< 2 Wafalme 1 >

1 Baada ya kifo cha Mfalme Ahabu, nchi ya Moabu iliasi dhidi ya Israeli.
Un Moabs atkāpās no Israēla, kad Ahabs bija nomiris.
2 Basi Ahazia alikuwa ameanguka huko Samaria kutoka baraza ya chumba chake cha juu, akaumia. Hivyo akatuma wajumbe, akiwaambia, “Nendeni mkaulize kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni, mkaone kama nitapona kutokana na kuumia huku.”
Un Ahazija nokrita caur savas augšistabas treliņiem Samarijā, un sasitās un sūtīja vēstnešus un tiem sacīja: ejat un vaicājiet BaālZebubu, Ekronas dievu, vai es palikšu vesels?
3 Lakini malaika wa Bwana akamwambia Eliya, Mtishbi, “Panda ukakutane na wajumbe wa mfalme wa Samaria, uwaulize, ‘Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana mnakwenda kumuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni?’
Bet Tā Kunga eņģelis runāja uz Eliju no Tizbes: celies, ej pretī Samarijas ķēniņa vēstnešiem un runā uz tiem: vai tad Dieva nav iekš Israēla, ka jūs ejat, vaicāt BaālZebubu, Ekronas dievu?
4 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana, ‘Hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!’” Hivyo Eliya akaenda.
Tāpēc Tas Kungs tā saka: tu necelsies no tās gultas, kur tu guli, bet tev jāmirst. Un Elija aizgāja.
5 Wajumbe waliporudi kwa mfalme, akawauliza, “Kwa nini mmerudi?”
Tā tie vēstneši nāca atpakaļ pie viņa, un viņš uz tiem sacīja: kāpēc jūs nākat atpakaļ?
6 Wakamjibu, “Mtu fulani alikuja kukutana nasi, naye akatuambia, ‘Rudini kwa mfalme aliyewatuma na mkamwambie, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana unawatuma watu kwenda kuuliza kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa hiyo hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”’”
Un tie uz viņu sacīja: viens vīrs mums nāca pretī un uz mums sacīja: ejat, griežaties atpakaļ pie ķēniņa, kas jūs sūtījis, un sakāt tam: tā saka Tas Kungs: vai tad nav Dieva iekš Israēla, ka tu sūti, vaicāt BaālZebubu, Ekronas dievu? Tāpēc tu necelsies no tās gultas, kur tu guli, bet tev jāmirst.
7 Mfalme akawauliza, “Alikuwa mtu wa namna gani ambaye mlikutana naye, akawaambia hili?”
Un viņš uz tiem sacīja: kādu izskatu tas vīrs bija, kas jums pretī nāca un šos vārdus uz jums runāja?
8 Wakamjibu, “Alikuwa mtu aliyekuwa na vazi la manyoya na mkanda wa ngozi kiunoni mwake.” Mfalme akasema, “Huyo alikuwa ni Eliya, Mtishbi.”
Un tie uz viņu sacīja: tas bija vīrs spalvas drēbēs un ar ādas jostu apjozies ap saviem gurniem. Tad viņš sacīja: tas ir Elija no Tizbes.
9 Ndipo mfalme akamtuma mkuu mmoja wa kikosi pamoja na kikosi chake cha askari hamsini kwa nabii Eliya. Yule mkuu wa kikosi akamwendea Eliya, aliyekuwa ameketi juu ya kilima, na kumwambia, “Mtu wa Mungu, mfalme anasema, ‘Shuka chini!’”
Un viņš pie tā sūtīja virsnieku pār piecdesmit un tos piecdesmit, kas tam bija. Un kad tas pie viņa nonāca, redzi, tad viņš sēdēja kalna galā, un tas uz viņu sacīja: tu Dieva vīrs, ķēniņš tev liek sacīt: nāc lejā.
10 Eliya akamjibu yule mkuu wa kikosi, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza yule mkuu wa kikosi pamoja na watu wake.
Bet Elija atbildēja un sacīja uz to virsnieku pār tiem piecdesmit: ja es esmu Dieva vīrs, tad lai uguns krīt no debesīm un aprij tevi ar taviem piecdesmit. Tad uguns krita no debesīm un aprija to un viņa piecdesmit.
11 Aliposikia hili, mfalme akatuma kwa Eliya mkuu wa kikosi mwingine na askari wake hamsini. Yule mkuu wa kikosi akamwambia Eliya, “Mtu wa Mungu, hili ndilo asemalo mfalme, ‘Shuka chini mara moja!’”
Bet viņš pie tā sūtīja vēl otru virsnieku pār piecdesmit un tos piecdesmit, kas tam bija, un tas bildināja un uz to sacīja: tu Dieva vīrs, tā ķēniņš saka: nāc tūdaļ lejā.
12 Eliya akajibu, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza yeye na watu wake hamsini.
Bet Elija atbildēja un uz tiem sacīja: ja es esmu Dieva vīrs, tad lai uguns krīt no debesīm, un aprij tevi ar taviem piecdesmit. Tad Dieva uguns nokrita no debesīm un aprija to un viņa piecdesmit.
13 Hivyo mfalme akatuma mkuu wa kikosi wa tatu na watu wake hamsini. Huyu mkuu wa kikosi wa tatu akapanda na kupiga magoti mbele ya Eliya, akiomba, “Mtu wa Mungu, tafadhali niachie uhai wangu na uhai wa hawa watu hamsini, watumishi wako!
Bet viņš sūtīja atkal trešo reiz virsnieku pār piecdesmit un tos piecdesmit, kas tam bija. Un tas trešais virsnieks pār piecdesmit nāca augšām un piegāja un metās ceļos priekš Elijas, to lūdza un uz to sacīja: tu Dieva vīrs, lai jel mana dvēsele un šo tavu piecdesmit kalpu dvēseles atrod žēlastību tavās acīs.
14 Tazama, moto umeshuka kutoka mbinguni na kuwateketeza wale wakuu wa vikosi viwili vya kwanza pamoja na watu wao. Lakini sasa niachie uhai wangu!”
Redzi, uguns ir kritis no debesīm un aprijis tos divus pirmos virsniekus pār piecdesmit līdz ar viņu piecdesmitiem, bet nu lai jel mana dvēsele ir dārga tavās acīs.
15 Malaika wa Bwana akamwambia Eliya, “Shuka pamoja naye, usimwogope.” Hivyo Eliya akainuka na kushuka pamoja naye kwa mfalme.
Un Tā Kunga eņģelis sacīja uz Eliju: noej ar viņu un nebīsties no viņa. Tad viņš cēlās un ar to nogāja pie ķēniņa,
16 Akamwambia mfalme, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli wa kumuuliza habari, ndiyo maana ukatuma wajumbe kuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa sababu umefanya hili, kamwe hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”
Un sacīja uz to: tā saka Tas Kungs: tāpēc ka tu vēstnešus esi sūtījis, vaicāt BaālZebubu, Ekronas dievu, kā kad nebūtu Dieva iekš Israēla, kura vārdu varētu vaicāt tāpēc tu necelsies no tās gultas, kur tu guli, bet tev jāmirst.
17 Hivyo akafa, sawasawa na lile neno la Bwana ambalo Eliya alikuwa amesema. Kwa kuwa Ahazia hakuwa na mwana, Yoramu akawa mfalme baada yake katika mwaka wa pili wa Yehoramu mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda.
Tā viņš nomira pēc Tā Kunga vārda, ko Elija bija runājis, un Jorams palika par ķēniņu viņa vietā, Jehorama, Jehošafata dēla, Juda ķēniņa, otrā gadā, jo viņam nebija dēla.
18 Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahazia na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
Un kas vēl stāstāms par Ahaziju, ko viņš darījis, tas viss rakstīts Israēla ķēniņu laiku grāmatā.

< 2 Wafalme 1 >