< 2 Wathesalonike 1 >

1 Paulo, Silvano na Timotheo: Kwa kanisa la Wathesalonike mlio katika Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo:
Paul, Silas, and Timothy: To the Church of the Thessalonians which is in God our Father and the Lord Jesus Christ.
2 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
May grace and peace be granted to you from God our Father and the Lord Jesus Christ.
3 Ndugu, imetubidi kumshukuru Mungu kwa ajili yenu siku zote, kama ulivyo wajibu wetu, kwa sababu imani yenu inakua zaidi na zaidi na upendo wa kila mmoja wenu alio nao kwa mwenzake unazidi kuongezeka.
Unceasing thanks are due from us to God on your behalf, brethren. They are appropriate because your faith is growing greatly, and the love of every one of you for all the others goes on increasing.
4 Ndiyo sababu miongoni mwa makanisa ya Mungu, tunajivuna kuhusu saburi yenu na imani mliyo nayo katika mateso yote na dhiki mnazostahimili.
It so increases that we ourselves make honourable mention of you among the Churches of God because of your patience and faith amid all your persecutions and amid the afflictions which you are enduring.
5 Haya yote ni uthibitisho kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na kwa sababu hiyo ninyi mtahesabiwa kwamba mnastahili kuwa wa Ufalme wa Mungu, mnaoteswa kwa ajili wake.
For these are a plain token of God's righteous judgement, which has in view your being deemed worthy of admission to God's Kingdom, for the sake of which, indeed, you are sufferers.
6 Mungu ni mwenye haki: yeye atawalipa mateso wale wawatesao ninyi
A plain token of God's righteous judgement, I say, since it is a righteous thing for Him to requite with affliction those who are now afflicting you;
7 na kuwapa ninyi mnaoteseka raha pamoja na sisi, wakati Bwana Yesu atakapodhihirishwa kutoka mbinguni katika mwali wa moto pamoja na malaika wake wenye nguvu.
and to requite with rest you who are suffering affliction now--rest with us at the re-appearing of the Lord Jesus from Heaven, attended by His mighty angels.
8 Atawaadhibu wale wasiomjua Mungu na ambao hawakuitii Injili ya Bwana wetu Yesu.
He will come in flames of fire to take vengeance on those who have no knowledge of God, and do not obey the Good News as to Jesus, our Lord.
9 Wataadhibiwa kwa uangamivu wa milele na kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa uweza wake, (aiōnios g166)
They will pay the penalty of eternal destruction, being banished from the presence of the Lord and from His glorious majesty, (aiōnios g166)
10 siku hiyo atakapokuja kutukuzwa katika watakatifu wake na kustaajabiwa miongoni mwa wote walioamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwa hawa kwa sababu mliamini ushuhuda wetu kwenu.
when He comes on that day to be glorified in His people and to be wondered at among all who have believed, including you--because you believed the testimony which we brought for your acceptance.
11 Kwa sababu hii, tunawaombea ninyi bila kukoma, ili Mungu apate kuwahesabu kuwa mnastahili wito wake na kwamba kwa uwezo wake apate kutimiza kila kusudi lenu jema na kila tendo linaloongozwa na imani yenu.
It is with this view also that we continually pray to our God for you, asking that He will count you worthy of His call, and by His mighty power fully gratify your every desire for what is truly good and make your work of faith complete;
12 Tunaomba hivi ili Jina la Bwana wetu Yesu lipate kutukuzwa ndani yenu, nanyi ndani yake, kulingana na neema ya Mungu wetu na Bwana Yesu Kristo.
in order that the name of our Lord Jesus may be glorified in you, and that you may be glorified in Him--so wonderful is the grace of our God and of the Lord Jesus Christ!

< 2 Wathesalonike 1 >