< Danieli 11 >

1 Nami katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario Mmedi, nilisimama kumsaidia na kumlinda.)
“And so, from the first year of Darius the Mede, I stood firm, so that he might be reinforced and strengthened.
2 “Sasa basi, ninakuambia kweli: Wafalme watatu zaidi watatokea Uajemi, kisha atatokea mfalme wa nne, ambaye atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Wakati atakapokuwa amekwisha kujipatia nguvu kwa utajiri wake, atamchochea kila mmoja dhidi ya ufalme wa Uyunani.
And now I will announce to you the truth. Behold, up to a certain point, three kings will stand in Persia, and the fourth will be exceedingly enriched in power above them all. And when he has grown strong by his resources, he will stir up all against the kingdom of Greece.
3 Ndipo mfalme mwenye nguvu atatokea, ambaye atatawala kwa nguvu nyingi na kufanya anavyopenda.
But there will rise up a strong king, and he will rule with great power, and he will do what he pleases.
4 Baada ya kujitokeza, milki yake itavunjwa na kugawanyika katika pande nne za mbinguni. Hautakwenda kwa wazao wake, wala hautakuwa na nguvu alizotumia, kwa sababu milki yake itangʼolewa na kupewa wengine.
And when he has been firmly established, his kingdom will be shattered and will be divided towards the four winds of the heaven, but not to his posterity, nor according to his power with which he ruled. For his kingdom will be torn to pieces, even for the outsiders who have been expelled from these.
5 “Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja wa majemadari wake atakuwa na nguvu zaidi kuliko mfalme, naye atatawala ufalme wake mwenyewe kwa nguvu nyingi.
And the king of the South will be reinforced, yet one of his leaders will prevail over him, and he will rule with riches, for great is his domain.
6 Baada ya miaka kadha, wataungana. Binti wa mfalme wa Kusini ataolewa kwa mfalme wa Kaskazini ili kuimarisha mapatano, lakini huyo binti nguvu zake hazitadumu; hata mfalme hatadumu wala nguvu zake. Katika siku hizo atafukuzwa, pamoja na hao wasindikizaji wake wa kifalme, watoto wake, na yeyote aliyemuunga mkono.
And after the end of years, they will form a federation, and the daughter of the king of the South will come to the king of the North to make friendship, but she will not obtain the strength of arms, neither will her offspring stand firm, and she will be handed over, along with those who brought her, her young men, and those who comforted her in these times.
7 “Mmoja kutoka jamaa ya huyo binti atainuka na kuchukua nafasi yake. Atashambulia majeshi ya mfalme wa Kaskazini na kuingia katika ngome yake; atapigana dhidi yao naye atashinda.
And a transplant from the germination of her roots will stand up, and he will come with an army, and will enter into the province of the king of the North, and he will abuse them, and will hold it fast.
8 Tena ataitwaa miungu yao, vinyago vyao vya chuma, na vitu vyao vya thamani vya fedha na dhahabu, na kuvichukua hadi Misri. Kwa miaka kadha atamwacha mfalme wa Kaskazini bila kumsumbua.
And, in addition, he will carry away captive into Egypt their gods, and their graven images, and likewise their precious vessels of gold and silver. He will prevail against the king of the North.
9 Kisha mfalme wa Kaskazini atashambulia nchi ya mfalme wa Kusini, lakini atarudi nyuma hadi kwenye nchi yake.
And the king of the South will enter into the kingdom, and will return to his own land.
10 Wana wa mfalme wa Kaskazini watajiandaa kwa vita na kukusanya jeshi kubwa, ambalo litafagia nchi kama mafuriko yasiyozuilika na kuendelea na vita hadi kwenye ngome ya mfalme wa Kusini.
But his sons will be challenged, and they will assemble a multitude of very many forces. And he will arrive rushing and overflowing. And he will be turned back, and he will be enraged, and he will join the battle in his redness.
11 “Kisha mfalme wa Kusini atatoka kwa ghadhabu na kupigana dhidi ya mfalme wa Kaskazini, ambaye ataunda jeshi kubwa, lakini litashindwa.
And the king of the South, having being challenged, will go forth and will fight against the king of the North, and he will prepare an exceedingly great multitude, and a multitude will be given into his hand.
12 Wakati jeshi litakapokuwa limechukuliwa, mfalme wa Kusini atajawa na kiburi na atachinja maelfu mengi, hata hivyo hatabaki na ushindi.
And he will seize a multitude, and his heart will be exalted, and he will cast down many thousands, but he will not prevail.
13 Kwa maana mfalme wa Kaskazini atakusanya jeshi jingine kubwa kuliko lile la kwanza; na baada ya miaka kadha, atasonga mbele na jeshi kubwa mno lililoandaliwa vizuri.
For the king of the North will change strategy and will prepare a multitude much greater than before, and at the end of times and years, he will rush forward with a great army and exceedingly great resources.
14 “Katika nyakati hizo wengi watainuka dhidi ya mfalme wa Kusini. Watu wenye ghasia miongoni mwa watu wako mwenyewe wataasi ili kutimiza maono, lakini bila mafanikio.
And in those times, many will rise up against the king of the South. And likewise the sons of the deceivers among your people will extol themselves, so as to fulfill the vision, and they will collapse.
15 Ndipo mfalme wa Kaskazini atakuja na kuuzunguka mji kwa majeshi, na kuuteka mji wa ngome. Majeshi ya Kusini yatakosa nguvu za kuyazuia; naam, hata vikosi vyao vya askari vilivyo bora zaidi, havitakuwa na nguvu ya kuwakabili.
And the king of the North will arrive and will transport siege works, and he will seize the most fortified cities. And the arms of the South will not withstand him, and his elect will rise up to resist, but the strength will not.
16 Huyo mvamia nchi atafanya apendavyo; hakuna yeyote atakayeweza kumpinga. Atajiimarisha katika Nchi ya Kupendeza, na atakuwa na uwezo wa kuiangamiza.
And when he arrives, he will do just as he pleases, and there will be none who stand against his face. And he will stand in the illustrious land, and it will be consumed by his hand.
17 Ataamua kuja na nguvu za ufalme wake wote na kufanya mapatano ya amani na mfalme wa Kusini. Naye atamtoa binti yake aolewe naye ili kuuangusha ufalme, lakini mipango yake haitafanikiwa wala kumsaidia.
And he will set his face to strive to hold his entire kingdom, and he will make fair conditions with him. And he will give him a daughter among women, so as to overthrow it. But she will not stand, neither will she be for him.
18 Ndipo atabadili nia yake kupigana na nchi za pwani na ataziteka nyingi, lakini jemadari mmoja atakomesha ufidhuli wake na kurudisha ufidhuli wake juu yake.
And he will turn his face towards the islands, and he will seize many. And he will cause the leader of his reproach to cease, and his reproach will be turned around for him.
19 Baada ya hili atazigeukia ngome za nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena.
And he will turn his face to the empire of his own land, and he will strike, and will overthrow, but he will not succeed.
20 “Atakayetawala baada yake atamtuma mtoza ushuru ili kudumisha fahari ya kifalme. Hata hivyo, baada ya miaka michache ataangamizwa, lakini si katika hasira wala katika vita.
And there will stand up in his place one who is most worthless and unworthy of kingly honor. And in a short time, he will be worn out, but not in fury, nor in battle.
21 “Atakayetawala baada yake atakuwa mtu wa kudharauliwa ambaye hajapewa heshima ya kifalme. Atauvamia ufalme wakati watu wake wanapojiona wako salama, naye atautwaa kwa hila.
And there will stand up in his place the despicable one, and he will not be assigned the honor of a king. And he will arrive in secret, and he will obtain the kingdom by deceitfulness.
22 Ndipo jeshi kubwa litafagiliwa mbele yake; jeshi pamoja na mkuu mmoja wa agano wataangamizwa.
And the arms of the fighting will be assaulted before his face and will be shattered, and, in addition, the leader of the federation.
23 Baada ya kufanya mapatano naye, atatenda kwa udanganyifu, na akitumia watu wachache tu ataingia madarakani.
And, after making friends, he will trick him, and he will go up and will overcome with a small people.
24 Wakati majimbo yaliyo tajiri sana yanajiona salama, atayavamia, naye atafanikisha kile ambacho baba zake wala babu zake hawakuweza. Atagawa nyara, mateka na utajiri miongoni mwa wafuasi wake. Atafanya hila ya kupindua miji yenye maboma, lakini kwa muda mfupi tu.
And he will enter into rich and resourceful cities, and he will do what his fathers never did, nor his fathers’ fathers. He will scatter their spoils, and their prey, and their riches, and will form a plan against the most steadfast, and this until a time.
25 “Pamoja na jeshi kubwa atachochea nguvu zake na ushujaa wake dhidi ya mfalme wa Kusini. Mfalme wa Kusini atafanya vita na jeshi lenye nguvu sana, lakini hataweza kusimama kwa sababu ya kwa hila zilizofanywa dhidi yake.
And his strength and his heart will be enraged against the king of the South with a great army. And the king of the South will be provoked into going to war by having many allies and exceedingly good circumstances, and yet these will not stand, for they will form plans against him.
26 Wale wanaokula kutoka kwenye ruzuku za mfalme watajaribu kumwangamiza; jeshi lake litafagiliwa mbali, nao wengi watakufa vitani.
And those who eat bread with him will crush him, and his army will be suppressed, and very many will die, having been executed.
27 Wafalme hawa wawili, mioyo yao ikiwa imekusudia mabaya, wataketi kwenye meza moja na kudanganyana wao kwa wao, lakini pasipo faida, kwa sababu bado mwisho utakuja katika wakati ulioamriwa.
And the heart of two kings will be similar, to do harm, and they will speak lies at one table, but they will not succeed, because as yet the end is for another time.
28 Mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake na utajiri mwingi, lakini atakuwa ameukaza moyo wake kinyume na agano takatifu. Atachukua hatua dhidi ya hilo agano, kisha atarudi nchi yake.
And he will return to his land with many resources. And his heart will be against the holy testament, and he will act, and he will return to his own land.
29 “Wakati ulioamriwa, atavamia tena Kusini, lakini wakati huu matokeo yake yatakuwa tofauti na yale ya wakati wa kwanza.
At the appointed time, he will return, and he will approach the South, but the latter time will not be like the former.
30 Meli za nchi ya Kitimu zitampinga, naye atavunjika moyo. Ndipo atarudi nyuma na kutoa wazi hasira yake dhidi ya agano takatifu. Atarudi na kuonyesha fadhili kwa wale waliachao agano takatifu.
And the Greek warships and the Romans will come upon him, and he will be pierced, and will retreat, and will have scorn against the testament of the sanctuary, and he will act. And he will return and will consult their adversaries, who have forsaken the covenant of the sanctuary.
31 “Majeshi yake yenye silaha yatainuka ili kunajisi ngome ya Hekalu, na kuondolea mbali sadaka ya kuteketezwa ya kila siku. Ndipo watalisimamisha chukizo la uharibifu lisababishalo ukiwa.
And arms will take his side, and they will pollute the sanctuary of the strength, and they will take away the continual sacrifice and will replace it with the abomination of desolation.
32 Kwa udanganyifu atapotosha wale walionajisi agano, lakini watu wanaomjua Mungu wao watampinga kwa uthabiti.
And the impious within the testament will imitate deceitfully, but the people, knowing their God, will persevere and will act.
33 “Wenye hekima watawafundisha wengi, ingawa kwa kitambo watauawa kwa upanga au kuchomwa moto, au kukamatwa au kufanywa mateka.
And the teachers among the people will teach many, but they will be ruined by the sword, and by fire, and by captivity, and by assaults for many days.
34 Watakapoanguka, watapokea msaada kidogo, nao wengi ambao si waaminifu wataungana nao.
And when they have fallen, they will be supported with a little help, but many will apply to them deceitfully.
35 Baadhi ya wenye hekima watajikwaa, ili waweze kusafishwa, kutakaswa na kufanywa wasio na waa mpaka wakati wa mwisho, kwa maana bado litakuja kwa wakati ulioamriwa.
And some of the learned will be ruined, that they may be kindled and chosen and purified, up to the predetermined time, because there will be still another time.
36 “Mfalme atafanya apendavyo. Atajikweza na kujitukuza juu ya kila mungu, naye atasema mambo ambayo hayajasikiwa dhidi ya Mungu wa miungu. Atafanikiwa hadi wakati wa ghadhabu utimie, kwa maana kile kilichokusudiwa lazima kitokee.
And the king will act according to his will, and he will be lifted up and will be extolled against every god. And he will speak great things against the God of gods, and he will control, until the passion is completed. Once accomplished, the limit is reached with certainty.
37 Hataonyesha heshima kwa miungu ya baba zake au kwa yule aliyetamaniwa na wanawake, wala hatajali mungu yeyote, bali atajikweza mwenyewe juu yao wote.
And he will give no thought to the God of his fathers, and he will be in the desire of women, and he will not attend to any gods, because he will rise up against all things.
38 Badala ya kuwajali miungu, ataheshimu mungu wa ngome; mungu ambaye hakujulikana na baba zake ndiye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa vito vya thamani na zawadi za thamani kubwa.
But he will do homage to the god Maozim in his place, and, a god whom his fathers did not know, he will worship with gold, and silver, and precious stones, and costly things.
39 Atashambulia ngome zenye nguvu mno kwa msaada wa mungu wa kigeni naye atawaheshimu sana wale watakaomkubali yeye. Atawafanya watawala juu ya watu wengi, na atagawa nchi kwa gharama.
And he will act to reinforce Maozim with an alien god, of whom he has become aware, and he will increase their glory, and will give them power over many, and he will distribute land for free.
40 “Katika wakati wa mwisho, mfalme wa Kusini atapigana naye vita, naye mfalme wa Kaskazini atamshambulia kwa magari ya vita, askari wapanda farasi, na idadi kubwa ya meli. Atavamia nchi nyingi na kuzikumba nchi hizo kama mafuriko.
And, at the predetermined time, the king of the South will fight against him, and the king of the North will come against him like a tempest, with chariots, and with horsemen, and with a great fleet, and he will enter into the lands, and will crush and pass through.
41 Pia ataivamia Nchi ya Kupendeza. Nchi nyingi zitapinduliwa, bali Edomu, Moabu na viongozi wa Amoni wataokolewa kutoka mkono wake.
And he will enter into the glorious land, and many will fall. But only these will be saved from his hand: Edom, and Moab, and the first part of the sons of Ammon.
42 Atapanua mamlaka yake juu ya nchi nyingi; hata Misri haitaepuka.
And he will cast his hand upon the lands, and the land of Egypt will not escape.
43 Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na utajiri wote wa Misri, pamoja na Walibia na Wakushi kwa kujisalimisha.
And he will rule over the treasure chests of gold, and silver, and all the precious things of Egypt, and likewise he will pass through Libya and Ethiopia.
44 Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamshtua, naye ataondoka kwa ghadhabu nyingi ili kuangamiza na kuharibu kabisa wengi.
And rumors from the East and from the North will trouble him. And he will arrive with a great multitude to destroy and to execute many.
45 Atasimika hema zake za ufalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa kupendeza. Hata hivyo, atafikia mwisho wake, wala hakuna yeyote atakayemsaidia.
And he will fasten his tabernacle, Apadno, between the seas, upon an illustrious and holy mountain, and he will come even to its summit, and no one will help him.”

< Danieli 11 >