< Ezra 8 >

1 Hawa ndio viongozi wa jamaa pamoja na wale walioandikwa ambao walikuja pamoja nami kutoka Babeli wakati wa utawala wa Mfalme Artashasta:
A oto naczelnicy rodów i rodowody tych, którzy wyruszyli ze mną z Babilonu za panowania króla Artakserksesa:
2 wa wazao wa Finehasi, alikuwa Gershoni; wa wazao wa Ithamari, alikuwa Danieli; wa wazao wa Daudi, alikuwa Hatushi
Z synów Pinchasa – Gerszom; z synów Itamara – Daniel; z synów Dawida – Chattusz;
3 wa wazao wa Shekania; wa wazao wa Paroshi, alikuwa Zekaria, na watu 150 walioandikishwa pamoja naye;
Z synów Szekaniasza, z synów Parosza – Zachariasz, a z nim spisanych według rodowodów było stu pięćdziesięciu mężczyzn;
4 wa wazao wa Pahath-Moabu, alikuwa Eliehoenai mwana wa Zerahia na wanaume 200 pamoja naye;
Z synów Pachat-Moaba – Elioenaj, syn Zerachiasza, a z nim dwustu mężczyzn;
5 wa wazao wa Zatu, alikuwa Shekania mwana wa Yahazieli na wanaume 300 pamoja naye;
Z synów Szekaniasza – syn Jahaziela, a z nim trzystu mężczyzn;
6 wa wazao wa Adini, alikuwa Ebedi mwana wa Yonathani na wanaume 50 pamoja naye;
Z synów Adina – Ebed, syn Jonatana, a z nim pięćdziesięciu mężczyzn;
7 wa wazao wa Elamu, alikuwa Yeshaya mwana wa Athalia, na wanaume 70 pamoja naye;
Z synów Elama – Jeszajasz, syn Ataliasza, a z nim siedemdziesięciu mężczyzn;
8 wa wazao wa Shefatia, alikuwa Zebadia mwana wa Mikaeli na wanaume 80 pamoja naye;
Z synów Szefatiasza – Zebadiasz, syn Mikaela, a z nim osiemdziesięciu mężczyzn;
9 wa wazao wa Yoabu, alikuwa Obadia mwana wa Yehieli na wanaume 218 pamoja naye;
Z synów Joaba – Obadiasz, syn Jechiela, a z nim dwustu osiemnastu mężczyzn;
10 wa wazao wa Bani, alikuwa Shelomithi mwana wa Yosifia na wanaume 160 pamoja naye;
Z synów Szelomita – syn Josifiasza, a z nim stu sześćdziesięciu mężczyzn;
11 wa wazao wa Bebai, alikuwa Zekaria mwana wa Bebai na wanaume 28 pamoja naye;
Z synów Bebaja – Zachariasz, syn Bebaja, a z nim dwudziestu ośmiu mężczyzn;
12 wa wazao wa Azgadi, alikuwa Yohanani mwana wa Hakatani na wanaume 110 pamoja naye;
Z synów Azgada – Johanan, syn Hakkatana, a z nim stu dziesięciu mężczyzn;
13 wa wazao wa Adonikamu, hawa walikuwa wa mwisho ambao majina yao ni Elifeleti, Yeueli, Shemaya na wanaume 60 pamoja nao;
Z synów Adonikama [wyruszyli] ostatni, a oto ich imiona: Elifelet, Jejel i Szemajasz, a z nimi sześćdziesięciu mężczyzn;
14 wa wazao wa Bigwai, walikuwa Uthai na Zakuri na wanaume 70 pamoja nao.
Z synów Bigwaja – Utaj i Zabbud, a z nimi siedemdziesięciu mężczyzn.
15 Niliwakusanya kwenye mto utiririkao kuelekea Ahava, nasi tukapiga kambi pale siku tatu. Wakati nilipokagua kati ya watu na makuhani, sikuwapata Walawi.
I zgromadziłem ich nad rzeką, która płynie do Achawy, i obozowaliśmy tam przez trzy dni. Potem dokonałem przeglądu ludu i kapłanów, a z synów Lewiego nie znalazłem tam [żadnego].
16 Basi niliwaita Eliezeri, Arieli, Shemaya, Elnathani, Yaribu, Elnathani, Nathani, Zekaria na Meshulamu waliokuwa viongozi na Yoyaribu na Elnathani waliokuwa wasomi,
Posłałem więc Eliezera, Ariela, Szemajasza, Elnatana, Jariba, Elnatana, Natana, Zachariasza i Meszullama, naczelników, a także Jojariba i Elnatana, [ludzi] rozumnych;
17 nikawatuma kwa Ido kiongozi huko Kasifia. Niliwaambia watakayomwambia Ido na ndugu zake, watumishi wa Hekalu huko Kasifia, ili waweze kutuletea wahudumu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.
I dałem przez nich polecenie Iddo, przełożonemu w miejscowości Kasifia, i przekazałem im słowa, które mieli powiedzieć do niego i jego braci Netinitów w miejscowości Kasifia; poleciłem, aby nam przyprowadzili sługi dla domu naszego Boga.
18 Kwa sababu mkono wa neema wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, walituletea Sherebia, mtu mwenye uwezo kutoka wazao wa Mahli mwana wa Lawi, mwana wa Israeli, na wana wa Sherebia pamoja na ndugu zao wanaume kumi na wanane.
I ponieważ łaskawa ręka naszego Boga była nad nami, przyprowadzili do nas, człowieka rozumnego spośród synów Machliego, syna Lewiego, syna Izraela, oraz Szerebiasza wraz z jego synami i braćmi – razem osiemnaście [osób];
19 Naye Hashabia, pamoja na Yeshaya kutoka wazao wa Merari na ndugu zake na wapwa wake wanaume ishirini.
I Chaszabiasza, a z nim Jeszajasz spośród synów Merariego wraz z jego braćmi i ich synów – razem dwadzieścia [osób];
20 Vilevile walileta watumishi wa Hekalu 220, kikundi ambacho Daudi na maafisa walikuwa wamekiweka kusaidia Walawi. Wote walikuwa wameorodheshwa kwa majina.
Ponadto spośród Netinitów, których Dawid i naczelnicy ustanowili do posługiwania Lewitom – dwieście dwadzieścia Netinitów. Ci wszyscy zostali imiennie wyznaczeni.
21 Kando ya Mto Ahava, hapo nilitangaza kufunga, ili tujinyenyekeshe mbele za Mungu wetu na kumwomba kwa ajili ya kutujalia safari ya amani sisi na watoto wetu, pamoja na mali zetu zote.
Wtedy tam, nad rzeką Achawa, ogłosiłem post, abyśmy ukorzyli się przed naszym Bogiem i abyśmy uprosili u niego szczęśliwą drogę dla nas, naszych dzieci i całego naszego dobytku.
22 Niliona aibu kumwomba mfalme askari na wapanda farasi wa kutulinda njiani kutokana na adui zetu, kwa sababu tulikwisha kumwambia mfalme, “Mkono wa neema wa Mungu wetu uko juu ya kila mmoja anayemtafuta, lakini hasira yake kubwa ni dhidi ya wote wamwachao.”
Wstydziłem się bowiem prosić króla o żołnierzy i jeźdźców, aby nas w drodze ratowali przed wrogami, ponieważ powiedzieliśmy królowi: Ręka naszego Boga [jest] nad wszystkimi, którzy go szukają, dla ich dobra, ale jego moc i gniew przeciwko wszystkim, którzy go opuszczają.
23 Kwa hiyo tulifunga na kumwomba Mungu wetu kuhusu jambo hili, naye akajibu maombi yetu.
Pościliśmy więc i prosiliśmy o to naszego Boga. A on nas wysłuchał.
24 Kisha niliwatenga viongozi wa makuhani kumi na wawili, pamoja na Sherebia, Hashabia na ndugu zao kumi,
Wtedy spośród przedniejszych kapłanów wydzieliłem dwunastu: Szerebiasza, Chaszabiasza, a z nimi dziesięciu ich braci;
25 nami nikawapimia fedha, dhahabu na vifaa ambavyo mfalme, washauri wake, maafisa wake na Israeli wote waliokuwepo walikuwa wamevitoa sadaka kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.
I odważyłem im srebro, złoto i naczynia, czyli ofiarę dla domu naszego Boga, którą złożyli: król, jego doradcy, jego dostojnicy oraz cały Izrael tam obecny.
26 Niliwapimia talanta 650 za fedha, vifaa vingine vya fedha vya uzito wa talanta mia moja, talanta mia moja za dhahabu,
Odważyłem im więc do rąk sześćset pięćdziesiąt talentów srebra, sto talentów naczyń srebrnych, sto talentów złota;
27 mabakuli ishirini ya dhahabu ya thamani ya darkoni elfu moja, na vyombo viwili vya shaba iliyosuguliwa, ya thamani kama dhahabu.
Dwadzieścia złotych pucharów, [ważących] po tysiąc darejków, i dwa naczynia z wybornego mosiądzu, tak piękne jak złoto.
28 Niliwaambia, “Ninyi pamoja na vyombo hivi ni wakfu kwa Bwana. Fedha na dhahabu ni sadaka ya hiari kwa Bwana, Mungu wa baba zenu.
Potem powiedziałem do nich: Wy jesteście poświęceni PANU, naczynia [także] są poświęcone, a to srebro i złoto [są] dobrowolnym darem dla PANA, Boga waszych ojców.
29 Vilindeni kwa uangalifu mpaka mtakapovipima ndani ya vyumba vya nyumba ya Bwana katika Yerusalemu mbele ya makuhani, viongozi na Walawi pamoja na wakuu wa jamaa za Israeli.”
Pilnujcie i strzeżcie [ich], dopóki nie odważycie [ich] przed przedniejszymi kapłanami, Lewitami i naczelnikami rodów Izraela w Jerozolimie, w komnatach domu PANA.
30 Ndipo makuhani na Walawi wakapokea fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu ambavyo vilipimwa na kupelekwa katika nyumba ya Mungu wetu mjini Yerusalemu.
Wzięli więc kapłani i Lewici odważone srebro, złoto i naczynia, aby [je] zanieść do Jerozolimy, do domu naszego Boga.
31 Tulianza safari kutoka Mto Ahava kwenda Yerusalemu kwenye siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza. Mkono wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, naye njiani alitulinda dhidi ya adui na wanyangʼanyi.
Potem wyruszyliśmy znad rzeki Achawa dwunastego [dnia] pierwszego miesiąca, aby udać się do Jerozolimy. A ręka naszego Boga była nad nami i wyrwała nas z ręki wrogów i czyhających [na nas] w drodze.
32 Kwa hiyo tuliwasili Yerusalemu ambapo tulipumzika kwa siku tatu.
I przybyliśmy do Jerozolimy, i zamieszkaliśmy tam przez trzy dni.
33 Katika siku ya nne, ndani ya nyumba ya Mungu wetu, tulipima fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu, tukakabidhi mikononi mwa kuhani Meremothi mwana wa Uria. Eleazari mwana wa Finehasi alikuwa pamoja naye, pia walikuwako Walawi wawili, Yozabadi mwana wa Yeshua na Noadia mwana wa Binui.
A czwartego dnia odważono srebro, złoto i naczynia w domu naszego Boga – do ręki Meremota, syna kapłana Uriasza, z którym był Eleazar, syn Pinchasa; z nimi też [byli] Jozabad, syn Jeszuy, i Noadiasz, syn Binnuja, Lewici;
34 Kila kitu kilihesabiwa kwa idadi na kupimwa kwa uzito, nao uzito wote uliandikwa wakati ule.
Wszystko według liczby i wagi; i zapisano wagę tego wszystkiego w tym czasie.
35 Kisha mateka waliokuwa wamerudi kutoka utumwani wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Mungu wa Israeli: mafahali kumi na wawili kwa ajili ya Israeli wote, kondoo dume tisini na sita, wana-kondoo sabini na saba na mbuzi dume kumi na wawili kuwa sadaka ya dhambi. Hii yote ilikuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto kwa Bwana.
Następnie ci, którzy zostali pojmani, a powrócili z niewoli, złożyli Bogu Izraela ofiarę całopalną: dwanaście cielców za całego Izraela, dziewięćdziesiąt sześć baranów, siedemdziesiąt siedem jagniąt i dwanaście kozłów na ofiarę za grzech, wszystko jako całopalenie PANU.
36 Pia walikabidhi manaibu wa mfalme na watawala wa Ngʼambo ya Mto Frati maagizo ya mfalme, ambao baadaye walitoa msaada kwa watu na kwa nyumba ya Mungu.
I przekazano rozporządzenie króla jego satrapom i namiestnikom zarzecza, a ci wspomagali lud i dom Boży.

< Ezra 8 >