< Salmos 17 >

1 Oración de David. OYE, oh Jehová, justicia; está atento á mi clamor; escucha mi oración hecha sin labios de engaño.
Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
2 De delante de tu rostro salga mi juicio; vean tus ojos la rectitud.
Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
3 Tú has probado mi corazón, hasme visitado de noche; me has apurado, y nada inicuo hallaste: heme propuesto que mi boca no ha de propasarse.
Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
4 Para las obras humanas, por la palabra de tus labios yo me he guardado de las vías del destructor.
Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
5 Sustenta mis pasos en tus caminos, porque mis pies no resbalen.
Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
6 Yo te he invocado, por cuanto tú me oirás, oh Dios: inclina á mí tu oído, escucha mi palabra.
Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
7 Muestra tus estupendas misericordias, tú que salvas á los que en ti confían de los que se levantan contra tu diestra.
Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
8 Guárdame como lo negro de la niñeta del ojo, escóndeme con la sombra de tus alas,
Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
9 De delante de los malos que me oprimen, de mis enemigos que me cercan por la vida.
kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
10 Cerrados están con su grosura; con su boca hablan soberbiamente.
Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
11 Nuestros pasos nos han cercado ahora: puestos tienen sus ojos para echar[nos] por tierra.
Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
12 Parecen al león que desea hacer presa, y al leoncillo que está escondido.
Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
13 Levántate, oh Jehová; prevén su encuentro, póstrale: libra mi alma del malo con tu espada;
Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
14 De los hombres con tu mano, oh Jehová, de los hombres de mundo, cuya parte es en [esta] vida, y cuyo vientre hinches de tu tesoro: hartan [sus] hijos, y dejan el resto á sus chiquitos.
Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
15 Yo en justicia veré tu rostro: seré saciado cuando despertare á tu semejanza.
Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.

< Salmos 17 >