< 2 Nyakati 35 >

1 Yosia akaadhimisha Pasaka kwa Bwana katika Yerusalemu, mwana-kondoo wa Pasaka akachinjwa siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza.
Potem Jozjasz obchodził w Jerozolimie święto Paschy dla PANA. I zabito baranka paschalnego czternastego [dnia] pierwszego miesiąca.
2 Akawaweka makuhani kwenye wajibu wao na kuwatia moyo katika utumishi wa Hekalu la Bwana.
Ustanowił też kapłanów na swoich urzędach i zachęcił ich do służby w domu PANA.
3 Akawaambia Walawi, waliowafundisha Waisraeli wote na waliokuwa wamejiweka wakfu kwa ajili ya kazi ya Bwana, “Liwekeni hilo Sanduku takatifu katika Hekalu lile alilojenga Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli. Halipaswi kubebwa huku na huko mabegani mwenu. Sasa mtumikieni Bwana Mungu wenu na watu wake Israeli.
I powiedział Lewitom, którzy nauczali całego Izraela i byli poświęceni PANU: Ustawcie świętą arkę w domu, który zbudował syn Dawida Salomon, król Izraela. Nie będziecie już jej dźwigać na swoich ramionach. Teraz służcie PANU, swojemu Bogu, i jego ludowi Izraela;
4 Jiandaeni kwa kufuata jamaa zenu katika migawanyo yenu, kufuatana na maelezo yaliyoandikwa na Daudi mfalme wa Israeli na mwanawe Solomoni.
Przygotujcie się według waszych rodów i według waszych zmian, jak napisał Dawid, król Izraela, i jak napisał jego syn Salomon;
5 “Simameni mahali patakatifu kwa kufuata migawanyo ya jamaa za baba zenu kulingana na koo zenu na pawepo Walawi kwa ajili ya kila mgawanyo wa nyumba ya baba zenu.
I stójcie w świątyni według podziału na rody waszych braci, którzy są z ludu, i według podziału na rody Lewitów.
6 Chinjeni mwana-kondoo wa Pasaka, jitakaseni, nanyi kwa niaba ya koo zenu fanyeni maandalizi, mkitenda sawasawa na neno la Bwana kwa mkono wa Mose.”
Wtedy zabijcie baranka paschalnego, poświęćcie się i przygotujcie waszych braci, by wszystko czynić według słowa PANA [przekazanego] przez Mojżesza.
7 Ndipo Yosia akawapa watu wote wana-mbuzi waliokuwepo jumla ya kondoo wapatao 30,000 kwa ajili ya sadaka ya Pasaka, pia na ngʼombe 10,000, vyote hivi kutoka mali binafsi ya mfalme.
Potem Jozjasz dał ludowi jagnięta i koźlęta z trzody, wszystkie na ofiary święta Paschy dla wszystkich obecnych w liczbie trzydziestu tysięcy, oraz trzy tysiące wołów. To [wszystko] pochodziło z dóbr króla.
8 Pia maafisa wake, wakatoa kwa hiari yao wakawapa watu, makuhani na Walawi. Hilkia, Zekaria na Yehieli, waliokuwa maafisa wakuu wa Hekalu la Mungu, wakawapa makuhani sadaka za Pasaka wana-kondoo na wana-mbuzi 2,600 na mafahali 300.
Jego książęta złożyli dobrowolne dary ludowi, kapłanom i Lewitom: Chilkiasz, Zachariasz, Jechiel, przełożeni domu Bożego, dali kapłanom na ofiary święta Paschy dwa tysiące sześćset [jagniąt] i trzysta wołów.
9 Konania na nduguze wawili, Shemaya na Nethaneli, pamoja na Hashabia, Yeieli na Yozabadi waliokuwa viongozi wa Walawi, nao pia wakawapa Walawi wana-kondoo na wana-mbuzi 5,000 na mafahali 500, kwa ajili ya sadaka za Pasaka.
Ponadto Konaniasz i jego bracia Szemejasz i Netaneel oraz Chaszabiasz, Jejel i Jozabad, naczelnicy z Lewitów, dali [innym] Lewitom na ofiary święta Paschy pięć tysięcy [jagniąt] i pięćset wołów.
10 Huduma ilipomalizika kuandaliwa makuhani wakasimama mahali pao na Walawi katika migawanyo yao kama mfalme alivyokuwa ameamuru.
Wszystko więc zostało przygotowane do służby, kapłani stanęli na swoich miejscach, a Lewici w swoich zmianach według rozkazu króla.
11 Wana-kondoo wa Pasaka wakachinjwa, nao makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa, wakati Walawi wakiwa wanawachuna wale wanyama ngozi.
I zabili baranki paschalne, kapłani kropili [ich] krwią, a Lewici obdzierali [je] ze skóry.
12 Wakatenga sadaka za kuteketezwa ili waweze kugawia ili migawanyo kwa kufuata jamaa za baba zao ili watoe sadaka kwa Bwana kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose. Wakafanya vivyo hivyo kwa wale mafahali.
Następnie oddzielili [część] z nich na całopalenie, aby dać [je] ludowi według podziału na rody jako ofiarę dla PANA, tak jak jest napisane w księdze Mojżesza. Podobnie też [uczyniono] z wołami.
13 Wakawaoka wale wanyama wa Pasaka kwenye moto kama ilivyoamriwa, wakachemsha zile sadaka takatifu kwenye vyungu, masufuria makubwa na vikaango na kuwagawia watu wote upesi.
I piekli baranki paschalne na ogniu według zwyczaju, inne zaś [ofiary] święte gotowali w garnkach, kotłach i rondlach, po czym rozdawali szybko całemu ludowi.
14 Hatimaye wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani, kwa sababu wale makuhani, yaani, wazao wa Aroni, walikuwa wanatoa sadaka za kuteketezwa pamoja na zile sehemu zilizonona mpaka usiku. Hivyo Walawi wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Aroni.
Potem też przygotowali [posiłek] dla siebie i kapłanów. Kapłani bowiem, synowie Aarona, byli [zajęci] składaniem całopaleń i tłuszczu aż do nocy. Lewici więc przygotowali [posiłek] dla siebie i dla kapłanów, synów Aarona.
15 Waimbaji, wazao wa Asafu, walikuwa katika nafasi zao, kama ilivyoagizwa na Mfalme Daudi, Asafu, Hemani na Yeduthuni mwonaji wa Mfalme. Mabawabu katika kila lango hawakuhitaji kuacha nafasi zao kwa sababu Walawi wenzao walifanya maandalizi kwa ajili yao.
Śpiewacy, synowie Asafa, [stali] na swoich stanowiskach według rozkazu Dawida, Asafa, Hemana i Jedutuna, widzącego króla. Odźwierni też [stali] przy każdej bramie. Nie musieli opuszczać swojej służby, ponieważ ich bracia Lewici przygotowywali dla nich [posiłki].
16 Kwa hiyo wakati ule huduma yote ya Bwana ilifanyika katika kuadhimisha Pasaka, kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana kama alivyoamuru Mfalme Yosia.
Tak więc cała służba została przygotowana w tym dniu, aby obchodzić święto Paschy i składać całopalenia na ołtarzu PANA według rozkazu króla Jozjasza.
17 Waisraeli waliokuwepo wakaadhimisha Pasaka wakati huo na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa siku saba.
Synowie Izraela, którzy tam się znajdowali, obchodzili w tym czasie święto Paschy, a Święto Przaśników przez siedem dni.
18 Kulikuwa hakujafanyika Pasaka kama hii katika Israeli tangu siku za nabii Samweli wala hakukuwa na mfalme yeyote wa Israeli ambaye kamwe alishaadhimisha Pasaka kama ile aliyofanya Mfalme Yosia, akiwa na makuhani, Walawi na watu wote wa Yuda na watu wa Israeli waliokuwepo huko, pamoja na watu wa Yerusalemu.
Żadne święto Paschy podobne do tego nie było obchodzone w Izraelu od czasów proroka Samuela i żaden z królów Izraela nie obchodził tak święta Paschy, jak obchodzili [je] Jozjasz, kapłani, Lewici, cały lud Judy i Izraela, który się tam znajdował, oraz mieszkańcy Jerozolimy.
19 Pasaka iliadhimishwa katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia.
Paschę tę obchodzono w osiemnastym roku panowania Jozjasza.
20 Baada ya haya yote, Yosia alipomaliza kulitengeneza vizuri Hekalu, Neko mfalme wa Misri, akapanda ili kupigana huko Karkemishi katika Mto Frati, naye Yosia akatoka kwenda kupigana naye.
Po tym wszystkim, gdy Jozjasz naprawił dom [Boży], nadciągnął Necho, król Egiptu, aby walczyć przeciw Karkemisz nad [rzeką] Eufrat, a Jozjasz wyruszył mu naprzeciw.
21 Lakini Neko akamtumia wajumbe kusema, “Kuna ugomvi gani kati yangu mimi na wewe, Ee Mfalme wa Yuda? Si wewe ninayekushambulia wakati huu, bali ile nyumba ambayo nina vita nayo, Mungu ameniambia niharakishe, kwa hivyo acha kumpinga Mungu, ambaye yuko pamoja nami, la sivyo atakuangamiza.”
Ale on posłał do niego swoich posłańców ze słowami: Co ja mam z tobą, królu Judy? Nie przeciw tobie [ciągnę] dzisiaj, lecz przeciwko domowi, który ze mną walczy. I Bóg nakazał mi, abym się pospieszył. Przestań walczyć z Bogiem, który [jest] ze mną, aby cię nie zniszczył.
22 Lakini hata hivyo, Yosia hakukubali kumwacha, bali alijibadilisha ili kupigana naye vita. Hakusikiliza yale Neko aliyokuwa amemwambia kwa agizo la Mungu bali alikwenda kupigana naye katika tambarare ya Megido.
Ale Jozjasz nie odwrócił się od niego, lecz zmienił swoje szaty, aby z nim walczyć, i nie posłuchał słów Necho, [które pochodziły] z ust Boga. Tak więc wyruszył, aby walczyć na równinie Megiddo.
23 Wapiga upinde wakampiga Mfalme Yosia, naye akawaambia maafisa wake, “Niondoeni, nimejeruhiwa vibaya sana.”
A łucznicy ugodzili króla Jozjasza i wtedy król powiedział do swoich sług: Wyprowadźcie mnie, bo jestem ciężko ranny.
24 Kwa hiyo wakamshusha kutoka kwenye gari lake la farasi, wakamweka kwenye gari lingine alilokuwa nalo na kumleta Yerusalemu, ambako alifia. Akazikwa katika makaburi ya baba zake, nayo Yuda yote na Yerusalemu wakamwombolezea Yosia.
Jego słudzy więc wyciągnęli go z rydwanu i wsadzili na inny rydwan, który należał do niego: zawieźli go do Jerozolimy i tam umarł. Potem pogrzebali go w grobach jego ojców, a cały lud Judy i Jerozolimy opłakiwał Jozjasza.
25 Nabii Yeremia akatunga maombolezo kwa ajili ya kifo chake, nao waimbaji wote, wanaume kwa wanawake, hufanya ukumbusho wa Yosia katika maombolezo hadi leo. Haya yakafanywa desturi katika Israeli, nayo yameandikwa katika Maombolezo.
Jeremiasz też lamentował nad Jozjaszem, a wszyscy śpiewacy i śpiewaczki wspominają Jozjasza w swoich lamentacjach aż do dziś, i uczynili z tego zwyczaj w Izraelu. Oto są zapisane w lamentacjach.
26 Matukio mengine ya utawala wa Yosia na matendo yake mema, kulingana na yale yaliyoandikwa katika sheria ya Bwana:
A pozostałe dzieje Jozjasza, jego życzliwość według tego, co jest napisane w Prawie PANA;
27 matukio yote, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
I jego czyny pierwsze i ostatnie są zapisane w księdze królów Izraela i Judy.

< 2 Nyakati 35 >