< 1 Wathesalonike 4 >

1 Hatimaye, ndugu, tuliwaomba na kuwasihi katika Bwana Yesu kwamba, kama mlivyojifunza kutoka kwetu jinsi iwapasavyo kuishi ili kumpendeza Mungu, kama vile mnavyoishi, imewapasa mzidi sana kufanya hivyo.
Moreover, brethren, as you learnt from our lips the lives which you ought to live, and do live, so as to please God, we beg and exhort you in the name of the Lord Jesus to live them more and more truly.
2 Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa mamlaka ya Bwana Yesu.
For you know the commands which we laid upon you by the authority of the Lord Jesus.
3 Mapenzi ya Mungu ni kwamba ninyi mtakaswe, ili kwamba mjiepushe na zinaa,
For this is God's will--your purity of life, that you abstain from fornication;
4 ili kwamba kila mmoja wenu ajifunze kuutawala mwili wake mwenyewe katika utakatifu na heshima,
that each man among you shall know how to procure a wife who shall be his own in purity and honour;
5 si kwa tamaa mbaya kama watu wa Mataifa wasiomjua Mungu.
that you be not overmastered by lustful cravings, like the Gentiles who have no knowledge of God;
6 Katika jambo hili mtu asimkosee ndugu yake wala kumlaghai. Kwa kuwa Bwana ni mlipiza kisasi katika mambo haya yote, kama vile tulivyokwisha kuwaambia mapema na kuwaonya vikali.
and that in this matter there be no encroaching on the rights of a brother Christian and no overreaching him. For the Lord is an avenger in all such cases, as we have already taught you and solemnly warned you.
7 Kwa maana Mungu hakutuitia uchafu, bali utakatifu.
God has not called us to an unclean life, but to one of purity.
8 Kwa hiyo, mtu yeyote anayekataa mafundisho haya hamkatai mwanadamu, bali anamkataa Mungu anayewapa ninyi Roho wake Mtakatifu.
Therefore a defiant spirit in such a case provokes not man but God, who puts His Holy Spirit into your hearts.
9 Sasa kuhusu upendo wa ndugu hamna haja mtu yeyote kuwaandikia, kwa maana ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu kupendana.
But on the subject of love for the brotherhood it is unnecessary for me to write to you, for you yourselves have been taught by God to love one another;
10 Nanyi kwa kweli mnawapenda ndugu wote katika Makedonia nzima. Lakini ndugu, tunawasihi mzidi sana kuwapenda.
and indeed you do love all the brethren throughout Macedonia. And we exhort you to do so more and more,
11 Jitahidini kuishi maisha ya utulivu, kila mtu akijishughulisha na mambo yake mwenyewe na kufanya kazi kwa mikono yake, kama vile tulivyowaagiza,
and to vie with one another in eagerness for peace, every one minding his own business and working with his hands, as we ordered you to do:
12 ili maisha yenu ya kila siku yajipatie heshima kutoka kwa watu walio nje, ili msimtegemee mtu yeyote.
so as to live worthy lives in relation to outsiders, and not be a burden to any one.
13 Lakini ndugu, hatutaki mkose kujua kuhusu wale waliolala mauti, ili msihuzunike kama watu wengine wasiokuwa na tumaini.
Now, concerning those who from time to time pass away, we would not have you to be ignorant, brethren, lest you should mourn as others do who have no hope.
14 Kwa kuwa tunaamini kwamba Yesu alikufa na kufufuka, na kwa hivyo, Mungu kwa njia ya Yesu atawafufua pamoja naye wale waliolala mautini ndani yake.
For if we believe that Jesus has died and risen again, we also believe that, through Jesus, God will bring with Him those who shall have passed away.
15 Kulingana na neno la Bwana mwenyewe, tunawaambia kwamba sisi ambao bado tuko hai, tuliobaki hadi kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia waliolala mauti.
For this we declare to you on the Lord's own authority--that we who are alive and continue on earth until the Coming of the Lord, shall certainly not forestall those who shall have previously passed away.
16 Kwa maana Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni, akitoa amri kwa sauti kuu, pamoja na sauti ya malaika mkuu, na sauti ya tarumbeta ya Mungu. Nao waliokufa wakiwa katika Kristo watafufuka kwanza.
For the Lord Himself will come down from Heaven with a loud word of command, and with an archangel's voice and the trumpet of God, and the dead in Christ will rise first.
17 Baada ya hilo sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu ili kumlaki Bwana hewani, hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.
Afterwards we who are alive and are still on earth will be caught up in their company amid clouds to meet the Lord in the air.
18 Kwa hiyo farijianeni kwa maneno haya.
And so we shall be with the Lord for ever. Therefore encourage one another with these words.

< 1 Wathesalonike 4 >