برخاست که جلال سلطنت را از میان خواهد برداشت لیکن در اندک ایامی او نیز هلاک خواهد شد نه به غضب و نه به جنگ.۲۰
21 “Atakayetawala baada yake atakuwa mtu wa kudharauliwa ambaye hajapewa heshima ya kifalme. Atauvamia ufalme wakati watu wake wanapojiona wako salama, naye atautwaa kwa hila.
و در جای او حقیری خواهدبرخاست اما جلال سلطنت را به وی نخواهند دادو او ناگهان داخل شده، سلطنت را با حیله هاخواهد گرفت.۲۱
22 Ndipo jeshi kubwa litafagiliwa mbele yake; jeshi pamoja na mkuu mmoja wa agano wataangamizwa.
و سیل افواج و رئیس عهد نیزاز حضور او رفته و شکسته خواهند شد.۲۲
23 Baada ya kufanya mapatano naye, atatenda kwa udanganyifu, na akitumia watu wachache tu ataingia madarakani.
و ازوقتی که ایشان با وی همداستان شده باشند او به حیله رفتار خواهد کرد و با جمعی قلیل افراشته وبزرگ خواهد شد.۲۳
24 Wakati majimbo yaliyo tajiri sana yanajiona salama, atayavamia, naye atafanikisha kile ambacho baba zake wala babu zake hawakuweza. Atagawa nyara, mateka na utajiri miongoni mwa wafuasi wake. Atafanya hila ya kupindua miji yenye maboma, lakini kwa muda mfupi tu.
و ناگهان به برومندترین بلادوارد شده، کارهایی را که نه پدرانش و نه پدران پدرانش کرده باشند بجا خواهد آورد و غارت وغنیمت و اموال را به ایشان بذل خواهد نمود و به ضد شهرهای حصاردار تدبیرها خواهد نمود، لیکن اندک زمانی خواهد بود.۲۴
25 “Pamoja na jeshi kubwa atachochea nguvu zake na ushujaa wake dhidi ya mfalme wa Kusini. Mfalme wa Kusini atafanya vita na jeshi lenye nguvu sana, lakini hataweza kusimama kwa sababu ya kwa hila zilizofanywa dhidi yake.
و قوت و دل خود را با لشکر عظیمی به ضد پادشاه جنوب برخواهد انگیخت و پادشاه جنوب با فوجی بسیار عظیم و قوی تهیه جنگ خواهد دید امایارای مقاومت نخواهد داشت زیرا که به ضد اوتدبیرها خواهند نمود.۲۵
26 Wale wanaokula kutoka kwenye ruzuku za mfalme watajaribu kumwangamiza; jeshi lake litafagiliwa mbali, nao wengi watakufa vitani.
و آنانی که خوراک او رامی خورند او را شکست خواهند داد و لشکر اوتلف خواهد شد و بسیاری کشته خواهند افتاد.۲۶
27 Wafalme hawa wawili, mioyo yao ikiwa imekusudia mabaya, wataketi kwenye meza moja na kudanganyana wao kwa wao, lakini pasipo faida, kwa sababu bado mwisho utakuja katika wakati ulioamriwa.
و دل این دو پادشاه به بدی مایل خواهد شد وبر یک سفره دروغ خواهند گفت، اما پیش نخواهد رفت زیرا که هنوز انتها برای وقت معین خواهد بود.۲۷
28 Mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake na utajiri mwingi, lakini atakuwa ameukaza moyo wake kinyume na agano takatifu. Atachukua hatua dhidi ya hilo agano, kisha atarudi nchi yake.
پس با اموال بسیار به زمین خودمراجعت خواهد کرد ودلش به ضد عهد مقدس جازم خواهد بود پس (برحسب اراده خود) عمل نموده، به زمین خود خواهد برگشت.۲۸
29 “Wakati ulioamriwa, atavamia tena Kusini, lakini wakati huu matokeo yake yatakuwa tofauti na yale ya wakati wa kwanza.
و دروقت معین مراجعت نموده، به زمین جنوب واردخواهد شد لیکن آخرش مثل اولش نخواهد بود.۲۹
30 Meli za nchi ya Kitimu zitampinga, naye atavunjika moyo. Ndipo atarudi nyuma na kutoa wazi hasira yake dhidi ya agano takatifu. Atarudi na kuonyesha fadhili kwa wale waliachao agano takatifu.
و کشتیها از کتیم به ضد او خواهند آمد لهذامایوس شده، رو خواهد تافت و به ضد عهدمقدس خشمناک شده، (برحسب اراده خود)عمل خواهد نمود و برگشته به آنانی که عهدمقدس را ترک می‌کنند توجه خواهد نمود.۳۰
31 “Majeshi yake yenye silaha yatainuka ili kunajisi ngome ya Hekalu, na kuondolea mbali sadaka ya kuteketezwa ya kila siku. Ndipo watalisimamisha chukizo la uharibifu lisababishalo ukiwa.
وافواج از جانب او برخاسته، مقدس حصین رانجس خواهند نمود و قربانی سوختنی دایمی راموقوف کرده، رجاست ویرانی را برپا خواهندداشت.۳۱
32 Kwa udanganyifu atapotosha wale walionajisi agano, lakini watu wanaomjua Mungu wao watampinga kwa uthabiti.
و آنانی را که به ضد عهد شرارت می‌ورزند با مکرها گمراه خواهد کرد. اما آنانی که خدای خویش را می‌شناسند قوی شده، (کارهای عظیم ) خواهند کرد.۳۲
33 “Wenye hekima watawafundisha wengi, ingawa kwa kitambo watauawa kwa upanga au kuchomwa moto, au kukamatwa au kufanywa mateka.
و حکیمان قوم بسیاری را تعلیم خواهند داد، لیکن ایامی چند به شمشیر و آتش و اسیری و تاراج خواهند افتاد.۳۳
34 Watakapoanguka, watapokea msaada kidogo, nao wengi ambao si waaminifu wataungana nao.
و چون بیفتند نصرت کمی خواهند یافت وبسیاری با فریب به ایشان ملحق خواهند شد.۳۴
35 Baadhi ya wenye hekima watajikwaa, ili waweze kusafishwa, kutakaswa na kufanywa wasio na waa mpaka wakati wa mwisho, kwa maana bado litakuja kwa wakati ulioamriwa.
وبعضی از حکیمان به جهت امتحان ایشان لغزش خواهند خورد که تا وقت آخر طاهر و سفیدبشوند زیرا که زمان معین هنوز نیست.۳۵
36 “Mfalme atafanya apendavyo. Atajikweza na kujitukuza juu ya kila mungu, naye atasema mambo ambayo hayajasikiwa dhidi ya Mungu wa miungu. Atafanikiwa hadi wakati wa ghadhabu utimie, kwa maana kile kilichokusudiwa lazima kitokee.
«و آن پادشاه موافق اراده خود عمل نموده، خویشتن را بر همه خدایان افراشته و بزرگ خواهد نمود و به ضد خدای خدایان سخنان عجیب خواهد گفت و تا انتهای غضب کامیاب خواهد شد زیرا آنچه مقدر است به وقوع خواهدپیوست.۳۶
37 Hataonyesha heshima kwa miungu ya baba zake au kwa yule aliyetamaniwa na wanawake, wala hatajali mungu yeyote, bali atajikweza mwenyewe juu yao wote.
و به خدای پدران خود و به فضیلت زنان اعتنا نخواهد نمود، بلکه بهیچ خدا اعتنانخواهد نمود زیرا خویشتن را از همه بلندترخواهد شمرد.۳۷
38 Badala ya kuwajali miungu, ataheshimu mungu wa ngome; mungu ambaye hakujulikana na baba zake ndiye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa vito vya thamani na zawadi za thamani kubwa.
و در جای او خدای قلعه‌ها راتکریم خواهد نمود و خدایی را که پدرانش او رانشناختند با طلا و نقره و سنگهای گرانبها ونفایس تکریم خواهد نمود.۳۸
39 Atashambulia ngome zenye nguvu mno kwa msaada wa mungu wa kigeni naye atawaheshimu sana wale watakaomkubali yeye. Atawafanya watawala juu ya watu wengi, na atagawa nchi kwa gharama.
و با قلعه های حصین مثل خدای بیگانه عمل خواهد نمود وآنانی را که بدو اعتراف نمایند در جلال ایشان خواهد افزود و ایشان را بر اشخاص بسیار تسلطخواهد داد و زمین را برای اجرت (ایشان ) تقسیم خواهد نمود.۳۹
40 “Katika wakati wa mwisho, mfalme wa Kusini atapigana naye vita, naye mfalme wa Kaskazini atamshambulia kwa magari ya vita, askari wapanda farasi, na idadi kubwa ya meli. Atavamia nchi nyingi na kuzikumba nchi hizo kama mafuriko.
«و در زمان آخر پادشاه جنوب با وی مقاتله خواهد نمود و پادشاه شمال با ارابه‌ها و سواران و کشتیهای بسیار مانند گردباد به ضد اوخواهد آمد و به زمینها سیلان کرده، از آنها عبورخواهد کرد.۴۰
41 Pia ataivamia Nchi ya Kupendeza. Nchi nyingi zitapinduliwa, bali Edomu, Moabu na viongozi wa Amoni wataokolewa kutoka mkono wake.
و به فخر زمینها وارد خواهد شدو بسیاری خواهند افتاد اما اینان یعنی ادوم وموآب و روسای بنی عمون از دست او خلاصی خواهند یافت.۴۱
42 Atapanua mamlaka yake juu ya nchi nyingi; hata Misri haitaepuka.
و دست خود را بر کشورهادراز خواهد کرد و زمین مصر رهایی نخواهدیافت.۴۲
43 Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na utajiri wote wa Misri, pamoja na Walibia na Wakushi kwa kujisalimisha.
و بر خزانه های طلا و نقره و بر همه نفایس مصر استیلا خواهد یافت و لبیان وحبشیان در موکب او خواهند بود.۴۳
44 Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamshtua, naye ataondoka kwa ghadhabu nyingi ili kuangamiza na kuharibu kabisa wengi.
لیکن اخباراز مشرق و شمال او را مضطرب خواهد ساخت، لهذا با خشم عظیمی بیرون رفته، اشخاص بسیاری را تباه کرده، بالکل هلاک خواهد ساخت.۴۴
45 Atasimika hema zake za ufalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa kupendeza. Hata hivyo, atafikia mwisho wake, wala hakuna yeyote atakayemsaidia.
و خیمه های ملوکانه خود را در کوه مجیدمقدس در میان دو دریا برپا خواهد نمود، لیکن به اجل خود خواهد رسید و معینی نخواهد داشت.۴۵

< Danieli 11 >