< Proverbios 24 >

1 NO tengas envidia de los hombres malos, ni desees estar con ellos:
Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
2 Porque su corazón piensa en robar, é iniquidad hablan sus labios.
kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
3 Con sabiduría se edificará la casa, y con prudencia se afirmará:
Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
4 Y con ciencia se henchirán las cámaras de todo bien preciado y agradable.
Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
5 El hombre sabio es fuerte; y de pujante vigor el hombre docto.
Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
6 Porque con ingenio harás la guerra: y la salud está en la multitud de consejeros.
maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
7 Alta está para el insensato la sabiduría: en la puerta no abrirá él su boca.
Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
8 Al que piensa mal hacer le llamarán hombre de malos pensamientos.
Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
9 El pensamiento del necio es pecado: y abominación á los hombres el escarnecedor.
Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
10 Si fueres flojo en el día de trabajo, tu fuerza será reducida.
Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
11 Si dejares de librar los que son tomados para la muerte, y los que son llevados al degolladero;
Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
12 Si dijeres: Ciertamente no lo supimos; ¿no lo entenderá el que pesa los corazones? El que mira por tu alma, él lo conocerá, y dará al hombre según sus obras.
Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
13 Come, hijo mío, de la miel, porque es buena, y del panal dulce á tu paladar:
Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
14 Tal será el conocimiento de la sabiduría á tu alma: si la hallares tendrá recompensa, y al fin tu esperanza no será cortada.
Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
15 Oh impío, no aceches la tienda del justo, no saquees su cámara;
Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
16 Porque siete veces cae el justo, y se torna á levantar; mas los impíos caerán en el mal.
Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
17 Cuando cayere tu enemigo, no te huelgues; y cuando tropezare, no se alegre tu corazón:
Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
18 Porque Jehová no lo mire, y le desagrade, y aparte de sobre él su enojo.
au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
19 No te entrometas con los malignos, ni tengas envidia de los impíos;
Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
20 Porque para el malo no habrá [buen] fin, y la candela de los impíos será apagada.
maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
21 Teme á Jehová, hijo mío, y al rey; no te entrometas con los veleidosos:
Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
22 Porque su quebrantamiento se levantará de repente; y el quebrantamiento de ambos, ¿quién lo comprende?
maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
23 También estas cosas [pertenecen] á los sabios. Tener respeto á personas en el juicio no es bueno.
Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
24 El que dijere al malo, Justo eres, los pueblos lo maldecirán, y le detestarán las naciones:
Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
25 Mas los que [lo] reprenden, serán agradables, y sobre ellos vendrá bendición de bien.
Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
26 Besados serán los labios del que responde palabras rectas.
Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
27 Apresta tu obra de afuera, y disponla en tu heredad; y después edificarás tu casa.
Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
28 No seas sin causa testigo contra tu prójimo; y no lisonjees con tus labios.
Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
29 No digas: Como me hizo, así le haré; daré el pago al hombre según su obra.
Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
30 Pasé junto á la heredad del hombre perezoso, y junto á la viña del hombre falto de entendimiento;
Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
31 Y he aquí que por toda ella habían ya crecido espinas, ortigas habían ya cubierto su haz, y su cerca de piedra estaba ya destruída.
Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
32 Y yo miré, y púse[lo] en mi corazón: vi[lo], y tomé consejo.
Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
33 Un poco de sueño, cabeceando otro poco, poniendo mano sobre mano otro poco para dormir;
Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
34 Así vendrá como caminante tu necesidad, y tu pobreza como hombre de escudo.
na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.

< Proverbios 24 >