< Danieli 11 >

1 Nami katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario Mmedi, nilisimama kumsaidia na kumlinda.)
Mais moi aussi, la première année de Darius, le Mède, je l'assistai pour le soutenir et le fortifier.
2 “Sasa basi, ninakuambia kweli: Wafalme watatu zaidi watatokea Uajemi, kisha atatokea mfalme wa nne, ambaye atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Wakati atakapokuwa amekwisha kujipatia nguvu kwa utajiri wake, atamchochea kila mmoja dhidi ya ufalme wa Uyunani.
Maintenant donc je vais te découvrir la vérité. Voici, il s'élèvera encore trois rois pour les Perses, et le quatrième s'enrichira d'une plus grande richesse que tous; et quand il sera affermi dans sa richesse, il soulèvera contre lui tout, le royaume de la Grèce.
3 Ndipo mfalme mwenye nguvu atatokea, ambaye atatawala kwa nguvu nyingi na kufanya anavyopenda.
Mais il s'élèvera un roi vaillant, et il régnera avec une grande puissance, et il agira selon son bon plaisir.
4 Baada ya kujitokeza, milki yake itavunjwa na kugawanyika katika pande nne za mbinguni. Hautakwenda kwa wazao wake, wala hautakuwa na nguvu alizotumia, kwa sababu milki yake itangʼolewa na kupewa wengine.
Et quand il aura sa consistance, son royaume sera morcelé, et donné en part aux quatre vents des Cieux, mais non pas à ses descendants, ni avec la domination qu'il exerçait quand il dominait; car son empire sera déchiré et dévolu à d'autres à l'exclusion de ceux-là.
5 “Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja wa majemadari wake atakuwa na nguvu zaidi kuliko mfalme, naye atatawala ufalme wake mwenyewe kwa nguvu nyingi.
Et le roi du midi se consolidera, et parmi ses généraux l'un deviendra plus fort que lui, et régnera; et son règne aura une grande puissance.
6 Baada ya miaka kadha, wataungana. Binti wa mfalme wa Kusini ataolewa kwa mfalme wa Kaskazini ili kuimarisha mapatano, lakini huyo binti nguvu zake hazitadumu; hata mfalme hatadumu wala nguvu zake. Katika siku hizo atafukuzwa, pamoja na hao wasindikizaji wake wa kifalme, watoto wake, na yeyote aliyemuunga mkono.
Et au bout de plusieurs années ils s'allieront, et la fille du roi du midi entrera dans la maison du roi du septentrion, pour opérer un raccommodement. Mais elle ne soutiendra pas l'efficace de l'expédient, et il ne tiendra pas ni lui, ni son expédient; et elle sera livrée, elle et ceux qui l'auront introduite, et celui qui l'aura engendrée, et celui qui la possédera dans ces temps-là.
7 “Mmoja kutoka jamaa ya huyo binti atainuka na kuchukua nafasi yake. Atashambulia majeshi ya mfalme wa Kaskazini na kuingia katika ngome yake; atapigana dhidi yao naye atashinda.
Mais de la souche des racines de celle-ci surgira pour le remplacer un [prince] qui rejoindra l'armée, et pénétrera dans les forteresses du roi du septentrion, et il les traitera à discrétion, et il sera puissant.
8 Tena ataitwaa miungu yao, vinyago vyao vya chuma, na vitu vyao vya thamani vya fedha na dhahabu, na kuvichukua hadi Misri. Kwa miaka kadha atamwacha mfalme wa Kaskazini bila kumsumbua.
Et leurs dieux avec leurs images de fonte, avec leur vaisselle précieuse d'argent et d'or, seront emmenés par lui captifs en Egypte, puis pendant des années il n'inquiétera plus le roi du septentrion.
9 Kisha mfalme wa Kaskazini atashambulia nchi ya mfalme wa Kusini, lakini atarudi nyuma hadi kwenye nchi yake.
Et celui-ci marchera contre le royaume du roi du midi, mais il reviendra dans son pays.
10 Wana wa mfalme wa Kaskazini watajiandaa kwa vita na kukusanya jeshi kubwa, ambalo litafagia nchi kama mafuriko yasiyozuilika na kuendelea na vita hadi kwenye ngome ya mfalme wa Kusini.
Mais ses fils engageront les hostilités, et réuniront une quantité de forces considérables, et l'un fera une invasion, et inondera, et submergera, puis opérera sa retraite, et ils pousseront les hostilités jusqu'à sa place forte.
11 “Kisha mfalme wa Kusini atatoka kwa ghadhabu na kupigana dhidi ya mfalme wa Kaskazini, ambaye ataunda jeshi kubwa, lakini litashindwa.
Alors le roi du midi s'exaspérera, et se mettra en campagne, et lui livrera bataille, au roi du septentrion, et il mettra sur pied de grandes troupes, et les troupes seront placées sous sa conduite.
12 Wakati jeshi litakapokuwa limechukuliwa, mfalme wa Kusini atajawa na kiburi na atachinja maelfu mengi, hata hivyo hatabaki na ushindi.
Et ces troupes s'enorgueilliront, et son cœur deviendra superbe, et il mettra en déroute des myriades; cependant il ne prévaudra pas.
13 Kwa maana mfalme wa Kaskazini atakusanya jeshi jingine kubwa kuliko lile la kwanza; na baada ya miaka kadha, atasonga mbele na jeshi kubwa mno lililoandaliwa vizuri.
Puis, le roi du septentrion reviendra à la charge, et mettra de grandes troupes sur pied, plus nombreuses que les premières, et au bout de quelques années il viendra, arrivera avec une grande armée et beaucoup de bagages.
14 “Katika nyakati hizo wengi watainuka dhidi ya mfalme wa Kusini. Watu wenye ghasia miongoni mwa watu wako mwenyewe wataasi ili kutimiza maono, lakini bila mafanikio.
Et dans ces temps-là il y aura une grande levée contre le roi du midi, et des factieux de ton peuple se soulèveront, en accomplissement de la vision, et ils succomberont.
15 Ndipo mfalme wa Kaskazini atakuja na kuuzunguka mji kwa majeshi, na kuuteka mji wa ngome. Majeshi ya Kusini yatakosa nguvu za kuyazuia; naam, hata vikosi vyao vya askari vilivyo bora zaidi, havitakuwa na nguvu ya kuwakabili.
Et le roi du septentrion s'avancera, et il élèvera des terrasses, et s'emparera d'une ville forte; et les bataillons du midi ne tiendront pas, et sa troupe d'élite, elle ne sera pas de force à résister.
16 Huyo mvamia nchi atafanya apendavyo; hakuna yeyote atakayeweza kumpinga. Atajiimarisha katika Nchi ya Kupendeza, na atakuwa na uwezo wa kuiangamiza.
Et celui qui aura marché contre lui, agira selon son bon plaisir, et personne ne lui tiendra tête; et il s'établira dans le pays qui est l'ornement [de la terre]; et il sera maître de consommer.
17 Ataamua kuja na nguvu za ufalme wake wote na kufanya mapatano ya amani na mfalme wa Kusini. Naye atamtoa binti yake aolewe naye ili kuuangusha ufalme, lakini mipango yake haitafanikiwa wala kumsaidia.
Et il aura en vue d'arriver à la suprématie sur tout son royaume, et à un accommodement avec lui, et il en viendra à bout; et il lui donnera la fille de la femme, dans le but de le perdre; mais ceci ne se réalisera pas, et ne lui réussira point.
18 Ndipo atabadili nia yake kupigana na nchi za pwani na ataziteka nyingi, lakini jemadari mmoja atakomesha ufidhuli wake na kurudisha ufidhuli wake juu yake.
Et il ramènera ses regards sur les îles dont il prendra un grand nombre; mais un capitaine mettra fin à son propre opprobre, et fera en outre retomber sur lui l'opprobre qu'il avait reçu de lui.
19 Baada ya hili atazigeukia ngome za nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena.
Et il tournera ses regards du côté des forteresses de ses États, et il chancellera, et tombera, et ne sera plus trouvé.
20 “Atakayetawala baada yake atamtuma mtoza ushuru ili kudumisha fahari ya kifalme. Hata hivyo, baada ya miaka michache ataangamizwa, lakini si katika hasira wala katika vita.
Et à sa place s'élèvera un [prince] qui fera parcourir par l'exacteur l'ornement de l'empire, et quelque temps après il sera brisé, mais ce ne sera ni dans l'ardeur de la mêlée, ni dans le combat.
21 “Atakayetawala baada yake atakuwa mtu wa kudharauliwa ambaye hajapewa heshima ya kifalme. Atauvamia ufalme wakati watu wake wanapojiona wako salama, naye atautwaa kwa hila.
Et à sa place s'élèvera quelqu'un d'abject, et on ne lui aura point conféré la dignité royale, et il paraîtra inopinément, et s'emparera de la royauté au moyen d'adulations.
22 Ndipo jeshi kubwa litafagiliwa mbele yake; jeshi pamoja na mkuu mmoja wa agano wataangamizwa.
Et les bataillons qui viendront submergeant, seront submergés par lui, et rompus, de même qu'un prince confédéré.
23 Baada ya kufanya mapatano naye, atatenda kwa udanganyifu, na akitumia watu wachache tu ataingia madarakani.
Car dès le moment de sa jonction avec lui, il mettra l'artifice en œuvre, et il entrera en campagne, et il aura le dessus avec un petit nombre d'hommes.
24 Wakati majimbo yaliyo tajiri sana yanajiona salama, atayavamia, naye atafanikisha kile ambacho baba zake wala babu zake hawakuweza. Atagawa nyara, mateka na utajiri miongoni mwa wafuasi wake. Atafanya hila ya kupindua miji yenye maboma, lakini kwa muda mfupi tu.
A l'improviste il envahira, et même les portions les plus fertiles de la province, et il fera ce qui n'avait été fait ni par ses pères, ni par les pères de ses pères; il leur distribuera du butin et des dépouilles et des biens, et il formera aussi des projets contre les places fortes, et cela jusqu'à une certaine époque.
25 “Pamoja na jeshi kubwa atachochea nguvu zake na ushujaa wake dhidi ya mfalme wa Kusini. Mfalme wa Kusini atafanya vita na jeshi lenye nguvu sana, lakini hataweza kusimama kwa sababu ya kwa hila zilizofanywa dhidi yake.
Et il donnera essor à sa puissance et à son ambition contre le roi du midi avec de grandes forces, et le roi du midi s'engagera dans la guerre avec une armée considérable et extrêmement forte, mais il ne tiendra pas tête; car on formera contre lui des complots.
26 Wale wanaokula kutoka kwenye ruzuku za mfalme watajaribu kumwangamiza; jeshi lake litafagiliwa mbali, nao wengi watakufa vitani.
Ceux-là même qui seront nourris de ses mets délicats, le feront tomber sous leurs coups. Et son armée se débandera, et il tombera beaucoup de morts.
27 Wafalme hawa wawili, mioyo yao ikiwa imekusudia mabaya, wataketi kwenye meza moja na kudanganyana wao kwa wao, lakini pasipo faida, kwa sababu bado mwisho utakuja katika wakati ulioamriwa.
Et quant à ces deux rois, en leur cœur ils ne penseront qu'à se nuire; et à la même table ils parleront en mentant. Mais cela ne réussira pas, car la fin est remise à un terme.
28 Mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake na utajiri mwingi, lakini atakuwa ameukaza moyo wake kinyume na agano takatifu. Atachukua hatua dhidi ya hilo agano, kisha atarudi nchi yake.
Et il reviendra dans ses États avec de grands biens, et son cœur sera hostile à l'Alliance Sainte, et il agira, et il reviendra dans ses États.
29 “Wakati ulioamriwa, atavamia tena Kusini, lakini wakati huu matokeo yake yatakuwa tofauti na yale ya wakati wa kwanza.
A une époque fixe il marchera de nouveau contre le midi, mais à la fin il n'en sera pas comme au commencement.
30 Meli za nchi ya Kitimu zitampinga, naye atavunjika moyo. Ndipo atarudi nyuma na kutoa wazi hasira yake dhidi ya agano takatifu. Atarudi na kuonyesha fadhili kwa wale waliachao agano takatifu.
Car des navires de Cittim s'avanceront contre lui, et il aura peur, puis il tournera sa rage contre l'Alliance Sainte, et il agira, et derechef il s'entendra avec les déserteurs de l'Alliance Sainte.
31 “Majeshi yake yenye silaha yatainuka ili kunajisi ngome ya Hekalu, na kuondolea mbali sadaka ya kuteketezwa ya kila siku. Ndipo watalisimamisha chukizo la uharibifu lisababishalo ukiwa.
Et de par lui seront levés des bataillons qui profaneront le sanctuaire, la citadelle, et aboliront le sacrifice perpétuel, et mettront en place l'abomination du dévastateur.
32 Kwa udanganyifu atapotosha wale walionajisi agano, lakini watu wanaomjua Mungu wao watampinga kwa uthabiti.
Et par des flatteries il entraînera à la défection les impies [opposés] à l'Alliance; mais le peuple de ceux qui connaissent leur Dieu, prendra courage et agira.
33 “Wenye hekima watawafundisha wengi, ingawa kwa kitambo watauawa kwa upanga au kuchomwa moto, au kukamatwa au kufanywa mateka.
Et ceux qui dans le peuple ont de l'intelligence, en éclaireront plusieurs, mais ils succomberont à l'épée et aux flammes, à la captivité et au rapt pendant quelque temps.
34 Watakapoanguka, watapokea msaada kidogo, nao wengi ambao si waaminifu wataungana nao.
Et pendant qu'ils succomberont, ils seront aidés d'un faible secours, et plusieurs se joindront à eux par hypocrisie.
35 Baadhi ya wenye hekima watajikwaa, ili waweze kusafishwa, kutakaswa na kufanywa wasio na waa mpaka wakati wa mwisho, kwa maana bado litakuja kwa wakati ulioamriwa.
Et parmi les intelligents quelques-uns succomberont, afin qu'il se fasse parmi eux une épuration, et un triage, et une purification jusqu'au temps de la fin; car ceci encore est pour l'époque fixée.
36 “Mfalme atafanya apendavyo. Atajikweza na kujitukuza juu ya kila mungu, naye atasema mambo ambayo hayajasikiwa dhidi ya Mungu wa miungu. Atafanikiwa hadi wakati wa ghadhabu utimie, kwa maana kile kilichokusudiwa lazima kitokee.
Et le roi agira selon son bon plaisir, et il s'insurgera et se soulèvera contre toute divinité, et il proférera des choses monstrueuses contre le Dieu des dieux, et il aura du succès jusqu'à l'achèvement des vengeances; car l'arrêt recevra son exécution.
37 Hataonyesha heshima kwa miungu ya baba zake au kwa yule aliyetamaniwa na wanawake, wala hatajali mungu yeyote, bali atajikweza mwenyewe juu yao wote.
Il ne reconnaîtra pas même les dieux de ses pères, ni la Désirée des femmes, et il ne reconnaîtra aucun dieu quelconque, mais il les bravera tous:
38 Badala ya kuwajali miungu, ataheshimu mungu wa ngome; mungu ambaye hakujulikana na baba zake ndiye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa vito vya thamani na zawadi za thamani kubwa.
cependant il honorera le dieu des forteresses sur son piédestal, et au dieu inconnu de ses pères il rendra ses hommages avec de l'or et de l'argent, et des pierres précieuses et des joyaux.
39 Atashambulia ngome zenye nguvu mno kwa msaada wa mungu wa kigeni naye atawaheshimu sana wale watakaomkubali yeye. Atawafanya watawala juu ya watu wengi, na atagawa nchi kwa gharama.
C'est ainsi qu'il procédera contre les citadelles fortifiées, avec le dieu étranger; à quiconque le reconnaîtra, il accordera de grands honneurs, et il les établira souverains de plusieurs, et leur distribuera des terres en récompense.
40 “Katika wakati wa mwisho, mfalme wa Kusini atapigana naye vita, naye mfalme wa Kaskazini atamshambulia kwa magari ya vita, askari wapanda farasi, na idadi kubwa ya meli. Atavamia nchi nyingi na kuzikumba nchi hizo kama mafuriko.
Et au temps de la fin, le roi du midi se heurtera avec lui, et le roi du septentrion reviendra l'assaillir avec des chars, et de la cavalerie, et une flotte nombreuse, et il s'avancera dans les terres, et submergera et inondera.
41 Pia ataivamia Nchi ya Kupendeza. Nchi nyingi zitapinduliwa, bali Edomu, Moabu na viongozi wa Amoni wataokolewa kutoka mkono wake.
Il viendra aussi dans le pays qui est l'ornement [de la terre], et des multitudes succomberont; mais ceux-ci s'échapperont de ses mains, Edom et Moab, et l'élite des enfants d'Ammon.
42 Atapanua mamlaka yake juu ya nchi nyingi; hata Misri haitaepuka.
Et il portera la main sur les pays divers, et le pays d'Egypte n'échappera pas non plus.
43 Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na utajiri wote wa Misri, pamoja na Walibia na Wakushi kwa kujisalimisha.
Et il s'emparera des trésors d'or et d'argent, et de tout ce que l'Egypte a de précieux; et les Libyens et les Éthiopiens suivront ses pas.
44 Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamshtua, naye ataondoka kwa ghadhabu nyingi ili kuangamiza na kuharibu kabisa wengi.
Mais du levant et du nord des bruits viendront l'effrayer, et il se mettra en campagne avec un grand courroux, pour en massacrer et en détruire plusieurs.
45 Atasimika hema zake za ufalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa kupendeza. Hata hivyo, atafikia mwisho wake, wala hakuna yeyote atakayemsaidia.
Et il dressera ses tentes pareilles à des palais entre la mer et le mont du saint ornement, mais il marche à sa fin, et nul ne l'assiste.

< Danieli 11 >