< 2 Nyakati 1 >

1 Solomoni mwana wa Daudi alijiimarisha kwenye milango yote! Katika ufalme wake, kwa kuwa Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye, naye akamfanya mkuu mno.
Or Salomon, fils de David, s'affermit dans son règne; l'Éternel son Dieu fut avec lui, et l'éleva extrêmement.
2 Ndipo Solomoni akasema na Israeli wote, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, waamuzi na viongozi wote katika Israeli, pamoja na wakuu wa jamaa.
Et Salomon parla à tout Israël, aux chefs de milliers et de centaines, aux juges et à tous les principaux de tout Israël, chefs des maisons des pères.
3 Naye Solomoni na kusanyiko lote wakakwea mpaka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kwa kuwa huko ndiko Hema la Kukutania la Mungu lilipokuwa, ambalo Mose mtumishi wa Bwana alikuwa amelitengeneza huko jangwani.
Et Salomon et toute l'assemblée avec lui, allèrent au haut lieu qui était à Gabaon; car là était le tabernacle d'assignation de Dieu, que Moïse, serviteur de l'Éternel, avait fait dans le désert.
4 Basi Daudi alikuwa amelipandisha Sanduku la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu mpaka mahali alipokuwa amepatengeneza kwa ajili yake, kwa sababu alikuwa amesimamisha hema kwa ajili ya hilo Sanduku huko Yerusalemu.
Mais David avait amené l'arche de Dieu, de Kirjath-Jearim au lieu qu'il avait préparé; car il lui avait dressé un tabernacle à Jérusalem.
5 Lakini yale madhabahu ya shaba ambayo Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, alikuwa ametengeneza yalikuwa huko Gibeoni mbele ya Maskani ya Bwana Mungu, hivyo Solomoni na kusanyiko lote walimtafuta Mungu huko.
L'autel d'airain que Betsaléel, fils d'Uri, fils de Hur, avait fait, était là devant la Demeure de l'Éternel. Et Salomon et l'assemblée y cherchèrent l'Éternel.
6 Solomoni akapanda huko yalikokuwa madhabahu ya shaba mbele za Bwana katika Hema la Kukutania, na kutoa dhabihu 1,000 za sadaka za kuteketezwa juu yake.
Et Salomon offrit là, devant l'Éternel, mille holocaustes, sur l'autel d'airain qui était devant le tabernacle d'assignation.
7 Usiku ule Mungu akamtokea Solomoni na kumwambia, “Omba lolote utakalo nikupe.”
En cette nuit-là, Dieu apparut à Salomon, et lui dit: Demande ce que tu veux que je te donne.
8 Solomoni akamjibu Mungu, “Umemwonyesha baba yangu Daudi fadhili nyingi, nawe umeniweka niwe mfalme mahali pake.
Et Salomon répondit à Dieu: Tu as usé de grande miséricorde envers David, mon père, et tu m'as établi roi à sa place.
9 Sasa, Bwana Mungu, ahadi yako kwa baba yangu Daudi na ithibitike, kwa kuwa umenifanya mimi mfalme juu ya watu ambao ni wengi kama mavumbi ya nchi.
Maintenant, Éternel Dieu! que ta parole à David, mon père, soit ferme; car tu m'as établi roi sur un peuple nombreux comme la poussière de la terre.
10 Nakuomba unipe mimi hekima na maarifa, ili niweze kuongoza watu hawa, kwa kuwa ni nani awezaye kutawala hawa watu wako walio wengi hivi?”
Donne-moi donc maintenant de la sagesse et de l'intelligence, afin que je sache me conduire devant ce peuple; car qui pourrait juger ton peuple, ce peuple si grand?
11 Mungu akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa jambo hili ndilo shauku ya moyo wako na hukuomba mali, utajiri au heshima, wala kifo kwa ajili ya adui zako, nawe kwa kuwa hukuomba maisha marefu, bali umeomba hekima na maarifa ili kuongoza watu wangu ambao nimekufanya uwe mfalme juu yao,
Et Dieu dit à Salomon: Puisque c'est là ce qui est dans ton cœur, et que tu n'as demandé ni des richesses, ni des biens, ni de la gloire, ni la mort de ceux qui te haïssent, ni même des jours nombreux, mais que tu as demandé pour toi de la sagesse et de l'intelligence, afin de pouvoir juger mon peuple, sur lequel je t'ai établi roi,
12 kwa hiyo utapewa hekima na maarifa. Tena nitakupa pia mali, utajiri na heshima, ambavyo hakuna mfalme yeyote aliyekuwepo kabla yako amewahi kuwa navyo, na hakuna yeyote baada yako atakayekuwa navyo.”
La sagesse et l'intelligence te sont données. Je te donnerai aussi des richesses, des biens et de la gloire, comme n'en ont pas eu les rois qui ont été avant toi, et comme n'en aura aucun après toi.
13 Ndipo Solomoni akaenda mpaka Yerusalemu kutoka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kutoka mbele ya Hema la Kukutania. Naye akatawala Israeli.
Puis Salomon s'en retourna à Jérusalem, du haut lieu qui était à Gabaon, de devant le tabernacle d'assignation; et il régna sur Israël.
14 Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu.
Salomon rassembla des chars et des cavaliers; il avait quatorze cents chars et douze mille cavaliers; et il les mit dans les villes où il tenait ses chars, et auprès du roi, à Jérusalem.
15 Mfalme akafanya fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
Et le roi fit que l'argent et l'or étaient aussi communs à Jérusalem que les pierres, et les cèdres, que les sycomores de la plaine.
16 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue.
Le lieu d'où l'on tirait les chevaux pour Salomon était l'Égypte; une troupe de marchands du roi allaient en chercher un convoi pour un prix convenu.
17 Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha, na farasi kwa shekeli 150. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.
On faisait monter et sortir d'Égypte un char pour six cents sicles d'argent, et un cheval pour cent cinquante. On en amenait de même par eux pour tous les rois des Héthiens, et pour les rois de Syrie.

< 2 Nyakati 1 >