< Salmos 72 >

1 Para Salomón. OH Dios, da tus juicios al rey, y tu justicia al hijo del rey.
Mpe mfalme amri ya haki yako, Mungu, haki yako kwa wana wa mfalme.
2 El juzgará tu pueblo con justicia, y tus afligidos con juicio.
Naye awaamue watu wako kwa haki na maskini wako kwa haki sawa.
3 Los montes llevarán paz al pueblo, y los collados justicia.
Milima iwazalie watu amani; vilima navyo vizae haki.
4 Juzgará los afligidos del pueblo, salvará los hijos del menesteroso, y quebrantará al violento.
Naye awahukumu watu maskini; awaokoe watoto wa wahitaji na kuwavunja vipande vipande wenye kuwatesa.
5 Temerte han mientras duren el sol y la luna, por generación de generaciones.
Na wakuheshimu wewe wakati wa jua, na kwa kipindi cha kudumu kwa mwezi katika vizazi vyote.
6 Descenderá como la lluvia sobre la hierba cortada; como el rocío que destila [sobre] la tierra.
Naye apate kuja kama mvua juu ya nyasi zilizokatwa, kama manyuyu yanyunyizayo nchi.
7 Florecerá en sus días justicia, y muchedumbre de paz, hasta que no haya luna.
Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
8 Y dominará de mar á mar, y desde el río hasta los cabos de la tierra.
Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
9 Delante de él se postrarán los Etiopes; y sus enemigos lamerán la tierra.
Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
10 Los reyes de Tharsis y de las islas traerán presentes: los reyes de Sheba y de Seba ofrecerán dones.
Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.
11 Y arrodillarse han á él todos los reyes; le servirán todas las gentes.
Hakika wafalme wote wamwinamie yeye; mataifa yote yamtumikie yeye.
12 Porque él librará al menesteroso que clamare, y al afligido que no tuviere quien le socorra.
Kwa kuwa yeye humsaidia mhitaji na maskini asiye na msaidizi.
13 Tendrá misericordia del pobre y del menesteroso, y salvará las almas de los pobres.
Yeye huwahurumia maskini na wahitaji, na huokoa maisha ya wahitaji.
14 De engaño y de violencia redimirá sus almas; y la sangre de ellos será preciosa en sus ojos.
Huyaokoa maisha yao dhidi ya mateso na vurugu, na damu yao ni ya thamani machoni pake.
15 Y vivirá, y darásele del oro de Seba; y oraráse por él continuamente; todo el día se le bendecirá.
Naye apate kuishi! Na dhahabu za Sheba apewe yeye. Watu wamuombee yeye siku zote; Mungu ambariki daima.
16 Será [echado] un puño de grano en tierra, en las cumbres de los montes; su fruto hará ruido como el Líbano, y los de la ciudad florecerán como la hierba de la tierra.
Kuwepo na nafaka nyingi katika ardhi; juu ya milima kuwe na mawimbi ya mimea. Matunda yake yawe kama Lebanoni; watu wasitawi katika miji kama nyansi za kondeni.
17 Será su nombre para siempre, perpetuaráse su nombre mientras el sol dure: y benditas serán en él todas las gentes: llamarlo han bienaventurado.
Jina lake lidumu milele; jina lake ilindelee kama vile jua ling'aavyo; watu wabarikiwe katika yeye; mataifa yote wamwite mbarikiwa.
18 Bendito Jehová Dios, el Dios de Israel, que solo hace maravillas.
Yahwe Mungu, Mungu wa Israel, atukuzwe, ambaye pekee hufanya mambo ya ajabu.
19 Y bendito su nombre glorioso para siempre: y toda la tierra sea llena de su gloria. Amén y Amén.
Jina lake tukufu litukuzawe milele, nayo nchi yote ijazwe na utukufu wake. Amina, Amina.
20 Acábanse las oraciones de David, hijo de Isaí.
Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamemalizika. Kutatu cha tatu

< Salmos 72 >