< 2 Wakorintho 4 >

1 Kwa hiyo, kwa kuwa tuna huduma hii kwa rehema za Mungu, hatukati tamaa.
Therefore, being engaged in this service and being mindful of the mercy which has been shown us, we are not cowards.
2 Tumekataa mambo ya siri na ya aibu, wala hatufuati njia za udanganyifu, tukichanganya Neno la Mungu na uongo. Kinyume cha hayo, tunadhihirisha kweli waziwazi na kujitambulisha wenyewe kwenye dhamiri ya kila mtu mbele za Mungu.
Nay, we have renounced the secrecy which marks a feeling of shame. We practice no cunning tricks, nor do we adulterate God's Message. But by a full clear statement of the truth we strive to commend ourselves in the presence of God to every human conscience.
3 Hata nayo Injili yetu kama imetiwa utaji, ni kwa wale tu wanaopotea.
If, however, the meaning of our Good News has been veiled, the veil has been on the hearts of those who are on the way to perdition,
4 Kwa habari yao, mungu wa dunia hii amepofusha akili za wasioamini, ili wasione nuru ya Injili ya utukufu wa Kristo, aliye sura ya Mungu. (aiōn g165)
in whom the god of this present age has blinded their unbelieving minds so as to shut out the sunshine of the Good News of the glory of the Christ, who is the image of God. (aiōn g165)
5 Kwa maana hatujihubiri sisi wenyewe ila tunamhubiri Yesu Kristo kuwa ni Bwana na sisi ni watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.
(For we do not proclaim ourselves, but we proclaim Christ Jesus as Lord, and ourselves as your bondservants for the sake of Jesus.)
6 Kwa kuwa Mungu, yeye aliyesema, “Nuru na ingʼae gizani,” ameifanya nuru yake ingʼae mioyoni mwetu ili kutupatia nuru ya maarifa ya utukufu wa Mungu katika uso wa Kristo.
For God who said, "Out of darkness let light shine," is He who has shone in our hearts to give us the light of the knowledge of God's glory, which is radiant on the face of Christ.
7 Lakini tunayo hazina hii katika vyombo vya udongo, ili ijulikane wazi kwamba uwezo huu wa ajabu unatoka kwa Mungu wala si kwetu.
But we have this treasure in a fragile vase of clay, in order that the surpassing greatness of the power may be seen to belong to God, and not to originate in us.
8 Twataabika kila upande lakini hatuangamizwi; twaona wasiwasi lakini hatukati tamaa;
We are hard pressed, yet never in absolute distress; perplexed, yet never utterly baffled;
9 twateswa lakini hatuachwi; twatupwa chini lakini hatupondwi.
pursued, yet never left unsuccoured; struck to the ground, yet never slain;
10 Siku zote twachukua katika mwili kufa kwake Yesu ili kwamba uzima wa Yesu uweze kudhihirika katika miili yetu.
always, wherever we go, carrying with us in our bodies the putting to death of Jesus, so that in our bodies it may also be clearly shown that Jesus lives.
11 Kwa maana sisi tulio hai siku zote tumetolewa tufe kwa ajili ya Yesu, ili kwamba uzima wake upate kudhihirishwa katika mwili wetu upatikanao na mauti.
For we, alive though we are, are continually surrendering ourselves to death for the sake of Jesus, so that in this mortal nature of ours it may also be clearly shown that Jesus lives.
12 Hivyo basi, mauti inatenda kazi ndani yetu, bali uzima unatenda kazi ndani yenu.
Thus we are constantly dying, while you are in full enjoyment of Life.
13 Imeandikwa, “Niliamini, kwa hiyo nimesema.” Kwa roho yule yule wa imani pia tuliamini na hivyo tunasema,
But possessing the same Spirit of faith as he who wrote, "I believed, and therefore I have spoken," we also believe, and therefore we speak.
14 kwa sababu tunajua kwamba yeye aliyemfufua Bwana Yesu kutoka kwa wafu, atatufufua sisi pia pamoja na Yesu na kutuleta sisi pamoja nanyi mbele zake.
For we know that He who raised the Lord Jesus from the dead will raise us also to be with Jesus, and will cause both us and you to stand in His own presence.
15 Haya yote ni kwa faida yenu, ili kwamba neema ile inavyowafikia watu wengi zaidi na zaidi, ipate kusababisha shukrani nyingi kwa utukufu wa Mungu.
For everything is for your sakes, in order that grace, being more richly bestowed because of the thanksgivings of the increased number, may more and more promote the glory of God.
16 Kwa hiyo, hatukati tamaa. Ingawa utu wetu wa nje unachakaa, utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.
Therefore we are not cowards. Nay, even though our outward man is wasting away, yet our inward man is being renewed day by day.
17 Kwa maana dhiki yetu nyepesi iliyo ya kitambo inatutayarisha kwa ajili ya utukufu wa milele unaozidi kuwa mwingi kupita kiasi, (aiōnios g166)
For this our light and transitory burden of suffering is achieving for us a preponderating, yes, a vastly preponderating, and eternal weight of glory; (aiōnios g166)
18 kwa sababu hatuangalii yale yanayoweza kuonekana bali yale yasiyoweza kuonekana. Kwa maana yale yanayoweza kuonekana ni ya kitambo tu, bali yale yasiyoweza kuonekana ni ya milele. (aiōnios g166)
while we look not at things seen, but things unseen; for things seen are temporary, but things unseen are eternal. (aiōnios g166)

< 2 Wakorintho 4 >