< 2 Nyakati 9 >

1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
A gdy królowa Saby usłyszała o sławie Salomona, przybyła do Jerozolimy, aby przez zagadki poddać go próbie. [Przybyła] z bardzo wielkim orszakiem, z wielbłądami niosącymi wonności, bardzo dużo złota i drogocennych kamieni. Gdy przyszła do Salomona, rozmawiała z nim o wszystkim, co leżało jej na sercu.
2 Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea.
Salomon zaś odpowiedział na wszystkie jej pytania. Nie było nic tajemnego dla Salomona, na co nie mógłby jej odpowiedzieć.
3 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
Gdy więc królowa Saby ujrzała mądrość Salomona i dom, który zbudował;
4 chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.
A także potrawy jego stołu, siadanie jego sług, stawanie jego służących, ich szaty, jego podczaszych i ich szaty oraz schody, po których wstępował do domu PANA, dech zamarł jej [w piersi].
5 Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
Wtedy przemówiła do króla: Prawdziwa była ta wieść, którą słyszałam w mojej ziemi o twoich dziełach i twojej mądrości.
6 Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia.
Jednak nie wierzyłam ich słowom, aż przybyłam i zobaczyłam [to wszystko] na własne oczy. I oto nie powiedziano mi nawet połowy o twojej wielkiej mądrości. Przeszedłeś bowiem sławę, o której słyszałam.
7 Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
Błogosławieni twoi ludzie i błogosławieni twoi słudzy, którzy zawsze stoją przed tobą i słuchają twojej mądrości.
8 Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”
Niech będzie błogosławiony PAN, twój Bóg, który cię sobie upodobał, aby cię posadzić na swoim tronie jako króla [dla] PANA, twojego Boga. A ponieważ twój Bóg umiłował Izraela, aby go umocnić na wieki, dlatego ustanowił cię królem nad nimi, abyś czynił sąd i sprawiedliwość.
9 Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
I dała królowi sto dwadzieścia talentów złota i bardzo wiele wonności oraz drogocennych kamieni. Nigdy nie [przywieziono] takich wonności, jakie królowa Saby dała królowi Salomonowi.
10 (Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
Ponadto słudzy Hurama i słudzy Salomona, którzy przywieźli złoto z Ofiru, sprowadzili także drzewa sandałowe i drogocenne kamienie.
11 Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)
Z tego drzewa sandałowego król wykonał schody do domu PANA i do domu królewskiego oraz harfy i cytry dla śpiewaków. Nigdy przedtem nie widziano takich rzeczy w ziemi Judy.
12 Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
Król Salomon dał królowej Saby wszystko, czego zapragnęła i o co poprosiła, nie licząc [daru za to], co przyniosła do króla. Potem odjechała i wróciła do swojej ziemi razem ze swoimi sługami.
13 Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
A waga złota, które wpływało do Salomona w ciągu jednego roku, wynosiła sześćset sześćdziesiąt sześć talentów złota;
14 mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.
Nie licząc [tego], co dostawał od kupców i handlarzy. Także wszyscy królowie arabscy i namiestnicy ziemi przywozili złoto i srebro Salomonowi.
15 Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
Wykonał więc król Salomon dwieście tarczy z kutego złota. Na każdą tarczę wychodziło sześćset [syklów] kutego złota.
16 Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
[Wykonał] także trzysta puklerzy z kutego złota. Na każdy puklerz wychodziło trzysta [syklów] złota. I król umieścił je w domu lasu Libanu.
17 Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
Król sporządził także wielki tron z kości słoniowej i pokrył go szczerym złotem.
18 Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
Tron [miał] sześć stopni, a podnóżek był ze złota, przymocowany do tronu. Po obu stronach siedzenia były poręcze, a przy poręczach stały dwa lwy.
19 Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
Dwanaście lwów stało na tych sześciu stopniach po obu stronach. Czegoś takiego nie uczyniono w żadnym [innym] królestwie.
20 Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni.
Wszystkie też naczynia, z których pił król Salomon, były złote, i wszystkie sprzęty w domu lasu Libanu [były] ze szczerego złota. [Nie było] nic ze srebra, gdyż nie uważano go za cenne w czasach Salomona.
21 Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
Królewskie okręty pływały bowiem do Tarszisz wraz ze sługami Hurama. Raz na trzy lata okręty wracały z Tarszisz, przywożąc złoto, srebro, kości słoniowe, małpy i pawie.
22 Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
I tak król Salomon przewyższał wszystkich królów ziemi bogactwem i mądrością.
23 Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
Wszyscy więc królowie ziemi pragnęli widzieć Salomona, aby słuchać jego mądrości, którą Bóg włożył w jego serce.
24 Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
Każdy z nich przynosił mu swoje dary: naczynia srebrne i złote, szaty, zbroje, wonności, konie i muły, rokrocznie.
25 Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye.
I Salomon miał cztery tysiące przegród dla koni i rydwanów oraz dwanaście tysięcy jeźdźców, których rozmieścił po miastach rydwanów i przy królu w Jerozolimie.
26 Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri.
I panował nad wszystkimi królami od rzeki aż do ziemi Filistynów i do granicy Egiptu.
27 Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
Król sprawił, że srebro w Jerozolimie było jak kamienie, a cedry tak liczne jak sykomory na nizinie.
28 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.
Sprowadzono też dla Salomona konie z Egiptu i ze wszystkich [innych] ziem.
29 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati?
A pozostałych dziejów Salomona, od pierwszych do ostatnich, czy nie zapisano w księdze proroka Natana, w proroctwie Achiasza Szilonity i w widzeniach Jeddo widzącego przeciw Jeroboamowi, synowi Nebata?
30 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
I Salomon królował w Jerozolimie nad całym Izraelem czterdzieści lat.
31 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Potem Salomon zasnął ze swoimi ojcami i pochowano go w mieście Dawida, jego ojca, a syn jego Roboam królował w jego miejsce.

< 2 Nyakati 9 >