< 1 Wafalme 7 >

1 Ilimchukua Solomoni miaka kumi na mitatu kukamilisha ujenzi wa Jumba lake la kifalme.
Bet pie sava nama Salamans strādāja trīspadsmit gadus, kamēr visu namu pabeidza.
2 Alijenga Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni, urefu wake ulikuwa dhiraa 100, upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini, likiwa na safu nne za nguzo za mierezi zikishikilia boriti za mierezi zilizorembwa.
Un viņš taisīja namu no Lībanus kokiem, simts olektis garumā un piecdesmit olektis platumā un trīsdesmit olektis augstumā, uz četrām ciedru stabu rindām, un uz tiem stabiem bija ciedru sijas.
3 Ilipauliwa kwa mierezi juu ya boriti zile zilizolala juu ya nguzo arobaini na tano, kumi na tano kwa kila safu.
Un ciedru griesti bija virsū uz tām istabām, kas uz tiem stabiem; šo bija četrdesmit pieci pa piecpadsmit ikkatrā rindā.
4 Madirisha yake yaliwekwa juu kwa safu tatu, yakielekeana.
Un treji griesti bija, tā ka logs logam stāvēja pretī trejās kārtās.
5 Milango yote ilikuwa na miimo ya mstatili, ilikuwa upande wa mbele katika safu tatu, ikielekeana.
Un visas durvis un logi bija četrkantīgi no baļķiem, un logs logam bija pretī trijās kārtās.
6 Akajenga ukumbi wa nguzo, ambao urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa thelathini. Mbele ya jengo hilo kulikuwepo baraza. Mbele ya baraza kulikuwepo na nguzo na paa lililoningʼinia.
Viņš arī taisīja namu uz stabiem, piecdesmit olektis garumā un trīsdesmit olektis platumā, un vēl vienu namu šim priekšā, un tiem priekšā stabus un slieksni.
7 Akajenga ukumbi wa kiti cha enzi, Ukumbi wa Hukumu, mahali ambapo angelitolea hukumu, akaufunika kwa mierezi kutoka sakafuni hadi darini.
Viņš arī taisīja namu goda krēslam, kur tiesu turēja, soģa namu, un to apsita ar ciedru galdiem no grīdas līdz griestiem.
8 Kwenye jumba la kifalme ambamo angeliishi, aliiweka nyuma zaidi, ikiwa na mjengo wa aina moja na hiyo nyingine. Pia Solomoni akajenga jumba la kifalme linalofanana na huo ukumbi mkubwa kwa ajili ya binti Farao, aliyekuwa amemwoa.
Un viņa paša nams, kur viņš dzīvoja, otrā pagalmā aiz šī nama, tāpat bija taisīts. Un Faraona meitai, ko Salamans bija apņēmis, viņš taisīja namu, kā šo namu.
9 Ujenzi huu wote, kuanzia nje mpaka kwenye ua mkuu na kuanzia kwenye msingi hadi upenuni, ulifanywa kwa mawe ya ubora wa hali ya juu yaliyokuwa yamechongwa kwa vipimo na kusawazishwa kwa msumeno nyuso zake za ndani na za nje.
Viss tas bija no dārgiem, pēc mēra cirstiem un ar zāģiem zāģētiem akmeņiem iekšpusē un ārpusē no pamata līdz jumtam un ārpusē līdz tam lielam pagalmam.
10 Misingi iliwekwa kwa mawe makubwa yaliyo bora, yenye urefu wa dhiraa kumi na mengine yenye urefu wa dhiraa nane
Un tie pamata akmeņi bija arī lieli dārgi akmeņi no desmit olektīm un akmeņi no astoņām olektīm.
11 Sehemu za juu kulikuwepo na mawe yenye ubora wa hali ya juu, yaliyokatwa kwa vipimo na boriti za mierezi.
Un uz tiem bija dārgi, pēc mēra izcirsti akmeņi un ciedru koki.
12 Ule ua mkuu ulizungukwa na ukuta wa safu tatu za mawe yaliyochongwa na safu moja ya boriti za mierezi zilizorembwa, kama ulivyokuwa ua wa ndani wa Hekalu la Bwana na baraza yake.
Bet tam lielam pagalmam bija visapkārt trīs rindas cirstu akmeņu un viena rinda ciedru baļķu; tāpat bija arī Tā Kunga nama iekšējais pagalms un tā nama priekšnams.
13 Mfalme Solomoni akatuma watu Tiro kumleta Hiramu,
Un ķēniņš Salamans sūtīja un lika atvest Hiramu no Tirus.
14 ambaye mama yake alikuwa mjane kutoka kabila la Naftali na baba yake alikuwa mtu wa Tiro tena fundi wa shaba. Hiramu alikuwa na ustadi wa hali ya juu na mzoefu katika aina zote za kazi ya shaba. Alikuja kwa Mfalme Solomoni na kufanya kazi zake zote alizopangiwa.
Tas bija atraitnes dēls no Naftalus cilts, un viņa tēvs bija bijis vīrs no Tirus, vara kalējs. Tas bija pilns gudrības un saprašanas un zināšanas, visādu vara darbu darīt. Šis nāca pie ķēniņa Salamana un strādāja visus viņa darbus.
15 Hiramu akasubu nguzo mbili za shaba, kila moja ikiwa na urefu wa dhiraa kumi na nane, kila nguzo ikiwa na mzingo wa dhiraa kumi na mbili kwa mstari.
Un viņš taisīja divus vara stabus; katrs stabs bija astoņpadsmit olektis augsts un divpadsmit olektis bija mērs ap katru stabu.
16 Pia alitengeneza mataji mawili ya shaba ya kusubu ili kuyaweka juu ya hizo nguzo; kila taji lilikuwa na kimo cha dhiraa tano kwenda juu.
Viņš taisīja arī divus kroņus no vara izlietus, liekamus uz stabu virsgaliem, piecas olektis bija katra kroņa augstums.
17 Wavu wa mikufu iliyosokotewa kwenye zile taji juu ya zile nguzo, saba kwa kila taji.
Un tie kroņi uz tiem stabiem bija aptīti kā ar tīkliem un apvīti kā ar ķēdēm, septiņas bija vienam kronim un septiņas otram.
18 Akatengeneza makomamanga katika safu mbili kuzunguka kila wavu kuremba mataji yaliyo juu ya nguzo. Alifanya hivyo kwa kila nguzo.
Tā viņš taisīja tos stabus un divās rindas granātābolu ap to tīkla darbu, apsegt tos kroņus, kas bija augšām; tā viņš taisīja arī tam otram kronim.
19 Mataji yaliyokuwa juu ya nguzo kwenye baraza, yalikuwa katika umbo la yungiyungi, kimo chake ni dhiraa nne
Un tie kroņi uz tiem diviem stabiem bija kā lilijas taisīti tai namā, četras olektis (augstumā).
20 Juu ya mataji ya zile nguzo mbili, juu ya ile sehemu yenye umbo kama bakuli, karibu na ule wavu, kulikuwa na yale makomamanga 200 katika safu kuzunguka pande zote.
Un tie kroņi bija uz tiem diviem stabiem un augšām pār to apaļumu bija divsimt granātābolu visapkārt rindās aiz tā tīkla darba; tāpat arī pie tā otra kroņa.
21 Hiramu akasimamisha nguzo kwenye baraza ya Hekalu. Nguzo ya upande wa kusini akaiita Yakini, na ile ya upande wa kaskazini Boazi.
Un viņš uzcēla tos stabus Dieva nama pagalmā, un to stabu, ko viņš pa labo roku bija uzcēlis, viņš nosauca: Jaķin, un to stabu, ko viņš pa kreiso roku bija uzcēlis, viņš nosauca: Boas.
22 Mataji yaliyokuwa juu yalikuwa na umbo la yungiyungi. Hivyo kazi ya nguzo ikakamilika.
Un augšām uz tiem stabiem bija tas liliju darbs. Tā tas stabu darbs tapa pabeigts.
23 Hiramu akasubu Bahari ya chuma, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Mzunguko wake ulikuwa dhiraa thelathini.
Un viņš taisīja arī vara lietu ūdens trauku, desmit olektis bija no viņa vienas malas līdz otrai malai, visapkārt apaļu, un piecas olektis bija viņa augstums, un tas mērs visapkārt bija trīsdesmit olektis.
24 Chini ya ukingo, ilizungukwa na maboga, kumi kwenye kila dhiraa moja. Maboga yalikuwa yamesubiwa katika safu mbili ili kuwa kitu kimoja na hiyo bahari.
Un apakšā pie viņa malas bija pogas visapkārt, desmit uz ikvienu olekti, un ap to trauku bija divas rindas no tādām pogām, vienā lējienā lietas.
25 Bahari iliwekwa juu ya mafahali kumi na wawili, watatu wakielekea kaskazini, watatu wakielekea magharibi, watatu wakielekea kusini na watatu wakielekea mashariki. Bahari iliwekwa juu yao na sehemu zao za nyuma zilielekeana.
Un tas stāvēja uz divpadsmit vēršiem; no tiem trīs griezās pret ziemeļa pusi un trīs griezās pret vakara pusi un trīs pret dienvidu pusi un trīs pret rīta pusi un tas vara trauks bija virsū uz tiem, un visas viņu pakaļpuses bija iekšpusē.
26 Ilikuwa na unene wa nyanda nne na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 2,000.
Un viņa biezums bija plaukstas platumā, un viņa mala bija kā kāda biķera mala, kā lilijas zieds; divi tūkstoši batu mēri tanī sagāja.
27 Pia akatengeneza vitako kumi vya shaba vinavyoweza kuhamishika, kila kimoja kilikuwa na urefu wa dhiraa nne, upana dhiraa nne na kimo chake dhiraa tatu
Viņš taisīja arī desmit vara krēslus, četras olektis bija krēsla garums un četras olektis viņa platums un trīs olektis viņa augstums.
28 Hivi ndivyo vile vitako vilivyotengenezwa: Vilikuwa na mbao za pembeni zilizoshikamanishwa na mihimili.
Un tie krēsli tā bija taisīti: tiem bija sāngaldi starp līstēm.
29 Juu ya mbao kati ya hiyo mihimili kulikuwa na simba, mafahali na makerubi, pia kwenye mihimili yake. Juu na chini ya simba na mafahali kulikuwa kumesokotewa taji za kufuliwa.
Un uz tiem sāngaldiem starp līstēm bija lauvas, vērši un ķerubi, un uz tām līstēm virs un apakš lauvām un vēršiem bija vēl kroņi, kas karājās.
30 Kila kitako kilikuwa na magurudumu manne ya shaba, na vyuma vya katikati vya kuyazungusha hayo magurudumu na kila kimoja kilikuwa na sinia kwenye vishikizo vinne vya taji iliyosubiwa kila upande.
Un ikkatram krēslam bija četri vara riteņi ar vara asīm. Un viņu četriem stūriem bija turamie, apakš tā katla bija šie vara turamie kroņiem pretī.
31 Ndani ya kitako kulikuwa na nafasi ya wazi iliyokuwa na umbile la mviringo lenye kina cha dhiraa moja. Nafasi hii ya wazi ilikuwa ya mviringo, pamoja na kitako chake ilikuwa dhiraa moja na nusu. Kuzunguka huo mdomo wake kulitiwa nakshi. Papi za vitako zilikuwa mraba na si za mviringo.
Un augšā kroņa iekšpusē tam bija olekts liels caurums un tam apkārt bija taisīta apaļa mala no pusotrām olektīm, un tai caurumā bija izrakstītas bildes, un krēslu sānu galdi bija četrkantīgi un ne apaļi.
32 Magurudumu manne yalikuwa chini ya papi, na vyuma vya katikati vya kuzungushia magurudumu hayo vilikuwa vimeunganishwa kwenye kitako. Kipenyo cha kila gurudumu kilikuwa dhiraa moja na nusu.
Un tie četri riteņi bija tiem sānu galdiem apakšā, un riteņu asis bija pie tiem krēsliem, un ikkatrs ritenis bija pusotras olekts augsts.
33 Magurudumu yalitengenezwa kama ya magari ya vita ya kukokotwa, vyuma vya katikati vya magurudumu, duara zake, matindi yake na vikombe vyake vyote vilikuwa vya kusubu.
Un tie riteņi bija taisīti tāpat kā ratu riteņi; viņu asis un viņu rumbas un viņu spieķi un viņu loki bija visi lieti.
34 Kila kitako kilikuwa na mikono minne, moja kwenye kila pembe, ukitokeza kutoka kwenye kitako.
Un tie četri turamie bija uz ikviena krēsla četriem stūriem uz augšu no tā krēsla.
35 Juu ya kitako kulikuwepo na utepe wa mviringo wenye kina cha nusu dhiraa. Vishikio na papi vilishikamana upande wa juu wa kitako.
Un augšā uz tā krēsla bija apaļa mala visapkārt pusolekts augstumā, un augšā uz tā krēsla bija viņa turamie un viņa sāngaldi pie viņa.
36 Alitia nakshi za makerubi, simba na miti ya mitende juu ya uso wa vishikio na juu ya papi, katika kila nafasi iliyopatikana, pamoja na mataji yaliyosokotwa kuzunguka pande zote.
Un uz viņa turamo sāniem un uz viņa sāngaldiem viņš izgrieza ķerubus, lauvas un palmu kokus, kā ikkatram vietas bija, un kroņi bija visapkārt.
37 Hivi ndivyo Hiramu alivyotengeneza vile vitako kumi. Vyote vilikuwa vya kusubu kwenye kalibu za kufanana kwa vipimo na kwa umbo.
Tā viņš taisīja tos desmit krēslus, visi bija vienādi lieti, pēc viena mēra, pēc viena izskata.
38 Kisha akatengeneza masinia kumi ya shaba, kila moja likiwa na ujazo wa bathi arobaini, yakiwa na kipenyo cha dhiraa nne kila sinia moja kwa kila kimoja ya vile vitako kumi.
Viņš taisīja arī desmit vara katlus, ikkatrā katlā sagāja četrdesmit bati, ikkatrs katls bija četras olektis plats, uz ikviena krēsla no tiem desmit krēsliem bija viens katls.
39 Aliweka vitako vitano upande wa kusini wa Hekalu na vingine vitano upande wa kaskazini. Akaweka ile bahari upande wa kusini, katika pembe ya kusini ya Hekalu.
Un viņš lika piecus no tiem krēsliem nama labajā pusē, un piecus viņš lika kreisajā nama pusē, bet to vara trauku viņš lika labajā nama pusē, uz to pusi starp rītiem un dienasvidu.
40 Pia akatengeneza masinia, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi zote katika Hekalu la Bwana kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
Hirams taisīja arī podus, lāpstas un bļodas, un Hirams pabeidza visu to darbu, ko viņš ķēniņam Salamanam darīja priekš Tā Kunga nama:
41 nguzo mbili; mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo; nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo;
(Proti) tos divus stabus un apaļus kroņus uz tiem diviem stabiem, un tos divus pinumus, kas apsedza tos divus apaļos kroņus stabu virsgalos,
42 makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu, yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
Un tos četrsimt granātābolus pie tiem diviem pinumiem, divas rindas granātābolu pie ikkatra pinuma, kas apsedza tos divus apaļos kroņus uz tiem stabiem,
43 vitako kumi pamoja na masinia yake kumi;
Un tos desmit krēslus un tos desmit katlus krēslu virsu,
44 ile Bahari ya chuma na yale mafahali kumi na wawili chini yake;
Un to vienu vara trauku un tos divpadsmit vēršus apakš tā vara trauka,
45 masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Vyombo hivi vyote ambavyo Huramu alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyongʼarishwa.
Un tos podus un tās lāpstas un bļodas. Un visi tie rīki, ko Hirams ķēniņam Salamanam taisīja priekš Dieva nama, bija no spoža vara.
46 Mfalme akaamuru wavisubu katika kalibu ya udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani ulio kati ya Sukothi na Sarethani.
Jardānes klajumā ķēniņš tos lika liet cietā zemē starp Sukotu un Cartanu.
47 Solomoni akaviacha vitu hivi vyote bila kupima uzani wake, kwa sababu vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
Un Salamans pameta nesvērtus visus šos rīkus tā gauži lielā svara dēļ; vara svars palika nezināms.
48 Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana: madhabahu ya dhahabu; meza ya dhahabu za kuweka mikate ya Wonyesho;
Salamans taisīja arī visus rīkus priekš Tā Kunga nama, zelta altāri un zelta galdu tām priekšā liekamām maizēm,
49 vinara vya taa vya dhahabu safi (vitano upande wa kuume na vitano upande wa kushoto, mbele ya Patakatifu pa Patakatifu); kazi ya maua ya dhahabu na taa na makoleo;
Un lukturus, piecus pa labo roku un piecus pa kreiso roku, visusvētākās vietas priekšā, no tīra zelta ar zelta puķēm un eļļas lukturīšiem un zelta lukts(dakts) šķērēm.
50 masinia ya dhahabu safi, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, vyano na vyetezo; na bawaba za dhahabu kwa ajili ya milango ya chumba cha ndani sana, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na pia kwa ajili ya milango ya ukumbi mkuu wa Hekalu.
Un kausus, nažus un bļodas un karotes un kvēpināšanas traukus no tīra zelta; ir tās durvju eņģes nama iekšpusē visusvētākā vietā un pie Dieva nama durvīm bija no zelta.
51 Hivyo Mfalme Solomoni alipomaliza kazi ya Hekalu la Bwana, akaviingiza ndani vile vitu ambavyo Daudi baba yake alikuwa ameviweka wakfu: yaani fedha, dhahabu na samani; kisha akaviweka katika hazina za Hekalu la Bwana.
Tā viss darbs tapa pabeigts, ko ķēniņš Salamans pie Tā Kunga nama darīja. Un Salamans tur ienesa sava tēva Dāvida Dievam svētītās dāvanas, sudrabu un zeltu un tos rīkus, un tos nolika pie Tā Kunga nama mantām.

< 1 Wafalme 7 >