< 1 Wathesalonike 1 >

1 Paulo, Silvano na Timotheo: Kwa kanisa la Wathesalonike, ninyi mlio ndani ya Mungu Baba yetu na ndani ya Bwana Yesu Kristo: Neema iwe kwenu na amani.
Paul, Silas, and Timothy: To the Church of the Thessalonians which is in God the Father and the Lord Jesus Christ. May grace and peace be granted to you.
2 Siku zote tunamshukuru Mungu kwa ajili yenu ninyi nyote, tukiwataja kwenye maombi yetu daima.
We continually give thanks to God because of you all, while we make mention of you in our prayers.
3 Tunaikumbuka daima kazi yenu ya imani mbele za Mungu aliye Baba yetu, taabu yenu katika upendo na saburi yenu ya tumaini katika Bwana wetu Yesu Kristo.
For we never fail to remember your works of faith and labours of love and your persistent and unwavering hope in our Lord Jesus Christ in the presence of our God and Father;
4 Ndugu zetu mpendwao na Mungu, kwa kuwa tunajua kwamba Mungu amewachagua,
knowing as we do, brethren, that you are beloved by God and that He has chosen you.
5 kwa sababu ujumbe wetu wa Injili haukuja kwenu kwa maneno matupu bali pia ulidhihirishwa katika nguvu na katika Roho Mtakatifu, tena ukiwa na uthibitisho kamili, kama vile ninyi wenyewe mnavyojua jinsi tulivyoenenda katikati yenu kwa ajili yenu.
The Good News that we brought you did not come to you in words only, but also with power and with the Holy Spirit and with much certainty, for you know the sort of men we became among you, as examples for your sakes.
6 Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, ingawa mlipata mateso mengi, mlilipokea lile Neno kwa furaha katika Roho Mtakatifu.
And you followed the pattern set you by us and by the Master, after you had received the Message amid severe persecution, and yet with the joy which the Holy Spirit gives,
7 Hivyo ninyi mkawa kielelezo kwa waumini wote katika Makedonia na Akaya.
so that you became a pattern to all the believers throughout Macedonia and Greece.
8 Kwa maana kutoka kwenu neno la Bwana limesikika, si katika Makedonia na Akaya tu, bali pia imani yenu katika Mungu imejulikana kila mahali kiasi kwamba hatuna haja ya kusema lolote kwa habari yake.
For it was not only from you that the Master's Message sounded forth throughout Macedonia and Greece; but everywhere your faith in God has become known, so that it is unnecessary for us to say anything about it.
9 Kwa maana watu wa maeneo hayo wenyewe wanaeleza jinsi mlivyotupokea na jinsi mlivyomgeukia Mungu mkaacha sanamu, ili kumtumikia Mungu aliye hai na wa kweli
For when others speak of us they report the reception we had from you, and how you turned from your idols to God, to be bondservants of the true and ever-living God,
10 na ili kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu: yaani, Yesu, yeye aliyetuokoa kutoka ghadhabu inayokuja.
and to await the return from Heaven of His Son, whom He raised from among the dead--even Jesus, our Deliverer from God's coming anger.

< 1 Wathesalonike 1 >