< 1 Nyakati 9 >

1 Waisraeli wote waliorodheshwa katika koo zilizoandikwa kwenye kitabu cha wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda walichukuliwa mateka kwenda Babeli kwa sababu ya kukosa uaminifu kwa Mungu.
Tous ceux d'Israël furent enregistrés dans les généalogies; et voici, ils sont inscrits dans le livre des rois d'Israël. Et Juda fut transporté à Babylone à cause de ses prévarications.
2 Basi watu wa kwanza kurudi kukaa kwenye milki zao katika miji yao walikuwa baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi na watumishi wa Hekalu.
Les premiers habitants qui demeurèrent dans leurs possessions, dans leurs villes, étaient les Israélites, les sacrificateurs, les Lévites et les Néthiniens.
3 Wale waliotoka Yuda, Benyamini, Efraimu na Manase ambao waliishi Yerusalemu walikuwa:
A Jérusalem habitaient des enfants de Juda, des enfants de Benjamin, des enfants d'Éphraïm et de Manassé.
4 Uthai mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imri, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
Des enfants de Pharets, fils de Juda: Uthaï, fils d'Ammihud, fils d'Omri, fils d'Imri, fils de Bani.
5 Wazao wa Washiloni waliorudi ni: Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe.
Des Shilonites: Asaja, le premier-né, et ses fils.
6 Kwa wana wa Zera: Yeueli. Watu wa Yuda jumla yao walikuwa watu 690.
Des enfants de Zérach: Jéuël et ses frères, six cent quatre-vingt-dix.
7 Kwa Benyamini walikuwa: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;
Des enfants de Benjamin: Sallu, fils de Meshullam, fils de Hodavia, fils d'Assénua;
8 Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya.
Jibnéja, fils de Jérocham; Éla, fils d'Uzzi, fils de Micri; Meshullam, fils de Shéphatia, fils de Réuël, fils de Jibnija;
9 Watu kutoka Benyamini kama walivyoorodheshwa katika koo zao jumla yao ni 956. Watu hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao.
Et leurs frères, selon leur génération: neuf cent cinquante-six. Tous ces hommes-là étaient chefs des pères, selon les maisons de leurs pères.
10 Wa jamaa za makuhani walikuwa: Yedaya, Yehoyaribu na Yakini;
Des sacrificateurs: Jédaeja, Jéhojarib, Jakin,
11 Azaria mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu aliyekuwa afisa kiongozi wa nyumba ya Mungu.
Azaria, fils de Hilkija, fils de Meshullam, fils de Tsadok, fils de Mérajoth, fils d'Achitub, gouverneur de la maison de Dieu;
12 Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yahzera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri.
Adaja, fils de Jérocham, fils de Pashur, fils de Malkija; Maesaï, fils d'Adiel, fils de Jachzéra, fils de Meshullam, fils de Meshillémith, fils d'Immer;
13 Makuhani waliokuwa viongozi wa jamaa zao walikuwa 1,760. Walikuwa watu wenye uwezo, waliowajibika kuhudumu katika nyumba ya Mungu.
Et leurs frères, chefs de la maison de leurs pères, mille sept cent soixante, hommes vaillants, pour l'œuvre du service de la maison de Dieu.
14 Jamaa za Walawi walikuwa: Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari.
Des Lévites: Shémaja, fils de Hashub, fils d'Azrikam, fils de Hashabia, des enfants de Mérari;
15 Bakbakari, Hereshi, Galali na Matania mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu.
Bakbakkar, Hérèsh, Galal, Matthania, fils de Mica, fils de Zicri, fils d'Asaph;
16 Obadia mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni. Berekia mwana wa Asa, mwana wa Elikana, ambao waliishi katika vijiji vya Wanetofathi.
Obadia, fils de Shémaja, fils de Galal, fils de Jéduthun; Bérekia, fils d'Asa, fils d'Elkana, qui habita dans les villages des Néthophatiens.
17 Mabawabu katika Hekalu la Bwana waliorudi walikuwa: Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani na ndugu zao. Shalumu alikuwa mlinzi wao mkuu.
Et les portiers: Shallum, Akkub, Talmon, Achiman, et leurs frères; Shallum était le chef.
18 Walikuwa wamewekwa katika lango la mfalme lililokuwa upande wa mashariki, mpaka wakati huu. Hawa walikuwa mabawabu wa kutoka kwenye kambi ya Walawi.
Et jusqu'à présent ils sont à la porte du roi, à l'orient. Ce sont les portiers pour le camp des enfants de Lévi.
19 Shalumu mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora, pamoja na mabawabu wenzake kutoka jamaa yake ya Kora waliwajibika kulinda malango ya Hema, kama vile baba zao walivyokuwa wamewajibika kulinda ingilio la Maskani ya Bwana.
Shallum, fils de Coré, fils d'Ebiasaph, fils de Coré, et ses frères, les Corites, de la maison de son père, avaient la charge de l'ouvrage du service, gardant les seuils du tabernacle; leurs pères avaient gardé l'entrée du camp de l'Éternel;
20 Hapo zamani Finehasi mwana wa Eleazari alikuwa kiongozi wa mabawabu, naye Bwana alikuwa pamoja naye:
Phinées, fils d'Éléazar, avec qui l'Éternel était, fut autrefois leur chef.
21 Zekaria mwana wa Meshelemia alikuwa bawabu katika ingilio la Hema la Kukutania.
Zacharie, fils de Meshélémia, était portier à l'entrée du tabernacle d'assignation.
22 Jumla ya waliochaguliwa kuwa mabawabu katika sakafu za kupuria nafaka walikuwa watu 212. Waliandikishwa kwa koo zao kwenye vijiji vyao. Mabawabu hawa waliwekwa katika nafasi zao za kuaminiwa na Daudi pamoja na mwonaji Samweli.
Tous choisis pour portiers des seuils, ils étaient deux cent douze, enregistrés dans les généalogies d'après leurs villages; David et Samuel, le Voyant, les avaient établis dans leur office.
23 Wao na wazao wao walikuwa viongozi wa kulinda malango ya nyumba ya Bwana, nyumba iliyoitwa Hema.
Eux et leurs enfants étaient préposés à la garde des portes de la maison de l'Éternel, de la maison du tabernacle.
24 Mabawabu walikuwa pande zote nne: mashariki, magharibi, kaskazini na kusini.
Il y avait des portiers aux quatre vents, à l'orient, à l'occident, au nord et au midi.
25 Ndugu zao katika vijiji vyao walikuwa wakija mara kwa mara na kuwasaidia katika kazi zao kwa vipindi mbalimbali vya siku saba.
Leurs frères, qui étaient dans leurs villages, devaient de temps en temps venir auprès d'eux pendant sept jours.
26 Lakini mabawabu wanne wakuu, waliokuwa Walawi, walikabidhiwa wajibu kwa ajili ya vyumba na hazina katika nyumba ya Mungu.
Car ces quatre chefs des portiers étaient toujours en fonctions. Ils étaient Lévites, et étaient préposés sur les chambres et sur les trésors de la maison de Dieu.
27 Walikesha mahali walipowekwa kuizunguka nyumba ya Mungu, kwa sababu iliwapasa kuilinda. Pia walitunza funguo kwa ajili ya kufungua mlango kila siku asubuhi.
Ils se tenaient la nuit autour de la maison de Dieu; car la garde leur en appartenait, et ils avaient la charge de l'ouvrir tous les matins.
28 Baadhi yao walikuwa viongozi wa kutunza vifaa vilivyotumika katika huduma ndani ya Hekalu; walivihesabu kila vilipoingizwa ndani na kila vilipotolewa.
Il y en avait d'entre eux qui étaient commis sur les ustensiles du service. Car on en faisait le compte lorsqu'on les rentrait et qu'on les sortait.
29 Wengine walipangiwa kutunza mapambo na vifaa vingine vya patakatifu, pamoja na unga, divai, mafuta, uvumba na vikolezo.
Il y en avait aussi qui étaient commis sur les ustensiles, sur tous les ustensiles du sanctuaire et sur la fleur de farine, le vin, l'huile, l'encens et les aromates.
30 Lakini baadhi ya makuhani walifanya kazi ya kuchanganya vikolezo.
Ceux qui faisaient les parfums aromatiques étaient des fils de sacrificateurs.
31 Mlawi aliyeitwa Matithia, mwana mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, wa ukoo wa Kora, alikabidhiwa wajibu kwa ajili ya kuoka mikate ya sadaka.
Matthithia, d'entre les Lévites, premier-né de Shallum, Corite, avait la charge des gâteaux cuits sur la plaque.
32 Baadhi ya ndugu zao wa ukoo wa Kohathi walikuwa viongozi wa kuandaa mikate ya Wonyesho kwa ajili ya kila Sabato, mikate iliyokuwa inawekwa mezani.
Parmi les enfants des Kéhathites, leurs frères, il y en avait qui avaient la charge des pains de proposition, pour les apprêter, chaque sabbat.
33 Wale waliokuwa waimbaji, viongozi wa jamaa za Walawi, waliishi katika vyumba vya Hekalu, nao hawakufanya shughuli nyingine yoyote kwa sababu iliwapasa kuwajibika kwa kazi hiyo usiku na mchana.
Ce sont là les chantres, chefs des maisons des pères des Lévites, demeurant dans les chambres, exemptés d'autres charges parce qu'ils devaient être en fonctions le jour et la nuit.
34 Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa za Walawi, wakuu kama walivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
Ce sont là les chefs des pères des Lévites, chefs selon leur naissance; ils habitaient à Jérusalem.
35 Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka,
Le père de Gabaon, Jéïel, habita à Gabaon; et le nom de sa femme était Maaca;
36 mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
Son fils, le premier-né, fut Abdon, puis Tsur, Kis, Baal, Ner, Nadab,
37 Gedori, Ahio, Zekaria na Miklothi.
Guédor, Achjo, Zacharie et Mikloth.
38 Miklothi akamzaa Shimeamu. Wao pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
Mikloth engendra Shiméam. Ils habitèrent aussi près de leurs frères à Jérusalem, avec leurs frères.
39 Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli. Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
Ner engendra Kis; Kis engendra Saül; Saül engendra Jonathan, Malkishua, Abinadab et Eshbaal.
40 Yonathani akamzaa Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
Le fils de Jonathan fut Mérib-Baal; et Mérib-Baal engendra Mica.
41 Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea, na Ahazi.
Fils de Mica: Pithon, Mélec, Thaeréa et Achaz.
42 Ahazi akamzaa Yara, Yara akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
Achaz engendra Jaera; Jaera engendra Alémeth, Azmaveth et Zimri; Zimri engendra Motsa;
43 Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
Motsa engendra Binea, qui eut pour fils Réphaja, qui eut pour fils Éleasa, qui eut pour fils Atsel.
44 Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Aseli.
Atsel eut six fils, dont voici les noms: Azrikam, Bocru, Ismaël, Shéaria, Obadia et Hanan. Ce sont là les fils d'Atsel.

< 1 Nyakati 9 >