< Danieli 11 >

1 Nami katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario Mmedi, nilisimama kumsaidia na kumlinda.)
Et moi, dans la première année de Darius le Mède, je me tenais auprès de lui pour le soutenir et le fortifier.
2 “Sasa basi, ninakuambia kweli: Wafalme watatu zaidi watatokea Uajemi, kisha atatokea mfalme wa nne, ambaye atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Wakati atakapokuwa amekwisha kujipatia nguvu kwa utajiri wake, atamchochea kila mmoja dhidi ya ufalme wa Uyunani.
Maintenant je vais te déclarer la vérité. Voici que trois rois se lèveront encore pour la Perse; le quatrième possédera de plus grandes richesses que tous les autres et, quand il sera puissant par ses richesses, il soulèvera tout contre le royaume de Javan.
3 Ndipo mfalme mwenye nguvu atatokea, ambaye atatawala kwa nguvu nyingi na kufanya anavyopenda.
Et il s'élèvera un roi vaillant, qui aura une grande puissance et fera ce qui lui plaira.
4 Baada ya kujitokeza, milki yake itavunjwa na kugawanyika katika pande nne za mbinguni. Hautakwenda kwa wazao wake, wala hautakuwa na nguvu alizotumia, kwa sababu milki yake itangʼolewa na kupewa wengine.
Dès qu'il se sera élevé, son royaume se brisera et sera divisé aux quatre vents du ciel, sans appartenir à ses descendants et sans avoir la même puissance qu'il avait eue; car son royaume sera déchiré, et il passera à d'autres qu'eux.
5 “Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja wa majemadari wake atakuwa na nguvu zaidi kuliko mfalme, naye atatawala ufalme wake mwenyewe kwa nguvu nyingi.
Le roi du Midi deviendra fort, ainsi qu'un de ses généraux, lequel deviendra plus fort que lui et sera puissant; sa puissance sera une grande puissance.
6 Baada ya miaka kadha, wataungana. Binti wa mfalme wa Kusini ataolewa kwa mfalme wa Kaskazini ili kuimarisha mapatano, lakini huyo binti nguvu zake hazitadumu; hata mfalme hatadumu wala nguvu zake. Katika siku hizo atafukuzwa, pamoja na hao wasindikizaji wake wa kifalme, watoto wake, na yeyote aliyemuunga mkono.
Au bout de quelques années, ils s'allieront, et la fille du roi du Midi viendra vers le roi du Septentrion pour établir un accord. Mais elle ne conservera pas l'appui d'un bras, car il ne tiendra pas, non plus que son propre bras; et elle sera livrée, elle et ceux qui l'avaient amenée, celui qui lui avait donné naissance et celui qui l'avait soutenue pendant quelque temps.
7 “Mmoja kutoka jamaa ya huyo binti atainuka na kuchukua nafasi yake. Atashambulia majeshi ya mfalme wa Kaskazini na kuingia katika ngome yake; atapigana dhidi yao naye atashinda.
Un des rejetons de ses racines s'élèvera à sa place; il viendra à l'armée, il entrera dans la forteresse du roi du Septentrion, il les traitera à son gré et il l'emportera.
8 Tena ataitwaa miungu yao, vinyago vyao vya chuma, na vitu vyao vya thamani vya fedha na dhahabu, na kuvichukua hadi Misri. Kwa miaka kadha atamwacha mfalme wa Kaskazini bila kumsumbua.
Leurs dieux mêmes, leurs images de fonte et leurs vases précieux d'argent et d'or, il les emmènera captifs en Egypte, et il prévaudra plusieurs années sur le roi du Septentrion.
9 Kisha mfalme wa Kaskazini atashambulia nchi ya mfalme wa Kusini, lakini atarudi nyuma hadi kwenye nchi yake.
Celui-ci entrera dans le royaume du Midi, et il s'en retournera dans son pays.
10 Wana wa mfalme wa Kaskazini watajiandaa kwa vita na kukusanya jeshi kubwa, ambalo litafagia nchi kama mafuriko yasiyozuilika na kuendelea na vita hadi kwenye ngome ya mfalme wa Kusini.
Mais ses fils s'armeront pour la guerre et rassembleront une grande multitude de troupes; l'un d'eux viendra, il inondera, il envahira, puis il reviendra, et poussera les hostilités contre la forteresse.
11 “Kisha mfalme wa Kusini atatoka kwa ghadhabu na kupigana dhidi ya mfalme wa Kaskazini, ambaye ataunda jeshi kubwa, lakini litashindwa.
Le roi du Midi s'irritera, il partira et combattra contre lui, contre le roi du Septentrion; il lèvera de grandes troupes, et la troupe du roi du Septentrion lui sera livrée.
12 Wakati jeshi litakapokuwa limechukuliwa, mfalme wa Kusini atajawa na kiburi na atachinja maelfu mengi, hata hivyo hatabaki na ushindi.
Devant la multitude levée contre lui, son courage s'élèvera; il en fera tomber des milliers, mais il n'en sera pas plus fort.
13 Kwa maana mfalme wa Kaskazini atakusanya jeshi jingine kubwa kuliko lile la kwanza; na baada ya miaka kadha, atasonga mbele na jeshi kubwa mno lililoandaliwa vizuri.
Car le roi du Septentrion rassemblera de nouveau des troupes plus nombreuses que les premières et, au bout d'un certain nombre d'années, il se mettra en marche avec une grande armée et un train considérable.
14 “Katika nyakati hizo wengi watainuka dhidi ya mfalme wa Kusini. Watu wenye ghasia miongoni mwa watu wako mwenyewe wataasi ili kutimiza maono, lakini bila mafanikio.
En ces temps-là beaucoup de gens s'élèveront contre le roi du Midi, et des hommes violents de ton peuple se lèveront pour accomplir la vision, et ils tomberont.
15 Ndipo mfalme wa Kaskazini atakuja na kuuzunguka mji kwa majeshi, na kuuteka mji wa ngome. Majeshi ya Kusini yatakosa nguvu za kuyazuia; naam, hata vikosi vyao vya askari vilivyo bora zaidi, havitakuwa na nguvu ya kuwakabili.
Le roi du Septentrion viendra, il élèvera des terrasses et prendra une ville fortifiée; les bras du Midi ne tiendront pas, non plus que sa troupe d'élite; il n'y aura pas de force pour résister.
16 Huyo mvamia nchi atafanya apendavyo; hakuna yeyote atakayeweza kumpinga. Atajiimarisha katika Nchi ya Kupendeza, na atakuwa na uwezo wa kuiangamiza.
Celui qui aura marché contre lui fera ce qui lui plaira, et personne ne tiendra devant lui; il s'arrêtera dans le glorieux pays, et la destruction sera dans sa main.
17 Ataamua kuja na nguvu za ufalme wake wote na kufanya mapatano ya amani na mfalme wa Kusini. Naye atamtoa binti yake aolewe naye ili kuuangusha ufalme, lakini mipango yake haitafanikiwa wala kumsaidia.
Il se décidera à venir avec la force de tout son royaume et il fera un arrangement avec lui; et il lui donnera une jeune fille pour amener sa ruine; mais cela ne réussira pas, et ce royaume ne sera point à lui.
18 Ndipo atabadili nia yake kupigana na nchi za pwani na ataziteka nyingi, lakini jemadari mmoja atakomesha ufidhuli wake na kurudisha ufidhuli wake juu yake.
Puis il se tournera vers les îles et en prendra beaucoup; mais un capitaine lui fera cesser son injure et, sans avoir reçu son injure, il la lui rendra.
19 Baada ya hili atazigeukia ngome za nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena.
Il se tournera vers les forteresses de son pays; mais il trébuchera, il tombera, et on ne le trouvera plus.
20 “Atakayetawala baada yake atamtuma mtoza ushuru ili kudumisha fahari ya kifalme. Hata hivyo, baada ya miaka michache ataangamizwa, lakini si katika hasira wala katika vita.
Un autre se tiendra à sa place, qui fera passer un exacteur dans le lieu qui est la gloire du royaume, et en quelques jours il sera brisé, et ce ne sera ni par la colère ni par la guerre.
21 “Atakayetawala baada yake atakuwa mtu wa kudharauliwa ambaye hajapewa heshima ya kifalme. Atauvamia ufalme wakati watu wake wanapojiona wako salama, naye atautwaa kwa hila.
A sa place se tiendra un homme méprisé, à qui on n'aura pas donné la dignité royale; il viendra sans bruit et s'emparera de la royauté par des intrigues.
22 Ndipo jeshi kubwa litafagiliwa mbele yake; jeshi pamoja na mkuu mmoja wa agano wataangamizwa.
Les forces de l'inondation seront submergées devant lui et seront brisées, et aussi le chef de l'alliance.
23 Baada ya kufanya mapatano naye, atatenda kwa udanganyifu, na akitumia watu wachache tu ataingia madarakani.
Sans tenir compte de l'alliance conclue avec lui, il agira de ruse, il se mettra en marche et aura le dessus avec peu de gens.
24 Wakati majimbo yaliyo tajiri sana yanajiona salama, atayavamia, naye atafanikisha kile ambacho baba zake wala babu zake hawakuweza. Atagawa nyara, mateka na utajiri miongoni mwa wafuasi wake. Atafanya hila ya kupindua miji yenye maboma, lakini kwa muda mfupi tu.
Il viendra sans bruit dans les plus riches provinces du pays; il fera ce que n'avaient pas fait ses pères, ni les pères de ses pères, il leur distribuera butin, dépouilles et richesses, et il formera des projets contre les forteresses, et cela jusqu'à un certain temps.
25 “Pamoja na jeshi kubwa atachochea nguvu zake na ushujaa wake dhidi ya mfalme wa Kusini. Mfalme wa Kusini atafanya vita na jeshi lenye nguvu sana, lakini hataweza kusimama kwa sababu ya kwa hila zilizofanywa dhidi yake.
Il excitera sa force et son courage contre le roi du Midi, à la tête d'une grande armée. Et le roi du Midi s'engagera dans la guerre avec une armée nombreuse et très forte; mais il ne tiendra pas, parce qu'on formera des complots contre lui.
26 Wale wanaokula kutoka kwenye ruzuku za mfalme watajaribu kumwangamiza; jeshi lake litafagiliwa mbali, nao wengi watakufa vitani.
Ceux qui mangent les mets de sa table le briseront, son armée se dissipera, et beaucoup d'hommes tomberont frappés de mort.
27 Wafalme hawa wawili, mioyo yao ikiwa imekusudia mabaya, wataketi kwenye meza moja na kudanganyana wao kwa wao, lakini pasipo faida, kwa sababu bado mwisho utakuja katika wakati ulioamriwa.
Les deux rois chercheront dans leur cœur à se nuire, et, à une même table, ils se diront des mensonges; mais cela ne réussira pas, car la fin ne viendra qu'au temps marqué.
28 Mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake na utajiri mwingi, lakini atakuwa ameukaza moyo wake kinyume na agano takatifu. Atachukua hatua dhidi ya hilo agano, kisha atarudi nchi yake.
Il retournera dans son pays avec de grandes richesses; son cœur médite le mal contre l'alliance sainte, et il le fait, et il rentre dans son pays.
29 “Wakati ulioamriwa, atavamia tena Kusini, lakini wakati huu matokeo yake yatakuwa tofauti na yale ya wakati wa kwanza.
Au temps marqué, il arrivera de nouveau dans le Midi; mais cette dernière campagne ne sera pas comme la première.
30 Meli za nchi ya Kitimu zitampinga, naye atavunjika moyo. Ndipo atarudi nyuma na kutoa wazi hasira yake dhidi ya agano takatifu. Atarudi na kuonyesha fadhili kwa wale waliachao agano takatifu.
Des navires de Céthim viendront contre lui et il perdra courage; il s'en retournera et il s'irritera contre l'alliance sainte; et il agira, et il s'entendra encore une fois avec ceux qui auront abandonné l'alliance.
31 “Majeshi yake yenye silaha yatainuka ili kunajisi ngome ya Hekalu, na kuondolea mbali sadaka ya kuteketezwa ya kila siku. Ndipo watalisimamisha chukizo la uharibifu lisababishalo ukiwa.
Des troupes envoyées par lui se tiendront là; elles profaneront le sanctuaire, la forteresse; elles feront cesser le sacrifice perpétuel et dresseront l'abomination du dévastateur.
32 Kwa udanganyifu atapotosha wale walionajisi agano, lakini watu wanaomjua Mungu wao watampinga kwa uthabiti.
Par des flatteries, il gagnera à l'idolâtrie les violateurs de l'alliance; mais le peuple de ceux qui connaissent leur Dieu tiendra ferme et agira.
33 “Wenye hekima watawafundisha wengi, ingawa kwa kitambo watauawa kwa upanga au kuchomwa moto, au kukamatwa au kufanywa mateka.
Ceux qui sont intelligents parmi le peuple instruiront la multitude; mais ils tomberont par l'épée et la flamme, par la captivité et le pillage, un certain temps.
34 Watakapoanguka, watapokea msaada kidogo, nao wengi ambao si waaminifu wataungana nao.
Pendant qu'ils tomberont ainsi, ils seront secourus d'un léger secours, et plusieurs se joindront à eux, mais avec hypocrisie.
35 Baadhi ya wenye hekima watajikwaa, ili waweze kusafishwa, kutakaswa na kufanywa wasio na waa mpaka wakati wa mwisho, kwa maana bado litakuja kwa wakati ulioamriwa.
Et parmi ces intelligents, il y en a qui tomberont, afin qu'ils soient éprouvés, purifiés et blanchis, jusqu'au temps de la fin, car on ne sera pas encore au terme fixé.
36 “Mfalme atafanya apendavyo. Atajikweza na kujitukuza juu ya kila mungu, naye atasema mambo ambayo hayajasikiwa dhidi ya Mungu wa miungu. Atafanikiwa hadi wakati wa ghadhabu utimie, kwa maana kile kilichokusudiwa lazima kitokee.
Le roi fera ce qui lui plaira, il s'élèvera et se grandira au-dessus de tout dieu, et contre le Dieu des dieux il dira des choses prodigieuses; et il prospérera, jusqu'à ce que la colère soit consommée; car ce qui est décrété doit s'accomplir.
37 Hataonyesha heshima kwa miungu ya baba zake au kwa yule aliyetamaniwa na wanawake, wala hatajali mungu yeyote, bali atajikweza mwenyewe juu yao wote.
Il n'aura égard ni aux dieux de ses pères, ni à la divinité chère aux femmes; il n'aura égard à aucun dieu; car il se grandira au-dessus de tout.
38 Badala ya kuwajali miungu, ataheshimu mungu wa ngome; mungu ambaye hakujulikana na baba zake ndiye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa vito vya thamani na zawadi za thamani kubwa.
Mais il honorera le dieu des forteresses en son lieu; le dieu que n'ont pas connu ses pères, il l'honorera avec de l'or, de l'argent, des pierres précieuses et des joyaux.
39 Atashambulia ngome zenye nguvu mno kwa msaada wa mungu wa kigeni naye atawaheshimu sana wale watakaomkubali yeye. Atawafanya watawala juu ya watu wengi, na atagawa nchi kwa gharama.
Il attaquera les remparts des forteresses avec le dieu étranger; ceux qui le reconnaîtront, il les comblera d'honneurs, il les fera dominer sur la multitude et leur distribuera des terres en récompense.
40 “Katika wakati wa mwisho, mfalme wa Kusini atapigana naye vita, naye mfalme wa Kaskazini atamshambulia kwa magari ya vita, askari wapanda farasi, na idadi kubwa ya meli. Atavamia nchi nyingi na kuzikumba nchi hizo kama mafuriko.
Au temps de la fin, le roi du Midi se heurtera avec lui. Le roi du Septentrion fondra sur lui, avec des chars et des cavaliers et de nombreux vaisseaux; il s'avancera dans les terres et passera en débordant.
41 Pia ataivamia Nchi ya Kupendeza. Nchi nyingi zitapinduliwa, bali Edomu, Moabu na viongozi wa Amoni wataokolewa kutoka mkono wake.
Il entrera dans le glorieux pays, et beaucoup tomberont sous ses coups, mais ceux-ci échapperont à sa main: Edom et Moab et la fleur des enfants d'Ammon.
42 Atapanua mamlaka yake juu ya nchi nyingi; hata Misri haitaepuka.
Il étendra la main sur les pays, et le pays d'Egypte n'échappera point.
43 Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na utajiri wote wa Misri, pamoja na Walibia na Wakushi kwa kujisalimisha.
Il se rendra maître de tous les trésors d'or et d'argent et de toutes les choses précieuses de l'Egypte; les Libyens et les Ethiopiens marcheront à sa suite.
44 Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamshtua, naye ataondoka kwa ghadhabu nyingi ili kuangamiza na kuharibu kabisa wengi.
Mais des nouvelles de l'orient et du septentrion viendront le troubler, et il partira avec une grande fureur pour détruire et exterminer une foule de gens.
45 Atasimika hema zake za ufalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa kupendeza. Hata hivyo, atafikia mwisho wake, wala hakuna yeyote atakayemsaidia.
Il dressera les tentes de son palais entre les mers, vers la montagne sainte et glorieuse. Puis il arrivera à sa fin, et personne ne le secourra.

< Danieli 11 >