< Salmos 75 >

1 Al Músico principal: sobre No destruyas: Salmo de Asaph: Cántico. ALABARÉMOSTE, oh Dios, alabaremos; que cercano está tu nombre: cuenten tus maravillas.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
2 Cuando yo tuviere tiempo, yo juzgaré rectamente.
Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
3 Arruinábase la tierra y sus moradores: yo sostengo sus columnas. (Selah)
Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
4 Dije á los insensatos: No os infatuéis; y á los impíos: No levantéis el cuerno:
Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
5 No levantéis en alto vuestro cuerno; no habléis con cerviz erguida.
Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
6 Porque ni de oriente, ni de occidente, ni del desierto [viene] el ensalzamiento.
Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
7 Mas Dios es el juez: á éste abate, y á aquél ensalza.
Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
8 Porque el cáliz está en la mano de Jehová, y el vino es tinto, lleno de mistura; y él derrama del mismo: ciertamente sus heces chuparán y beberán todos los impíos de la tierra.
Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
9 Mas yo anunciaré siempre, cantaré alabanzas al Dios de Jacob.
Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
10 Y quebraré todos los cuernos de los pecadores: los cuernos del justo serán ensalzados.
Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.

< Salmos 75 >