< 1 Timotheo 4 >

1 Roho asema waziwazi kwamba katika siku za mwisho baadhi ya watu wataiacha imani na kufuata roho zidanganyazo na mafundisho ya mashetani.
Now the Spirit expressly declares that in later times some will fall away from the faith, giving heed to deceiving spirits and the teachings of demons;
2 Mafundisho kama hayo huja kupitia kwa waongo ambao ni wanafiki, hali dhamiri zao zikiungua kwa kuchomwa moto.
through the hypocrisy of men who teach falsely and have their own consciences seared as with a hot iron;
3 Wao huwakataza watu wasioe na kuwaagiza wajiepushe na vyakula fulani, ambavyo Mungu aliviumba ili vipokewe kwa shukrani na wale wanaoamini na kuijua kweli.
forbidding people to marry, and insisting on abstinence from foods which God has created to be partaken of, with thankfulness, by those who believe and have a clear knowledge of the truth.
4 Kwa maana kila kitu alichokiumba Mungu ni chema, wala hakuna kitu chochote cha kukataliwa kama kikipokewa kwa shukrani,
For everything that God has created is good, and nothing is to be cast aside, if only it is received with thanksgiving.
5 kwa sababu kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.
For it is made holy by the word of God and by prayer.
6 Kama ukiwakumbusha ndugu mambo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, uliyelelewa katika kweli ya imani na yale mafundisho mazuri uliyoyafuata.
If you warn the brethren of these dangers you will be a good and faithful servant of Christ Jesus, inwardly feeding on the lessons of the faith and of the sound teaching of which you have been, and are, so close a follower.
7 Usijishughulishe kamwe na hadithi za kipagani na masimulizi ya uongo ya wanawake wazee; badala yake, jizoeze kuwa mtauwa.
But worldly stories, fit only for credulous old women, have nothing to do with.
8 Kwa maana mazoezi ya mwili yana faida kwa sehemu, lakini utauwa una faida katika mambo yote, yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa na ya ule ujao.
Train yourself in godliness. Exercise for the body is not useless, but godliness is useful in every respect, possessing, as it does, the promise of Life now and of the Life which is soon coming.
9 Hili ni neno la kuaminiwa tena lastahili kukubaliwa kabisa,
Faithful is this saying and deserving of universal acceptance:
10 (nasi kwa ajili ya hili tunajitaabisha na kujitahidi), kwamba tumeweka tumaini letu kwa Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, hasa wale waaminio.
and here is the motive of our toiling and wrestling, because we have our hopes fixed on the ever-living God, who is the Saviour of all mankind, and especially of believers.
11 Mambo haya yaagize na kuyafundisha.
Command this and teach this.
12 Mtu yeyote asikudharau kwa kuwa wewe ni kijana, bali uwe kielelezo kizuri kwa waumini katika usemi, mwenendo, upendo, imani na usafi.
Let no one think slightingly of you because you are a young man; but in speech, conduct, love, faith and purity, be an example for your fellow Christians to imitate.
13 Fanya bidii kusoma Maandiko hadharani, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
Till I come, bestow your attention on reading, exhortation and teaching.
14 Usiache kutumia kipawa kilicho ndani yako, ambacho ulipewa kwa neno la unabii wakati wazee walikuwekea mikono.
Do not be careless about the gifts with which you are endowed, which were conferred on you through a divine revelation when the hands of the elders were placed upon you.
15 Uwe na bidii katika mambo haya; ujitolee kwa ajili ya mambo haya kikamilifu, ili kila mtu aone kuendelea kwako.
Habitually practise these duties, and be absorbed in them; so that your growing proficiency in them may be evident to all.
16 Jilinde sana nafsi yako na mafundisho yako. Dumu katika hayo, kwa maana kwa kufanya hivyo, utajiokoa wewe mwenyewe pamoja na wale wanaokusikia.
Be on your guard as to yourself and your teaching. Persevere in these things; for by doing this you will make certain your own salvation and that of your hearers.

< 1 Timotheo 4 >