< Salmos 96 >

1 CANTAD á Jehová canción nueva; cantad á Jehová, toda la tierra.
Oh, mwimbieni Yahwe wimbo mpya; mwimbieni Yahwe, nchi yote.
2 Cantad á Jehová, bendecid su nombre: anunciad de día en día su salud.
Mwimbieni Yahwe, tukuzeni jina lake; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
3 Contad entre las gentes su gloria, en todos los pueblos sus maravillas.
Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa, matendo yake ya ajabu kati ya mataifa.
4 Porque grande es Jehová, y digno de suprema alabanza; terrible sobre todos los dioses.
Maana Yahwe ni mkuu na wakusifiwa sana. Ni wakuhofiwa kuliko miungu mingine.
5 Porque todos los dioses de los pueblos son ídolos: mas Jehová hizo los cielos.
Maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, bali ni Yahwe aliye zifanya mbingu.
6 Alabanza y magnificencia delante de él: fortaleza y gloria en su santuario.
Heshima na adhama ziko mbele zake. Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.
7 Dad á Jehová, oh familias de los pueblos, dad á Jehová la gloria y la fortaleza.
Mpeni Yahwe sifa, enyi ukoo wa watu, mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
8 Dad á Jehová la honra debida á su nombre: tomad presentes, y venid á sus atrios.
Mpeni Yahwe utukufu ambao unastahili jina lake. Leteni matoleo na muingie nyuani mwake.
9 Encorvaos á Jehová en la hermosura de [su] santuario: temed delante de él, toda la tierra.
Mpigieni magoti Yahwe mkiwa mmevaa mavazi ambayo yanaheshimu utakatifu wake. Nchi yote tetemekeni mbele zake.
10 Decid en las gentes: Jehová reinó, también afirmó el mundo, no será conmovido: juzgará á los pueblos en justicia.
Semeni kati ya mataifa, Yahwe anatawala.” Ulimwengu pia umeimarishwa; hauwezi kutikiswa. Yeye huwahukumu watu kwa haki.
11 Alégrense los cielos, y gócese la tierra: brame la mar y su plenitud.
Mbingu na zifurahi, na nchi ishangilie; bahari na ivume na vyote viijazavyo vipige kelele kwa shangwe.
12 Regocíjese el campo, y todo lo que en él está: entonces todos los árboles del bosque rebosarán de contento,
Mashamba yashangilie na vyote vilivyomo. Kisha miti ya mstuni ipige kelele kwa furaha
13 Delante de Jehová que vino: porque vino á juzgar la tierra. Juzgará al mundo con justicia, y á los pueblos con su verdad.
mbele za Yahwe, maana yeye anakuja. Anakuja kuihukumu nchi. Naye atauhukumu ulumwengu kwa haki na mataifa kwa uaminifu wake.

< Salmos 96 >