< Salmos 18 >

1 Al Músico principal: Salmo de David, siervo de Jehová, el cual profirió á Jehová las palabras de este cántico el día que le libró Jehová de mano de todos sus enemigos, y de mano de Saúl. Entonces dijo: AMARTE he, oh Jehová, fortaleza mía.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi: Nakupenda wewe, Ee Bwana, nguvu yangu.
2 Jehová, roca mía y castillo mío, y mi libertador; Dios mío, fuerte mío, en él confiaré; escudo mío, y el cuerno de mi salud, mi refugio.
Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu, Mungu wangu ni mwamba, ambaye kwake ninakimbilia. Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.
3 Invocaré á Jehová, digno de ser alabado, y seré salvo de mis enemigos.
Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
4 Cercáronme dolores de muerte, y torrentes de perversidad me atemorizaron.
Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
5 Dolores del sepulcro me rodearon, previniéronme lazos de muerte. (Sheol h7585)
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
6 En mi angustia invoqué á Jehová, y clamé á mi Dios: él oyó mi voz desde su templo, y mi clamor llegó delante de él, á sus oídos.
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.
7 Y la tierra fué conmovida y tembló; y moviéronse los fundamentos de los montes, y se estremecieron, porque se indignó él.
Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
8 Humo subió de su nariz, y de su boca consumidor fuego; carbones fueron por él encendidos.
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
9 Y bajó los cielos, y descendió; y oscuridad debajo de sus pies.
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
10 Y cabalgó sobre un querubín, y voló: voló sobre las alas del viento.
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
11 Puso tinieblas por escondedero suyo, su pabellón en derredor de sí; oscuridad de aguas, nubes de los cielos.
Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, hema lake kumzunguka, mawingu meusi ya mvua ya angani.
12 Por el resplandor delante de él, sus nubes pasaron; granizo y carbones ardientes.
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
13 Y tronó en los cielos Jehová, y el Altísimo dió su voz; granizo y carbones de fuego.
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
14 Y envió sus saetas, y desbaratólos; y echó relámpagos, y los destruyó.
Aliipiga mishale yake na kutawanya adui, naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.
15 Y aparecieron las honduras de las aguas, y descubriéronse los cimientos del mundo, á tu reprensión, oh Jehová, por el soplo del viento de tu nariz.
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwako, Ee Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.
16 Envió desde lo alto; tomóme, sacóme de las muchas aguas.
Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
17 Libróme de mi poderoso enemigo, y de los que me aborrecían, aunque eran ellos más fuertes que yo.
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
18 Asaltáronme en el día de mi quebranto: mas Jehová fué mi apoyo.
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
19 Y sacóme á anchura: libróme, porque se agradó de mí.
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
20 Hame pagado Jehová conforme á mi justicia: conforme á la limpieza de mis manos me ha vuelto.
Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
21 Porque yo he guardado los caminos de Jehová, y no me aparté impíamente de mi Dios.
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
22 Pues todos sus juicios estuvieron delante de mí, y no eché de mí sus estatutos.
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
23 Y fuí íntegro para con él, y cauteléme de mi maldad.
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
24 Pagóme pues Jehová conforme á mi justicia; conforme á la limpieza de mis manos delante de sus ojos.
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.
25 Con el misericordioso te mostrarás misericordioso, y recto para con el hombre íntegro.
Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia.
26 Limpio te mostrarás para con el limpio, y severo serás para con el perverso.
Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi.
27 Y tú salvarás al pueblo humilde, y humillarás los ojos altivos.
Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini huwashusha wenye kiburi.
28 Tú pues alumbrarás mi lámpara: Jehová mi Dios alumbrará mis tinieblas.
Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka; Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga.
29 Porque contigo desharé ejércitos; y con mi Dios asaltaré muros.
Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
30 Dios, perfecto su camino: es acendrada la palabra de Jehová: escudo es á todos los que en él esperan.
Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu, neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
31 Porque ¿qué Dios hay fuera de Jehová? ¿y qué fuerte fuera de nuestro Dios?
Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
32 Dios es el que me ciñe de fuerza, é hizo perfecto mi camino;
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
33 Quien pone mis pies como [pies] de ciervas, é hízome estar sobre mis alturas;
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
34 Quien enseña mis manos para la batalla, y será quebrado con mis brazos el arco de acero.
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
35 Dísteme asimismo el escudo de tu salud: y tu diestra me sustentó, y tu benignidad me ha acrecentado.
Hunipa ngao yako ya ushindi, nao mkono wako wa kuume hunitegemeza, unajishusha chini ili kuniinua.
36 Ensanchaste mis pasos debajo de mí, y no titubearon mis rodillas.
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
37 Perseguido he mis enemigos, y alcancélos, y no volví hasta acabarlos.
Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
38 Helos herido, y no podrán levantarse: cayeron debajo de mis pies.
Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
39 Pues me ceñiste de fortaleza para la pelea; has agobiado mis enemigos debajo de mí.
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
40 Y dísteme la cerviz de mis enemigos, y destruí á los que me aborrecían.
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
41 Clamaron, y no hubo quien salvase: [aun] á Jehová, mas no los oyó.
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
42 Y molílos como polvo delante del viento; esparcílos como lodo de las calles.
Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; niliwamwaga nje kama tope barabarani.
43 Librásteme de contiendas de pueblo: pusísteme por cabecera de gentes: pueblo que yo no conocía, me sirvió.
Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, watu ambao sikuwajua wananitumikia.
44 Así que hubo oído, me obedeció; los hijos de extraños me mintieron;
Mara wanisikiapo hunitii, wageni hunyenyekea mbele yangu.
45 Los extraños flaquearon, y tuvieron miedo desde sus encerramientos.
Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
46 Viva Jehová, y sea bendita mi roca; y ensalzado sea el Dios de mi salud:
Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu!
47 El Dios que me da las venganzas, y sujetó pueblos á mí.
Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, awatiishaye mataifa chini yangu,
48 Mi libertador de mis enemigos: hicísteme también superior de mis adversarios; librásteme de varón violento.
aniokoaye na adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
49 Por tanto yo te confesaré entre las gentes, oh Jehová, y cantaré á tu nombre.
Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana; nitaliimbia sifa jina lako.
50 El cual engrandece las saludes de su rey, y hace misericordia á su ungido, á David y á su simiente, para siempre.
Humpa mfalme wake ushindi mkuu, huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.

< Salmos 18 >