< 1 Wakorintho 5 >

1 Yamkini habari imeenea ya kuwa miongoni mwenu kuna uzinzi ambao haujatokea hata miongoni mwa watu wasiomjua Mungu: Kwamba mtu anaishi na mke wa baba yake.
It is actually reported that there is fornication among you, and of a kind unheard of even among the Gentiles--a man has his father's wife!
2 Nanyi mwajivuna! Je, haiwapasi kuhuzunika na kumtenga na ushirika wenu mtu huyo aliyefanya mambo hayo?
And you, instead of mourning and removing from among you the man who has done this deed of shame, are filled with self-complacency!
3 Hata kama siko pamoja nanyi katika mwili, niko nanyi katika roho. Nami nimekwisha kumhukumu mtu huyo aliyetenda jambo hili, kama vile ningekuwepo.
I for my part, present with you in spirit although absent in body, have already, as though I were present, judged him who has so acted.
4 Mnapokutana katika Jina la Bwana wetu Yesu nami nikiwepo pamoja nanyi katika roho na uweza wa Bwana Yesu ukiwepo,
In the name of our Lord Jesus, when you are all assembled and my spirit is with you, together with the power of our Lord Jesus,
5 mkabidhini mtu huyu kwa Shetani, ili mwili wake uharibiwe, ili roho yake iokolewe katika siku ya Bwana.
I have handed over such a man to Satan for the destruction of his body, that his spirit may be saved on the day of the Lord Jesus.
6 Majivuno yenu si mazuri. Je, hamjui ya kwamba chachu kidogo huchachusha donge zima la unga?
It is no good thing--this which you make the ground of your boasting. Do you not know that a little yeast corrupts the whole of the dough?
7 Ondoeni chachu ya kale ili mpate kuwa donge jipya lisilotiwa chachu, kama vile mlivyo. Kwa maana Kristo, Mwana-Kondoo wetu wa Pasaka amekwisha tolewa kuwa dhabihu.
Get rid of the old yeast so that you may be dough of a new kind; for in fact you are free from corruption. For our Passover Lamb has already been offered in sacrifice--even Christ.
8 Kwa hiyo, tusiiadhimishe sikukuu hii, kwa chachu ya zamani, chachu ya nia mbaya na uovu, bali kwa mkate usiotiwa chachu, ndio weupe wa moyo na kweli.
Therefore let us keep our festival not with old yeast nor with the yeast of what is evil and mischievous, but with bread free from yeast--the bread of transparent sincerity and of truth.
9 Niliwaandikia katika waraka wangu kuwa msishirikiane na wazinzi.
I wrote to you in that letter that you were not to associate with fornicators;
10 Sina maana kwamba msishirikiane na wazinzi wa ulimwengu huu, au wenye tamaa mbaya, wanyangʼanyi au waabudu sanamu. Kwa kufanya hivyo ingewalazimu mtoke ulimwenguni humu.
not that in this world you are to keep wholly aloof from such as they, any more than from people who are avaricious and greedy of gain, or from worshippers of idols. For that would mean that you would be compelled to go out of the world altogether.
11 Lakini sasa nawaandikia kwamba msishirikiane na mtu yeyote anayejiita ndugu, hali akiwa ni mzinzi, au mwenye tamaa mbaya, mwabudu sanamu au msingiziaji, mlevi au mdhalimu. Mtu kama huyo hata msile naye.
But what I meant was that you were not to associate with any one bearing the name of "brother," if he was addicted to fornication or avarice or idol-worship or abusive language or hard-drinking or greed of gain. With such a man you ought not even to eat.
12 Yanihusu nini kuwahukumu wale watu walio nje ya kanisa? Je, si mnapaswa kuwahukumu hao walio ndani?
For what business of mine is it to judge outsiders? Is it not for you to judge those who are within the Church
13 Mungu atawahukumu hao walio nje. “Ninyi mwondoeni huyo mtu mwovu miongoni mwenu.”
while you leave to God's judgement those who are outside? Remove the wicked man from among you.

< 1 Wakorintho 5 >