< Salmos 44 >

1 Al Músico principal: de los hijos de Coré: Masquil. OH Dios, con nuestros oídos hemos oído, nuestros padres nos han contado, la obra que hiciste en sus días, en los tiempos antiguos.
Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
2 Tú con tu mano echaste las gentes, y los plantaste á ellos; afligiste los pueblos, y los arrojaste.
Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
3 Porque no se apoderaron de la tierra por su espada, ni su brazo los libró; sino tu diestra, y tu brazo, y la luz de tu rostro, porque te complaciste en ellos.
Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
4 Tú, oh Dios, eres mi rey: manda saludes á Jacob.
Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
5 Por medio de ti sacudiremos á nuestros enemigos: en tu nombre atropellaremos á nuestros adversarios.
Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
6 Porque no confiaré en mi arco, ni mi espada me salvará.
Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
7 Pues tú nos has guardado de nuestros enemigos, y has avergonzado á los que nos aborrecían.
Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
8 En Dios nos gloriaremos todo tiempo, y para siempre loaremos tu nombre. (Selah)
Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
9 Empero [nos] has desechado, y nos has hecho avergonzar; y no sales en nuestros ejércitos.
Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
10 Nos hiciste retroceder del enemigo, y saqueáron[nos] para sí los que nos aborrecían.
Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
11 Pusístenos como á ovejas para comida, y esparcístenos entre las gentes.
Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
12 Has vendido tu pueblo de balde, y no pujaste en sus precios.
Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
13 Pusístenos por vergüenza á nuestros vecinos, por escarnio y por burla á los que nos rodean.
Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
14 Pusístenos por proverbio entre las gentes, por movimiento de cabeza en los pueblos.
Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
15 Cada día mi vergüenza está delante de mí, y cúbreme la confusión de mi rostro,
Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
16 Por la voz del que [me] vitupera y deshonra, por razón del enemigo y del que se venga.
kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
17 Todo esto nos ha venido, y no nos hemos olvidado de ti; y no hemos faltado á tu pacto.
Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
18 No se ha vuelto atrás nuestro corazón, ni tampoco se han apartado nuestros pasos de tus caminos.
Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
19 Cuando nos quebrantaste en el lugar de los dragones, y nos cubriste con sombra de muerte,
Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
20 Si nos hubiésemos olvidado del nombre de nuestro Dios, ó alzado nuestras manos á dios ajeno,
Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
21 ¿No demandaría Dios esto? porque él conoce los secretos del corazón.
Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
22 Empero por tu causa nos matan cada día; somos tenidos como ovejas para el matadero.
Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
23 Despierta; ¿por qué duermes, Señor? Despierta, no te alejes para siempre.
Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
24 ¿Por qué escondes tu rostro, y te olvidas de nuestra aflicción, y de la opresión nuestra?
Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
25 Porque nuestra alma está agobiada hasta el polvo: nuestro vientre está pegado con la tierra.
Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
26 Levántate para ayudarnos, y redímenos por tu misericordia.
Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.

< Salmos 44 >