< Danieli 11 >

1 Nami katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario Mmedi, nilisimama kumsaidia na kumlinda.)
“As for me, during the first year that Darius was king, I helped and encouraged Michael.”
2 “Sasa basi, ninakuambia kweli: Wafalme watatu zaidi watatokea Uajemi, kisha atatokea mfalme wa nne, ambaye atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Wakati atakapokuwa amekwisha kujipatia nguvu kwa utajiri wake, atamchochea kila mmoja dhidi ya ufalme wa Uyunani.
[The angel also said], “And what I am going to reveal to you now will truly [happen]. There will be three more kings to rule Persia, [one after the other]. Then there will be a fourth king, who will be much richer than the others. As a result of [his giving] a lot of money [to people, they will enable him to] become very powerful. Then he will incite/persuade many nations [HYP] [to fight] against the kingdom of Greece.
3 Ndipo mfalme mwenye nguvu atatokea, ambaye atatawala kwa nguvu nyingi na kufanya anavyopenda.
Then a very powerful king will appear [in Greece]. He will rule over a very large empire, and he will do whatever he wants to do.
4 Baada ya kujitokeza, milki yake itavunjwa na kugawanyika katika pande nne za mbinguni. Hautakwenda kwa wazao wake, wala hautakuwa na nguvu alizotumia, kwa sababu milki yake itangʼolewa na kupewa wengine.
But when he has become very powerful, [he will die]. Then his kingdom will be divided into four parts. Kings who are not his descendants will rule, but they will not be as powerful as he was.
5 “Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja wa majemadari wake atakuwa na nguvu zaidi kuliko mfalme, naye atatawala ufalme wake mwenyewe kwa nguvu nyingi.
Then the King of Egypt [MTY] will become very powerful. But one of his army generals will become more powerful than he is, and he will rule a bigger area.
6 Baada ya miaka kadha, wataungana. Binti wa mfalme wa Kusini ataolewa kwa mfalme wa Kaskazini ili kuimarisha mapatano, lakini huyo binti nguvu zake hazitadumu; hata mfalme hatadumu wala nguvu zake. Katika siku hizo atafukuzwa, pamoja na hao wasindikizaji wake wa kifalme, watoto wake, na yeyote aliyemuunga mkono.
Several years later, the King of Egypt and the King of Syria will make an (alliance/agreement to help each other) [MTY]. The King of Syria will give his daughter to the King of Egypt to become his wife. But she will not be able to influence him [MTY] very long, and that woman, her husband, her child, and her servants will all be killed/assassinated.
7 “Mmoja kutoka jamaa ya huyo binti atainuka na kuchukua nafasi yake. Atashambulia majeshi ya mfalme wa Kaskazini na kuingia katika ngome yake; atapigana dhidi yao naye atashinda.
Soon after that, one of her relatives [MET] will become King [of Egypt]. His army will attack the army of Syria. They will enter the fortress of the soldiers of Syria and defeat them.
8 Tena ataitwaa miungu yao, vinyago vyao vya chuma, na vitu vyao vya thamani vya fedha na dhahabu, na kuvichukua hadi Misri. Kwa miaka kadha atamwacha mfalme wa Kaskazini bila kumsumbua.
They will return to Egypt, taking the statues of the gods [of the people of Syria] and many items made of silver and gold that had been dedicated to those gods. Then for several years his army will not attack [the army of] the King of Syria.
9 Kisha mfalme wa Kaskazini atashambulia nchi ya mfalme wa Kusini, lakini atarudi nyuma hadi kwenye nchi yake.
Then the army of the King of Syria will invade Egypt, but they will soon return to Syria.
10 Wana wa mfalme wa Kaskazini watajiandaa kwa vita na kukusanya jeshi kubwa, ambalo litafagia nchi kama mafuriko yasiyozuilika na kuendelea na vita hadi kwenye ngome ya mfalme wa Kusini.
However, the sons of the King of Syria will prepare to start a war, and they will gather a large army. That army will march [south] and spread all over [Israel] like a huge flood. They will attack a strong fortress [in the south of Israel].
11 “Kisha mfalme wa Kusini atatoka kwa ghadhabu na kupigana dhidi ya mfalme wa Kaskazini, ambaye ataunda jeshi kubwa, lakini litashindwa.
Then the King of Egypt, having become very angry, will march [with his army north] from Egypt and fight against the army of Syria. The King [of Syria] will gather together a very large army, but [the army of the King of Egypt] will defeat them.
12 Wakati jeshi litakapokuwa limechukuliwa, mfalme wa Kusini atajawa na kiburi na atachinja maelfu mengi, hata hivyo hatabaki na ushindi.
The King of Egypt will become very proud because of [his army] having killed a very large number of soldiers [from Syria], but his army will not continue to win battles.
13 Kwa maana mfalme wa Kaskazini atakusanya jeshi jingine kubwa kuliko lile la kwanza; na baada ya miaka kadha, atasonga mbele na jeshi kubwa mno lililoandaliwa vizuri.
The King of Syria will again gather together an army that will be bigger than the one that he had before. After a few years, he will again march [south on their way to Egypt] with a large army and a lot of equipment [for fighting battles].
14 “Katika nyakati hizo wengi watainuka dhidi ya mfalme wa Kusini. Watu wenye ghasia miongoni mwa watu wako mwenyewe wataasi ili kutimiza maono, lakini bila mafanikio.
At that time, many people in Egypt will rebel against their king. In order to fulfill a vision that [one of their leaders had seen], some violent/lawless people from your country [of Israel] will also rebel [in order to not be controlled by Egypt any more], but they will be defeated.
15 Ndipo mfalme wa Kaskazini atakuja na kuuzunguka mji kwa majeshi, na kuuteka mji wa ngome. Majeshi ya Kusini yatakosa nguvu za kuyazuia; naam, hata vikosi vyao vya askari vilivyo bora zaidi, havitakuwa na nguvu ya kuwakabili.
Then the King of Syria will come [south with his army] and pile up dirt against the walls of a city that is well protected, and they will [break through those walls and] they will capture the city. The soldiers from Egypt [who have come to defend that city], even the best troops, will not be strong enough to continue to fight.
16 Huyo mvamia nchi atafanya apendavyo; hakuna yeyote atakayeweza kumpinga. Atajiimarisha katika Nchi ya Kupendeza, na atakuwa na uwezo wa kuiangamiza.
So the King of Syria will do whatever he wants to, and no one will be able to oppose him. [His army] will occupy the glorious land [of Israel] and completely control/subdue it.
17 Ataamua kuja na nguvu za ufalme wake wote na kufanya mapatano ya amani na mfalme wa Kusini. Naye atamtoa binti yake aolewe naye ili kuuangusha ufalme, lakini mipango yake haitafanikiwa wala kumsaidia.
Then he will decide to march [south] with all the soldiers from his kingdom. He will make an alliance with the King [of Egypt] and in order that his own daughter will [help him to] destroy the kingdom of Egypt, he will give her to the King of Egypt to become his wife. But that plan will fail.
18 Ndipo atabadili nia yake kupigana na nchi za pwani na ataziteka nyingi, lakini jemadari mmoja atakomesha ufidhuli wake na kurudisha ufidhuli wake juu yake.
After that, the [army of] the King of Syria will attack the regions that are close to the [Mediterranean] Sea, and his [army] will conquer many of them. But [the army of] a leader from another country will defeat the army of Syria and will stop their king from continuing to be proud. He will do to the King of Syria what he deserved for being very insolent.
19 Baada ya hili atazigeukia ngome za nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena.
Then the King of Syria will return to the fortresses in his own land. But he will be defeated, and he will (die/be assassinated) [EUP] there.
20 “Atakayetawala baada yake atamtuma mtoza ushuru ili kudumisha fahari ya kifalme. Hata hivyo, baada ya miaka michache ataangamizwa, lakini si katika hasira wala katika vita.
Then another man will (succeed him/become king). That king will send one of his officers to oppress the people [in Jerusalem] by forcing them to pay big taxes, in order to get more money for his kingdom. But after a few years [HYP] that king will die, but he will not die as a result of people being angry with him or in a battle.
21 “Atakayetawala baada yake atakuwa mtu wa kudharauliwa ambaye hajapewa heshima ya kifalme. Atauvamia ufalme wakati watu wake wanapojiona wako salama, naye atautwaa kwa hila.
The next King of Syria will be an evil man who, [because he will not be the son of the previous king, ] will not have the right to become king. But he will come when people do not expect it, and he will become king by tricking the people.
22 Ndipo jeshi kubwa litafagiliwa mbele yake; jeshi pamoja na mkuu mmoja wa agano wataangamizwa.
When his army advances, they will attack any armies that oppose him and destroy those armies. They will also kill God’s Supreme Priest.
23 Baada ya kufanya mapatano naye, atatenda kwa udanganyifu, na akitumia watu wachache tu ataingia madarakani.
By making treaties/alliances with [the rulers of] other nations, he will deceive them, and he will become very powerful, even though he rules a nation that does not have a lot of people.
24 Wakati majimbo yaliyo tajiri sana yanajiona salama, atayavamia, naye atafanikisha kile ambacho baba zake wala babu zake hawakuweza. Atagawa nyara, mateka na utajiri miongoni mwa wafuasi wake. Atafanya hila ya kupindua miji yenye maboma, lakini kwa muda mfupi tu.
Suddenly his [army] will invade a province that is very wealthy, and they will do things that none of his ancestors did: they will capture in battles all kinds of possessions from the people whom they defeat. Then the king will divide those possessions among his friends. He will also plan [for his army] to attack fortresses [in Egypt], but only for a short time.
25 “Pamoja na jeshi kubwa atachochea nguvu zake na ushujaa wake dhidi ya mfalme wa Kusini. Mfalme wa Kusini atafanya vita na jeshi lenye nguvu sana, lakini hataweza kusimama kwa sababu ya kwa hila zilizofanywa dhidi yake.
He will courageously/boldly conscript/gather a large and powerful army to attack [the army of] the king of Egypt. But the King of Egypt will prepare to fight against them with a huge and powerful army. However, someone will deceive him, with the result that his plan will not be successful.
26 Wale wanaokula kutoka kwenye ruzuku za mfalme watajaribu kumwangamiza; jeshi lake litafagiliwa mbali, nao wengi watakufa vitani.
Even his most trusted advisors will plan to get rid of him. His army will be defeated and many of his soldiers will be killed.
27 Wafalme hawa wawili, mioyo yao ikiwa imekusudia mabaya, wataketi kwenye meza moja na kudanganyana wao kwa wao, lakini pasipo faida, kwa sababu bado mwisho utakuja katika wakati ulioamriwa.
Then the two [kings who both want to rule that area] will sit down at the same table and eat together, but they will both lie to each other. Neither of them will get what he wants, because it will not be the time [that God] has determined/set [for them to rule Egypt].
28 Mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake na utajiri mwingi, lakini atakuwa ameukaza moyo wake kinyume na agano takatifu. Atachukua hatua dhidi ya hilo agano, kisha atarudi nchi yake.
[The army of] the King [of Syria] will return to Syria, taking with them all the valuable things [that they had captured]. The king will be determined to get rid of the Supreme Priest of the Jewish people. He will do what he wants to [in Israel], and then return to his own country.
29 “Wakati ulioamriwa, atavamia tena Kusini, lakini wakati huu matokeo yake yatakuwa tofauti na yale ya wakati wa kwanza.
When it is the time that God has decided, the King of Syria [and his army] will invade Egypt again. But this time he will not be successful like he was before.
30 Meli za nchi ya Kitimu zitampinga, naye atavunjika moyo. Ndipo atarudi nyuma na kutoa wazi hasira yake dhidi ya agano takatifu. Atarudi na kuonyesha fadhili kwa wale waliachao agano takatifu.
The army of Rome will come in ships and oppose his army and cause him to be afraid. So he will be very angry, and [with his army] he will return [to Israel] and try to get rid of the Supreme Priest. The King of Syria will do what those who have abandoned the Jewish religion advise/want him to do for them.
31 “Majeshi yake yenye silaha yatainuka ili kunajisi ngome ya Hekalu, na kuondolea mbali sadaka ya kuteketezwa ya kila siku. Ndipo watalisimamisha chukizo la uharibifu lisababishalo ukiwa.
Some of his soldiers will do things to (defile the temple/cause the temple to become unholy for them). They will prevent the priests from offering sacrifices each day, and they will put [in the temple] something that is disgusting/abominable.
32 Kwa udanganyifu atapotosha wale walionajisi agano, lakini watu wanaomjua Mungu wao watampinga kwa uthabiti.
By deceiving those who have abandoned the Jewish religion, he will persuade them to (become his supporters/help him to do what he wants to do). But those who are devoted to their God will firmly oppose them.
33 “Wenye hekima watawafundisha wengi, ingawa kwa kitambo watauawa kwa upanga au kuchomwa moto, au kukamatwa au kufanywa mateka.
And wise [Israeli] leaders will teach others also. But for a while, some of those wise leaders will be killed in battles, and some will be burned to death, and some will be robbed, and some will be put in prison.
34 Watakapoanguka, watapokea msaada kidogo, nao wengi ambao si waaminifu wataungana nao.
While God’s people are being persecuted, some people will help them a little bit, although some of those who help them will not do it sincerely.
35 Baadhi ya wenye hekima watajikwaa, ili waweze kusafishwa, kutakaswa na kufanywa wasio na waa mpaka wakati wa mwisho, kwa maana bado litakuja kwa wakati ulioamriwa.
Some of those wise leaders will be killed [EUP], but as a result the others will be purified [DOU]. This suffering will continue until it is the time [that God] has appointed [for it to] end.
36 “Mfalme atafanya apendavyo. Atajikweza na kujitukuza juu ya kila mungu, naye atasema mambo ambayo hayajasikiwa dhidi ya Mungu wa miungu. Atafanikiwa hadi wakati wa ghadhabu utimie, kwa maana kile kilichokusudiwa lazima kitokee.
The King [of Syria] will do what he wants to. He will boast and say that he is greater than any god. He will even revile the Supreme God. He will be able to do what he wants until the time that [God] punishes [MTY] him. [God] will accomplish what he has planned.
37 Hataonyesha heshima kwa miungu ya baba zake au kwa yule aliyetamaniwa na wanawake, wala hatajali mungu yeyote, bali atajikweza mwenyewe juu yao wote.
The [King of Syria] will ignore the god that his ancestors worshiped and the god that many women love. He will ignore every god, because he will think that he is greater than all of them.
38 Badala ya kuwajali miungu, ataheshimu mungu wa ngome; mungu ambaye hakujulikana na baba zake ndiye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa vito vya thamani na zawadi za thamani kubwa.
But he will honor the god who [people think] protects fortresses. That is a god whom his ancestors did not honor. And he will give gold, silver, (jewels/very valuable stones) and other expensive gifts to that god.
39 Atashambulia ngome zenye nguvu mno kwa msaada wa mungu wa kigeni naye atawaheshimu sana wale watakaomkubali yeye. Atawafanya watawala juu ya watu wengi, na atagawa nchi kwa gharama.
He will ask that god (OR, people who worship a god) from another country to help him to defend his fortresses. He will greatly honor those who allow him [to be their ruler]. He will appoint [some of] them to important positions in the government; and to reward them, he will give them some land.
40 “Katika wakati wa mwisho, mfalme wa Kusini atapigana naye vita, naye mfalme wa Kaskazini atamshambulia kwa magari ya vita, askari wapanda farasi, na idadi kubwa ya meli. Atavamia nchi nyingi na kuzikumba nchi hizo kama mafuriko.
But when his time [to rule] is almost ended, [the army of] the King of Egypt will attack his [army]. The [army of the] King of Syria will fight against them furiously [SIM]. [His soldiers will be driving] chariots and [riding on] horses and [traveling in] many ships. His army will invade many countries and [spread all over those countries] like a flood [MET].
41 Pia ataivamia Nchi ya Kupendeza. Nchi nyingi zitapinduliwa, bali Edomu, Moabu na viongozi wa Amoni wataokolewa kutoka mkono wake.
They will invade the glorious land [of Israel] and kill [EUP] tens of thousands of people. But the people of the Edom people-group and the people of the Moab people-group and the people of the Ammon people-group who are still alive will escape.
42 Atapanua mamlaka yake juu ya nchi nyingi; hata Misri haitaepuka.
When the army of Syria invades other countries, even the people of Egypt will be defeated.
43 Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na utajiri wote wa Misri, pamoja na Walibia na Wakushi kwa kujisalimisha.
The army of Syria will take away from Egypt gold, silver, and other valuable items. The people of Libya and Ethiopia will allow [the King of Syria] to rule over them.
44 Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamshtua, naye ataondoka kwa ghadhabu nyingi ili kuangamiza na kuharibu kabisa wengi.
But he will become very frightened/alarmed when he hears reports about what is happening in the east and in the north. So he will become very angry, and send his army to fight furiously and kill many [of their enemies].
45 Atasimika hema zake za ufalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa kupendeza. Hata hivyo, atafikia mwisho wake, wala hakuna yeyote atakayemsaidia.
The [King of Syria] will set up his royal tents in the area between the [Mediterranean] Sea and the hill [in Jerusalem] on which the temple (exists/was built). But he will be killed there, because there will be no one to help him.”

< Danieli 11 >