< 2 Wafalme 18 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Hoshea mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Hezekia mwana wa Ahazi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
W trzecim roku Ozeasza, syna Eli, króla Izraela, Ezechiasz, syn Achaza, króla Judy, [zaczął] królować.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.
Miał on dwadzieścia pięć lat, kiedy zaczął królować, i królował dwadzieścia dziewięć lat w Jerozolimie. Jego matka [miała] na imię Abi [i była] córką Zachariasza.
3 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Daudi baba yake alivyofanya.
Czynił on to, co było słuszne w oczach PANA, wszystko tak, jak czynił Dawid, jego ojciec.
4 Akapaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, akazivunja sanamu, akakatakata nguzo za Ashera. Akavunja vipande vipande ile nyoka ya shaba Mose aliyotengeneza, kwa kuwa hadi siku hizo wana wa Israeli walikuwa wanaifukizia uvumba (ilikuwa ikiitwa Nehushtani).
Zniósł wyżyny, rozbił posągi, powycinał gaje i potłukł węża miedzianego, którego uczynił Mojżesz, bo aż do tego czasu synowie Izraela palili mu kadzidło, i nazwał go Nehustan.
5 Hezekia aliweka tumaini lake kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Hapakuwepo na mfalme mwingine wa kufanana naye miongoni mwa wafalme wa Yuda, kabla yake au baada yake.
Zaufał PANU, Bogu Izraela. I spośród wszystkich królów Judy nie było nikogo podobnego do niego ani [z tych, którzy byli] po nim, ani [z tych], którzy byli przed nim.
6 Alishikamana na Bwana kwa bidii wala hakuacha kumfuata; alishika amri ambazo Bwana alikuwa amempa Mose.
Przylgnął bowiem do PANA i nie odstępował od niego, ale przestrzegał jego przykazań, które PAN nadał Mojżeszowi.
7 Naye Bwana alikuwa pamoja naye, akafanikiwa katika kila alichokifanya. Aliasi dhidi ya mfalme wa Ashuru, wala hakumtumikia.
A PAN był z nim i powodziło mu się, gdziekolwiek wyruszał. Zbuntował się przeciw królowi Asyrii i nie służył mu.
8 Kuanzia mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye ngome, aliwashinda Wafilisti, hadi kufikia Gaza na himaya yake yote.
To on pokonał Filistynów aż do Gazy i jej granic, od wieży strażników aż do miasta warownego.
9 Mwaka wa nne wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa saba wa Hoshea mwana wa Ela kutawala Israeli, Shalmanesa mfalme wa Ashuru alikwenda kuishambulia Samaria na kuuzunguka kwa majeshi.
W czwartym roku króla Ezechiasza – był to siódmy rok Ozeasza, syna Eli, króla Izraela – Salmanaser, król Asyrii, wyruszył przeciwko Samarii i obległ ją.
10 Baada ya miaka mitatu Waashuru wakautwaa. Kwa hiyo Samaria ulitekwa katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea mfalme wa Israeli.
I zdobył ją pod koniec trzeciego roku. W szóstym roku Ezechiasza – był to dziewiąty rok Ozeasza, króla Izraela – Samaria została zdobyta.
11 Mfalme wa Ashuru akawahamishia Waisraeli huko Ashuru na akawaweka Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
Wtedy król Asyrii uprowadził Izraela do Asyrii i osiedlił ich w Chalach i Chaborze, przy rzece Gozanu, i w miastach Medów;
12 Hili lilitokea kwa sababu hawakumtii Bwana Mungu wao, lakini walikuwa wamevunja agano lake, yale yote ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwaamuru. Hawakuzisikiliza amri wala kuzitimiza.
Ponieważ nie posłuchali głosu PANA, swego Boga, ale przekroczyli jego przymierze [oraz] to wszystko, co nakazał Mojżesz, sługa PANA. Nie słuchali tego i nie wypełniali.
13 Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
W czternastym roku króla Ezechiasza Sennacheryb, król Asyrii, wyruszył przeciw wszystkim warownym miastom Judy i zdobył je.
14 Basi Hezekia mfalme wa Yuda akamtumia ujumbe mfalme wa Ashuru huko Lakishi akisema: “Nimefanya makosa. Ondoka katika nchi yangu, nami nitakulipa chochote unachokitaka kwangu.” Mfalme wa Ashuru akamtoza Hezekia mfalme wa Yuda talanta 300 za fedha, na talanta thelathini za dhahabu.
Wtedy Ezechiasz, król Judy, posłał do króla Asyrii do Lakisz, mówiąc: Postąpiłem źle, odstąp ode mnie. Cokolwiek na mnie nałożysz, poniosę. Król Asyrii nałożył więc na Ezechiasza, króla Judy, trzysta talentów srebra i trzydzieści talentów złota.
15 Basi Hezekia akampa fedha yote iliyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme.
I Ezechiasz dał mu całe srebro, które się znalazło w domu PANA i w skarbcach domu królewskiego.
16 Wakati huu Hezekia mfalme wa Yuda akabandua dhahabu yote iliyokuwa imefunika milango na miimo ya Hekalu la Bwana, akampa mfalme wa Ashuru.
W tym samym czasie Ezechiasz zerwał złoto z drzwi domu PANA oraz ze słupów, które obił [sam] Ezechiasz, król Judy, i dał je królowi Asyrii.
17 Mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wake mkuu, na afisa wake mkuu, na jemadari wa jeshi, pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Wakaja Yerusalemu na kusimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
Jednakże król Asyrii posłał z Lakisz Tartana, Rabsarisa i Rabszaka z wielkim wojskiem do Jerozolimy, do króla Ezechiasza. Wyruszyli i przybyli do Jerozolimy. Gdy przybyli, przyszli i zatrzymali się przy kanale górnej sadzawki, która jest przy drodze pola folusznika.
18 Wakaagiza mfalme aitwe. Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la mfalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakawaendea.
A gdy wołali do króla, wyszli do nich Eliakim, syn Chilkiasza, przełożony domu, Szebna, pisarz, oraz Joach, syn Asafa, kronikarz.
19 Yule jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia: “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
Wtedy Rabszak powiedział do nich: Powiedzcie Ezechiaszowi: Tak mówi wielki król, król Asyrii: Co to za ufność, na której polegasz?
20 Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
Mówisz – ale to słowa daremne – mam dość rady i siły do wojny. Teraz więc w kim pokładasz ufność, że zbuntowałeś się przeciwko mnie?
21 Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
Oto teraz opierasz się na tej nadłamanej lasce trzcinowej – na Egipcie – która gdy ktoś się oprze na niej, wbija mu się w dłoń i przebija ją. Taki jest faraon, król Egiptu, dla wszystkich, którzy mu ufają.
22 Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya katika Yerusalemu”?
A jeśli mi powiecie: Ufamy PANU, naszemu Bogu – czy on nie jest tym, którego wyżyny i ołtarze zniósł Ezechiasz i nakazał Judzie i Jerozolimie: Przed tym ołtarzem w Jerozolimie będziecie oddawać pokłon?
23 “‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
Dlatego teraz proszę, daj zastaw memu panu, królowi Asyrii, a dam ci dwa tysiące koni, jeśli zdołasz posadzić na nich jeźdźców.
24 Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
Jakże więc stawisz opór jednemu dowódcy z najmniejszych sług mego pana, a pokładasz nadzieję w Egipcie, że [otrzymasz] rydwany i jeźdźców?
25 Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza mahali hapa pasipo neno kutoka kwa Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
Poza tym – czy bez [woli] PANA wyruszyłem przeciw temu miejscu, aby je zburzyć? PAN powiedział do mnie: Wyrusz przeciwko tej ziemi i spustosz ją.
26 Ndipo Eliakimu mwana wa Hilkia, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
Wtedy Eliakim, syn Chilkiasza, Szebna i Joach powiedzieli do Rabszaka: Proszę, mów do swoich sług po syryjsku, bo rozumiemy, a nie mów z nami po hebrajsku wobec ludu, który jest na murze.
27 Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
Lecz Rabszak odpowiedział: Czy do twego pana i do ciebie posłał mnie mój pan, abym mówił te słowa? Czyż nie do tych mężczyzn siedzących na murze, aby jedli swój kał i pili swój mocz razem z wami?
28 Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni neno la mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
Wstał więc Rabszak i zawołał donośnym głosem po hebrajsku tymi słowami: Słuchajcie słów wielkiego króla, króla Asyrii.
29 Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa mkononi mwangu.
Tak mówi król: Niech was nie zwodzi Ezechiasz, bo nie będzie mógł wyrwać was z mojej ręki.
30 Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
I nie dajcie się przekonać Ezechiaszowi, by zaufać PANU, gdy mówi: Na pewno PAN nas wybawi i to miasto nie będzie wydane w ręce króla Asyrii.
31 “Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
Nie słuchajcie Ezechiasza. Tak bowiem mówi król Asyrii: Zawrzyjcie ze mną przymierze i wyjdźcie do mnie, a każdy będzie jeść ze swojej winorośli i ze swego drzewa figowego i każdy będzie pić wodę ze swojej studni;
32 mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na mashamba ya mizabibu, nchi ya mizeituni na asali. Chagueni uzima, sio mauti! “Msimsikilize Hezekia, kwa kuwa anawapotosha asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’
Aż przyjdę i zabiorę was do ziemi podobnej do waszej, do ziemi zboża i wina, do ziemi chleba i winnic, do ziemi drzew oliwnych, oliwy i miodu. Będziecie żyć, a nie umierać. Nie słuchajcie Ezechiasza, bo was zwodzi, mówiąc: PAN nas wybawi.
33 Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
Czy bogowie [innych] narodów mogli wybawić swoją ziemię z ręki króla Asyrii?
34 Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu, Hena na Iva? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
Gdzie są bogowie Chamatu i Arpadu? Gdzie są bogowie Sefarwaim, Heny i Iwwy? Czy wyrwali Samarię z moich rąk?
35 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
Którzy spośród wszystkich bogów tych ziem wybawili swoją ziemię z mojej ręki, żeby PAN miał wybawić Jerozolimę z mojej ręki?
36 Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
Lecz lud milczał i nie odpowiedział mu ani słowa, bo taki był rozkaz króla: Nie odpowiadajcie mu.
37 Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.
Wtedy przyszli przełożony domu Eliakim, syn Chilkiasza, pisarz Szebna i kronikarz Joach, syn Asafa, do Ezechiasza, z rozdartymi szatami, i oznajmili mu słowa Rabszaka.

< 2 Wafalme 18 >