< Salmos 73 >

1 Salmo de Asaph. CIERTAMENTE bueno es Dios á Israel, á los limpios de corazón.
Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
2 Mas yo, casi se deslizaron mis pies; por poco resbalaron mis pasos.
Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
3 Porque tuve envidia de los insensatos, viendo la prosperidad de los impíos.
kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
4 Porque no hay ataduras para su muerte; antes su fortaleza está entera.
Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
5 No están ellos en el trabajo humano; ni son azotados con [los otros] hombres.
Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
6 Por tanto soberbia los corona: cúbrense de vestido de violencia.
Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
7 Sus ojos están salidos de gruesos: logran con creces los antojos del corazón.
Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
8 Soltáronse, y hablan con maldad de [hacer] violencia; hablan con altanería.
Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
9 Ponen en el cielo su boca, y su lengua pasea la tierra.
Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
10 Por eso su pueblo vuelve aquí, y aguas de lleno les son exprimidas.
Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
11 Y dicen: ¿Cómo sabe Dios? ¿y hay conocimiento en lo alto?
Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
12 He aquí estos impíos, sin ser turbados del mundo, alcanzaron riquezas.
Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
13 Verdaderamente en vano he limpiado mi corazón, y lavado mis manos en inocencia;
Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
14 Pues he sido azotado todo el día, [y empezaba] mi castigo por las mañanas.
Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
15 Si dijera yo, Discurriré de esa suerte; he aquí habría negado la nación de tus hijos:
Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
16 Pensaré pues para saber esto: es á mis ojos [duro] trabajo,
Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
17 Hasta que venido al santuario de Dios, entenderé la postrimería de ellos.
Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
18 Ciertamente los has puesto en deslizaderos; en asolamientos los harás caer.
Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
19 ¡Cómo han sido asolados! ¡cuán en un punto! Acabáronse, fenecieron con turbaciones.
Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
20 Como sueño del que despierta, así, Señor, cuando despertares, menospreciarás sus apariencias.
Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
21 Desazonóse á la verdad mi corazón, y en mis riñones sentía punzadas.
Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
22 Mas yo era ignorante, y no entendía: era como una bestia acerca de ti.
Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
23 Con todo, yo siempre estuve contigo: trabaste de mi mano derecha.
Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
24 Hasme guiado según tu consejo, y después me recibirás en gloria.
Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
25 ¿A quién tengo yo en los cielos? Y fuera de ti nada deseo en la tierra.
Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
26 Mi carne y mi corazón desfallecen: [mas] la roca de mi corazón y mi porción es Dios para siempre.
Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
27 Porque he aquí, los que se alejan de ti perecerán: tú cortarás á todo aquel que fornicando, de ti [se aparta].
Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 Y en cuanto á mí, el acercarme á Dios es el bien: he puesto en el Señor Jehová mi esperanza, para contar todas tus obras.
Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.

< Salmos 73 >