< Proverbios 29 >

1 EL hombre que reprendido endurece la cerviz, de repente será quebrantado; ni habrá [para él] medicina.
Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
2 Cuando los justos dominan, el pueblo se alegra: mas cuando domina el impío, el pueblo gime.
Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
3 El hombre que ama la sabiduría, alegra á su padre: mas el que mantiene rameras, perderá la hacienda.
Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
4 El rey con el juicio afirma la tierra: mas el hombre de presentes la destruirá.
Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
5 El hombre que lisonjea á su prójimo, red tiende delante de sus pasos.
Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
6 En la prevaricación del hombre malo hay lazo: mas el justo cantará y se alegrará.
Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
7 Conoce el justo la causa de los pobres: [mas] el impío no entiende sabiduría.
Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
8 Los hombres escarnecedores enlazan la ciudad: mas los sabios apartan la ira.
Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
9 Si el hombre sabio contendiere con el necio, que se enoje ó que se ría, no tendrá reposo.
Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
10 Los hombres sanguinarios aborrecen al perfecto: mas los rectos buscan su contentamiento.
Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
11 El necio da suelta á todo su espíritu; mas el sabio al fin le sosiega.
Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
12 Del señor que escucha la palabra mentirosa, todos sus ministros son impíos.
Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
13 El pobre y el usurero se encontraron: Jehová alumbra los ojos de ambos.
Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
14 El rey que juzga con verdad á los pobres, su trono será firme para siempre.
Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
15 La vara y la corrección dan sabiduría: mas el muchacho consentido avergonzará á su madre.
Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
16 Cuando los impíos son muchos, mucha es la prevaricación; mas los justos verán la ruina de ellos.
Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
17 Corrige á tu hijo, y te dará descanso, y dará deleite á tu alma.
Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
18 Sin profecía el pueblo será disipado: mas el que guarda la ley, bienaventurado él.
Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
19 El siervo no se corregirá con palabras: porque entiende, mas no corresponde.
Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
20 ¿Has visto hombre ligero en sus palabras? más esperanza hay del necio que de él.
Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
21 El que regala á su siervo desde su niñez, á la postre será su hijo.
Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
22 El hombre iracundo levanta contiendas; y el furioso muchas veces peca.
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
23 La soberbia del hombre le abate; pero al humilde de espíritu sustenta la honra.
Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
24 El aparcero del ladrón aborrece su vida; oirá maldiciones, y no [lo] denunciará.
Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
25 El temor del hombre pondrá lazo: mas el que confía en Jehová será levantado.
Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
26 Muchos buscan el favor del príncipe: mas de Jehová [viene] el juicio de cada uno.
Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
27 Abominación es á los justos el hombre inicuo; y abominación es al impío el de rectos caminos.
Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.

< Proverbios 29 >