< 1 Timotheo 2 >

1 Awali ya yote, nasihi kwamba dua, sala, maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote:
I exhort then, first of all, that supplications, prayers, intercessions and thanksgivings be offered on behalf of all men;
2 kwa ajili ya wafalme na wale wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi kwa amani na utulivu, katika uchaji wote wa Mungu na utakatifu.
including kings and all who are in high station, in order that we may live peaceful and tranquil lives with all godliness and gravity.
3 Jambo hili ni jema, tena linapendeza machoni pa Mungu Mwokozi wetu,
This is right, and is pleasing in the sight of God our Saviour,
4 anayetaka watu wote waokolewe na wafikie kuijua kweli.
who is willing for all mankind to be saved and come to a full knowledge of the truth.
5 Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, yaani mwanadamu Kristo Yesu,
For there is but one God and but one Mediator between God and men--Christ Jesus, Himself man;
6 aliyejitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wanadamu wote: jambo hili lilishuhudiwa kwa wakati wake ufaao.
who gave Himself as the redemption price for all--a fact testified to at its own appointed time,
7 Nami kwa kusudi hili nimewekwa niwe mhubiri na mtume (nasema kweli katika Kristo wala sisemi uongo), mwalimu wa watu wa Mataifa katika imani na kweli.
and of which I have been appointed a herald and an Apostle (I am speaking the truth: it is not a fiction), a teacher of the Gentiles in faith and truth.
8 Nataka kila mahali wanaume wasali wakiinua mikono mitakatifu pasipo hasira wala kugombana.
So then I would have the men everywhere pray, lifting to God holy hands which are unstained with anger or strife;
9 Vivyo hivyo nataka wanawake wajipambe kwa adabu na kwa heshima katika mavazi yanayostahili, si kwa kusuka nywele, kuvalia dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
and I would have the women dress becomingly, with modesty and self-control, not with plaited hair or gold or pearls or costly clothes,
10 bali kwa matendo mazuri kama iwapasavyo wanawake wanaokiri kuwa wanamcha Mungu.
but--as befits women making a claim to godliness--with the ornament of good works.
11 Mwanamke na ajifunze kwa utulivu na kwa utiifu wote.
A woman should quietly learn from others with entire submissiveness.
12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha au kuwa na mamlaka juu ya mwanaume. Mwanamke inampasa kukaa kimya.
I do not permit a woman to teach, nor have authority over a man, but she must remain silent.
13 Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.
For Adam was formed first, and then Eve;
14 Wala si Adamu aliyedanganywa, bali ni mwanamke aliyedanganywa akawa mkosaji.
and Adam was not deceived, but his wife was thoroughly deceived, and so became involved in transgression.
15 Lakini mwanamke ataokolewa kwa kuzaa kwake, kama wakiendelea kudumu katika imani, upendo na utakatifu, pamoja na kuwa na kiasi.
Yet a woman will be brought safely through childbirth if she and her husband continue to live in faith and love and growing holiness, with habitual self-restraint.

< 1 Timotheo 2 >