< Danieli 11 >

1 Nami katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario Mmedi, nilisimama kumsaidia na kumlinda.)
Forsothe fro the firste yeer of Darius of Medei Y stood, that he schulde be coumfortid, and maad strong.
2 “Sasa basi, ninakuambia kweli: Wafalme watatu zaidi watatokea Uajemi, kisha atatokea mfalme wa nne, ambaye atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Wakati atakapokuwa amekwisha kujipatia nguvu kwa utajiri wake, atamchochea kila mmoja dhidi ya ufalme wa Uyunani.
And now Y schal telle to thee the treuthe. And lo! thre kyngis schulen stonde yit in Persis, and the fourthe schal be maad riche with ful many richessis ouer alle. And whanne he hath woxe strong bi hise richessis, he schal reise alle men ayens the rewme of Greece.
3 Ndipo mfalme mwenye nguvu atatokea, ambaye atatawala kwa nguvu nyingi na kufanya anavyopenda.
Forsothe a strong kyng schal rise, and shal be lord in greet power, and schal do that, that schal plese hym.
4 Baada ya kujitokeza, milki yake itavunjwa na kugawanyika katika pande nne za mbinguni. Hautakwenda kwa wazao wake, wala hautakuwa na nguvu alizotumia, kwa sababu milki yake itangʼolewa na kupewa wengine.
And whanne he schal stonde, his rewme schal be al to-brokun, and it schal be departid in to foure wyndis of heuene, but not in to hise eiris, nether bi the power of hym in which he was lord; for his rewme schal be to-rente, yhe, in to straungeris, outakun these.
5 “Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja wa majemadari wake atakuwa na nguvu zaidi kuliko mfalme, naye atatawala ufalme wake mwenyewe kwa nguvu nyingi.
And the kyng of the south schal be coumfortid; and of the princes of hym oon schal haue power aboue hym, and he schal be lord in power; for whi his lordschipe schal be myche.
6 Baada ya miaka kadha, wataungana. Binti wa mfalme wa Kusini ataolewa kwa mfalme wa Kaskazini ili kuimarisha mapatano, lakini huyo binti nguvu zake hazitadumu; hata mfalme hatadumu wala nguvu zake. Katika siku hizo atafukuzwa, pamoja na hao wasindikizaji wake wa kifalme, watoto wake, na yeyote aliyemuunga mkono.
And after the ende of yeeris `thei schulen be knyt in pees; and the douyter of the kyng of the south schal come to the kyng of the north, to make frenschipe. And sche schal not gete strengthe of arm, nether the seed of hir schal stonde; and sche schal be bitakun, and the yonglyngis of hir that brouyten hir, and he that coumfortide hir in tymes.
7 “Mmoja kutoka jamaa ya huyo binti atainuka na kuchukua nafasi yake. Atashambulia majeshi ya mfalme wa Kaskazini na kuingia katika ngome yake; atapigana dhidi yao naye atashinda.
And a plauntyng of the seed of the rootis of hir schal stonde; and he schal come with an oost, and schal entre in to the prouynce of the kyng of the north, and he schal mysuse hem, and he schal gete;
8 Tena ataitwaa miungu yao, vinyago vyao vya chuma, na vitu vyao vya thamani vya fedha na dhahabu, na kuvichukua hadi Misri. Kwa miaka kadha atamwacha mfalme wa Kaskazini bila kumsumbua.
ferthir more he schal gete both the goddis of hem, and grauun ymagis. Also he schal lede into Egipt preciouse vessels of gold, and of siluer, takun in batel. He schal haue the maistrie ayens the kyng of the north;
9 Kisha mfalme wa Kaskazini atashambulia nchi ya mfalme wa Kusini, lakini atarudi nyuma hadi kwenye nchi yake.
and the kyng of the south schal entre in to the rewme, and schal turne ayen to his lond.
10 Wana wa mfalme wa Kaskazini watajiandaa kwa vita na kukusanya jeshi kubwa, ambalo litafagia nchi kama mafuriko yasiyozuilika na kuendelea na vita hadi kwenye ngome ya mfalme wa Kusini.
Forsothe the sones of hym schulen be stirid to wraththe, and thei schulen gadere togidere a multitude of ful many coostis. And he schal come hastynge and flowynge, and he schal turne ayen, and schal be stirid, and schal bigynne batel with his strengthe.
11 “Kisha mfalme wa Kusini atatoka kwa ghadhabu na kupigana dhidi ya mfalme wa Kaskazini, ambaye ataunda jeshi kubwa, lakini litashindwa.
And the king of the south schal be stirid, and schal go out, and schal fiyte ayens the kyng of the north, and schal make redi a ful grete multitude; and the multitude schal be youun in his hond.
12 Wakati jeshi litakapokuwa limechukuliwa, mfalme wa Kusini atajawa na kiburi na atachinja maelfu mengi, hata hivyo hatabaki na ushindi.
And he schal take the multitude, and his herte schal be enhaunsid; and he schal caste doun many thousyndis, but he schal not haue the maistrie.
13 Kwa maana mfalme wa Kaskazini atakusanya jeshi jingine kubwa kuliko lile la kwanza; na baada ya miaka kadha, atasonga mbele na jeshi kubwa mno lililoandaliwa vizuri.
For the kyng of the north schal turne, and schal make redi a multitude, myche more than bifore; and in the ende of tymes and of yeeris he schal come hastynge with a ful greet oost, and with ful many richessis.
14 “Katika nyakati hizo wengi watainuka dhidi ya mfalme wa Kusini. Watu wenye ghasia miongoni mwa watu wako mwenyewe wataasi ili kutimiza maono, lakini bila mafanikio.
And in tho tymes many men schulen rise togidere ayens the kyng of the south; and the sones of trespassouris of thi puple schulen be enhaunsid, that thei fille the visioun, and thei schulen falle doun.
15 Ndipo mfalme wa Kaskazini atakuja na kuuzunguka mji kwa majeshi, na kuuteka mji wa ngome. Majeshi ya Kusini yatakosa nguvu za kuyazuia; naam, hata vikosi vyao vya askari vilivyo bora zaidi, havitakuwa na nguvu ya kuwakabili.
And the kyng of the north schal come, and schal bere togidere erthe, he schal take strongeste citees; and the armes of the south schulen not susteyne. And the chosun men therof schulen rise togidere, to ayenstonde, and strengthe schal not be.
16 Huyo mvamia nchi atafanya apendavyo; hakuna yeyote atakayeweza kumpinga. Atajiimarisha katika Nchi ya Kupendeza, na atakuwa na uwezo wa kuiangamiza.
And he schal come on hym, and schal do bi his wille; and noon schal be, that schal stonde ayens his face. And he schal stonde in the noble lond, and it schal be wastid in his hond.
17 Ataamua kuja na nguvu za ufalme wake wote na kufanya mapatano ya amani na mfalme wa Kusini. Naye atamtoa binti yake aolewe naye ili kuuangusha ufalme, lakini mipango yake haitafanikiwa wala kumsaidia.
And he schal sette his face, that he come to holde al the rewme of him, and he schal do riytful thingis with hym. And he schal yyue to hym the douyter of wymmen, to distrie hym; and it schal not stonde, and it schal not be his.
18 Ndipo atabadili nia yake kupigana na nchi za pwani na ataziteka nyingi, lakini jemadari mmoja atakomesha ufidhuli wake na kurudisha ufidhuli wake juu yake.
And he schal turne his face to ilis, and he schal take many ilis. And he schal make ceesse the prince of his schenschipe, and his schenschipe schal turne in to hym.
19 Baada ya hili atazigeukia ngome za nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena.
And he schal turne his face to the lordschip of his loond, and he schal snapere, and falle doun, and he schal not be foundun.
20 “Atakayetawala baada yake atamtuma mtoza ushuru ili kudumisha fahari ya kifalme. Hata hivyo, baada ya miaka michache ataangamizwa, lakini si katika hasira wala katika vita.
And the vilest and vnworthi to the kyngis onour schal stonde in the place of hym, and in fewe daies he schal be al to-brokun, not in woodnesse, nether in batel.
21 “Atakayetawala baada yake atakuwa mtu wa kudharauliwa ambaye hajapewa heshima ya kifalme. Atauvamia ufalme wakati watu wake wanapojiona wako salama, naye atautwaa kwa hila.
And a dispisid man schal stonde in the place of hym, and the onour of a kyng schal not be youun to hym; and he schal come priueli, and he schal gete the rewme bi gile.
22 Ndipo jeshi kubwa litafagiliwa mbele yake; jeshi pamoja na mkuu mmoja wa agano wataangamizwa.
And the armes of the fiytere schulen be ouercomun of his face, and schulen be al to-brokun, ferthermore and the duyk of boond of pees.
23 Baada ya kufanya mapatano naye, atatenda kwa udanganyifu, na akitumia watu wachache tu ataingia madarakani.
And after frenschipe with hym, he schal do gile. And he schal stie, and he schal ouercome with litil puple;
24 Wakati majimbo yaliyo tajiri sana yanajiona salama, atayavamia, naye atafanikisha kile ambacho baba zake wala babu zake hawakuweza. Atagawa nyara, mateka na utajiri miongoni mwa wafuasi wake. Atafanya hila ya kupindua miji yenye maboma, lakini kwa muda mfupi tu.
and he schal entre in to grete and riche citees, and he schal do thingis which hise fadris and the fadris of hise fadris diden not. He schal distrie the raueyns, and prei, and richessis of hem, and ayens most stidfast thouytis he schal take counsel, and this `vn to a tyme.
25 “Pamoja na jeshi kubwa atachochea nguvu zake na ushujaa wake dhidi ya mfalme wa Kusini. Mfalme wa Kusini atafanya vita na jeshi lenye nguvu sana, lakini hataweza kusimama kwa sababu ya kwa hila zilizofanywa dhidi yake.
And the strengthe of hym, and the herte of hym schal be stirid ayens the kyng of the south with a greet oost. And the king of the south schal be stirid to batel with many helpis and ful stronge; and thei schulen not stonde, for thei schulen take counsels ayens hym.
26 Wale wanaokula kutoka kwenye ruzuku za mfalme watajaribu kumwangamiza; jeshi lake litafagiliwa mbali, nao wengi watakufa vitani.
And thei that eeten breed with hym schulen al to-breke hym; and his oost schal be oppressid, and ful many men of hise schulen be slayn, and falle doun.
27 Wafalme hawa wawili, mioyo yao ikiwa imekusudia mabaya, wataketi kwenye meza moja na kudanganyana wao kwa wao, lakini pasipo faida, kwa sababu bado mwisho utakuja katika wakati ulioamriwa.
And the herte of twei kyngis schal be, that thei do yuel, and at o boord thei schulen speke leesyng, and thei schulen not profite; for yit the ende schal be in to an other tyme.
28 Mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake na utajiri mwingi, lakini atakuwa ameukaza moyo wake kinyume na agano takatifu. Atachukua hatua dhidi ya hilo agano, kisha atarudi nchi yake.
And he schal turne ayen in to his lond with many richessis, and his herte schal be ayens the hooli testament, and he schal do, and schal turne ayen in to his lond.
29 “Wakati ulioamriwa, atavamia tena Kusini, lakini wakati huu matokeo yake yatakuwa tofauti na yale ya wakati wa kwanza.
In tyme ordeyned he schal turne ayen, and schal come to the south, and the laste schal not be lijk the formere.
30 Meli za nchi ya Kitimu zitampinga, naye atavunjika moyo. Ndipo atarudi nyuma na kutoa wazi hasira yake dhidi ya agano takatifu. Atarudi na kuonyesha fadhili kwa wale waliachao agano takatifu.
And schippis with three ordris of ooris, and Romayns, schulen come on hym, and he schal be smytun. And he schal turne ayen, and schal haue indignacioun ayens the testament of seyntuarie, and he schal do. And he schal turne ayen, and he schal thenke ayens hem that forsoken the testament of seyntuarie.
31 “Majeshi yake yenye silaha yatainuka ili kunajisi ngome ya Hekalu, na kuondolea mbali sadaka ya kuteketezwa ya kila siku. Ndipo watalisimamisha chukizo la uharibifu lisababishalo ukiwa.
And armes of hym schulen stonde, and schulen defoule the seyntuarie, and schulen take awei the contynuel sacrifice, and schulen yyue abhomynacioun in to desolacioun.
32 Kwa udanganyifu atapotosha wale walionajisi agano, lakini watu wanaomjua Mungu wao watampinga kwa uthabiti.
And wickid men schulen feyne testament gilefuli; but the puple that knowith her God schal holde, and do.
33 “Wenye hekima watawafundisha wengi, ingawa kwa kitambo watauawa kwa upanga au kuchomwa moto, au kukamatwa au kufanywa mateka.
And tauyt men in the puple schulen teche ful many men, and schulen falle in swerd, and in flawme, and in to caitifte, and in to raueyn of daies.
34 Watakapoanguka, watapokea msaada kidogo, nao wengi ambao si waaminifu wataungana nao.
And whanne thei han feld doun, thei schulen be reisid bi a litil help; and ful many men schulen be applied to hym gilefuli.
35 Baadhi ya wenye hekima watajikwaa, ili waweze kusafishwa, kutakaswa na kufanywa wasio na waa mpaka wakati wa mwisho, kwa maana bado litakuja kwa wakati ulioamriwa.
And of lerud men schulen falle, that thei be wellid togidere, and be chosun, and be maad whijt til to a tyme determyned; for yit another tyme schal be.
36 “Mfalme atafanya apendavyo. Atajikweza na kujitukuza juu ya kila mungu, naye atasema mambo ambayo hayajasikiwa dhidi ya Mungu wa miungu. Atafanikiwa hadi wakati wa ghadhabu utimie, kwa maana kile kilichokusudiwa lazima kitokee.
And the kyng schal do bi his wille, and he schal be reisid, and magnefied ayens ech god, and ayens God of goddis he schal speke grete thingis; and he schal be dressid, til wrathfulnesse be fillid. For the determynynge is perfitli maad.
37 Hataonyesha heshima kwa miungu ya baba zake au kwa yule aliyetamaniwa na wanawake, wala hatajali mungu yeyote, bali atajikweza mwenyewe juu yao wote.
And he schal not arette the God of hise fadris, and he schal be in the coueitisis of wymmen, and he schal not charge ony of goddis, for he schal rise ayens alle thingis.
38 Badala ya kuwajali miungu, ataheshimu mungu wa ngome; mungu ambaye hakujulikana na baba zake ndiye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa vito vya thamani na zawadi za thamani kubwa.
Forsothe he schal onoure god of Maosym in his place, and he schal worschipe god, whom hise fadris knewen not, with gold, and siluer, and preciouse stoon, and preciouse thingis.
39 Atashambulia ngome zenye nguvu mno kwa msaada wa mungu wa kigeni naye atawaheshimu sana wale watakaomkubali yeye. Atawafanya watawala juu ya watu wengi, na atagawa nchi kwa gharama.
And he schal do that he make strong Moosym, with the alien god which he knew. And he schal multiplie glorie, and schal yyue power to hem in many thingis, and schal departe the lond at his wille.
40 “Katika wakati wa mwisho, mfalme wa Kusini atapigana naye vita, naye mfalme wa Kaskazini atamshambulia kwa magari ya vita, askari wapanda farasi, na idadi kubwa ya meli. Atavamia nchi nyingi na kuzikumba nchi hizo kama mafuriko.
And in the tyme determyned the kyng of the south schal fiyte ayens hym, and the kyng of the north schal come as a tempest ayens hym, in charis, and with knyytis, and in greet nauei.
41 Pia ataivamia Nchi ya Kupendeza. Nchi nyingi zitapinduliwa, bali Edomu, Moabu na viongozi wa Amoni wataokolewa kutoka mkono wake.
And he schal entre in to londis, and schal defoule hem; and he schal passe, and schal entre in to the gloriouse lond, and many schulen falle. Forsothe these londis aloone schulen be sauyd fro his hond, Edom, and Moab, and princes of the sones of Amon.
42 Atapanua mamlaka yake juu ya nchi nyingi; hata Misri haitaepuka.
And he schal sende his hond in to londis, and the lond of Egipt schal not ascape.
43 Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na utajiri wote wa Misri, pamoja na Walibia na Wakushi kwa kujisalimisha.
And he schal be lord of tresouris of gold, and of siluer, and in alle preciouse thingis of Egipt; also he schal passe bi Libie and Ethiopie.
44 Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamshtua, naye ataondoka kwa ghadhabu nyingi ili kuangamiza na kuharibu kabisa wengi.
And fame fro the eest and fro the north schal disturble hym; and he schal come with a greet multitude, to al to-breke, and to sle ful many men.
45 Atasimika hema zake za ufalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa kupendeza. Hata hivyo, atafikia mwisho wake, wala hakuna yeyote atakayemsaidia.
And he schal sette his tabernacle in Apheduo, bitwixe the sees, on the noble hil and hooli; and he schal come til to the heiythe therof, and no man schal helpe hym.

< Danieli 11 >