< 2 Wakorintho 5 >

1 Kwa maana twajua kama hema yetu ya dunia tunayoishi ikiharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu, nyumba iliyo ya milele kule mbinguni, isiyojengwa kwa mikono ya wanadamu. (aiōnios g166)
For we know that if this poor tent, our earthly house, is taken down, we have in Heaven a building which God has provided, a house not built by human hands, but eternal. (aiōnios g166)
2 Katika hema hii twalia kwa uchungu, tukitamani kuvikwa makao yetu ya mbinguni,
For in this one we sigh, because we long to put on over it our dwelling which comes from Heaven--
3 kwa kuwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tena kuwa uchi.
if indeed having really put on a robe we shall not be found to be unclothed.
4 Kwa kuwa tukiwa bado katika hema hii twalia kwa uchungu na kulemewa, kwa sababu hatutaki kuvuliwa bali kuvikwa makao yetu ya mbinguni ili kwamba kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima.
Yes, we who are in this tent certainly do sigh under our burdens, for we do not wish to lay aside that with which we are now clothed, but to put on more, so that our mortality may be absorbed in Life.
5 Basi Mungu ndiye alitufanya kwa ajili ya jambo lilo hilo naye ametupa Roho Mtakatifu kuwa amana, akituhakikishia ahadi ya kile kijacho.
And He who formed us with this very end in view is God, who has given us His Spirit as a pledge and foretaste of that bliss.
6 Kwa hiyo siku zote tunalo tumaini, hata ingawa tunajua kwamba wakati tukiwa katika mwili huu, tuko mbali na Bwana,
We have therefore a cheerful confidence. We know that while we are at home in the body we are banished from the Lord;
7 kwa maana twaenenda kwa imani wala si kwa kuona.
for we are living a life of faith, and not one of sight.
8 Naam, tunalo tumaini na ingekuwa bora zaidi kuuacha mwili huu na kwenda kukaa na Bwana.
So we have a cheerful confidence, and we anticipate with greater delight being banished from the body and going home to the Lord.
9 Kwa hiyo, kama tuko katika mwili huu au tuko mbali nao, lengo letu ni kumpendeza Bwana.
And for this reason also we make it our ambition, whether at home or in exile, to please Him perfectly.
10 Kwa kuwa sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apate kulipwa kwa ajili ya yale ambayo yametendwa katika mwili wake, yakiwa mema au mabaya.
For we must all of us appear before Christ's judgement-seat in our true characters, in order that each may then receive an award for his actions in this life, in accordance with what he has done, whether it be good or whether it be worthless.
11 Basi, kwa kuwa tunajua kumcha Bwana, tunajitahidi kuwavuta wengine. Lakini Mungu anatufahamu dhahiri, nami natumaini kwamba tu dhahiri katika dhamiri zenu pia.
Therefore, because we realize how greatly the Lord is to be feared, we are endeavouring to win men over, and God recognizes what our motives are, and I hope that you, in your hearts, recognize them too.
12 Sio kwamba tunajaribu kujistahilisha kwenu tena, lakini tunataka kuwapa nafasi ili mwone fahari juu yetu mweze kuwajibu hao wanaoona fahari juu ya mambo yanayoonekana badala ya mambo yaliyo moyoni.
We are not again commending ourselves to your favour, but are furnishing you with a ground of boasting on our behalf, so that you may have a reply ready for those with whom superficial appearances are everything and sincerity of heart counts for nothing.
13 Kama tumerukwa na akili, ni kwa ajili ya Mungu; kama tuna akili timamu, ni kwa ajili yenu.
For if we have been beside ourselves, it has been for God's glory; or if we are now in our right senses, it is in order to be of service to you.
14 Kwa kuwa upendo wa Kristo unatutia nguvu, kwa sababu tunasadiki kuwa mmoja alikufa kwa ajili ya wote, kwa hiyo wote walikufa.
For the love of Christ overmasters us, the conclusion at which we have arrived being this--that One having died for all, His death was their death,
15 Naye alikufa kwa ajili ya watu wote, ili kwamba wote wanaoishi wasiishi tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa na kufufuliwa tena kwa ajili yao.
and that He died for all in order that the living may no longer live to themselves, but to Him who died for them and rose again.
16 Hivyo tangu sasa hatumwangalii mtu yeyote kwa mtazamo wa kibinadamu. Ingawa wakati fulani tulimwangalia Kristo kwa namna ya kibinadamu, hatumwangalii tena hivyo.
Therefore for the future we know no one simply as a man. Even if we have known Christ as a man, yet now we do so no longer.
17 Kwa hiyo kama mtu akiwa ndani ya Kristo, amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama, yamekuwa mapya.
So that if any one is in Christ, he is a new creature: the old state of things has passed away; a new state of things has come into existence.
18 Haya yote yanatokana na Mungu, ambaye ametupatanisha sisi na nafsi yake kwa njia ya Yesu Kristo na kutupata sisi huduma ya upatanisho:
And all this is from God, who has reconciled us to Himself through Christ, and has appointed us to serve in the ministry of reconciliation.
19 Kwamba Mungu alikuwa ndani ya Kristo akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake mwenyewe, akiwa hawahesabii watu dhambi zao. Naye ametukabidhi sisi ujumbe huu wa upatanisho.
We are to tell how God was in Christ reconciling the world to Himself, not charging men's transgressions to their account, and that He has entrusted to us the Message of this reconciliation.
20 Kwa hiyo sisi ni mabalozi wa Kristo, kana kwamba Mungu anawasihi kupitia kwa vinywa vyetu. Nasi twawaomba sana ninyi kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu.
On Christ's behalf therefore we come as ambassadors, God, as it were, making entreaty through our lips: we, on Christ's behalf, beseech men to be reconciled to God.
21 Kwa maana Mungu alimfanya yeye asiyekuwa na dhambi kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kufanywa haki ya Mungu kwake yeye.
He has made Him who knew nothing of sin to be sin for us, in order that in Him we may become the righteousness of God.

< 2 Wakorintho 5 >