< Proverbios 24 >

1 NO tengas envidia de los hombres malos, ni desees estar con ellos:
Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
2 Porque su corazón piensa en robar, é iniquidad hablan sus labios.
kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
3 Con sabiduría se edificará la casa, y con prudencia se afirmará:
Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
4 Y con ciencia se henchirán las cámaras de todo bien preciado y agradable.
kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
5 El hombre sabio es fuerte; y de pujante vigor el hombre docto.
Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
6 Porque con ingenio harás la guerra: y la salud está en la multitud de consejeros.
kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
7 Alta está para el insensato la sabiduría: en la puerta no abrirá él su boca.
Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
8 Al que piensa mal hacer le llamarán hombre de malos pensamientos.
Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
9 El pensamiento del necio es pecado: y abominación á los hombres el escarnecedor.
Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
10 Si fueres flojo en el día de trabajo, tu fuerza será reducida.
Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
11 Si dejares de librar los que son tomados para la muerte, y los que son llevados al degolladero;
Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
12 Si dijeres: Ciertamente no lo supimos; ¿no lo entenderá el que pesa los corazones? El que mira por tu alma, él lo conocerá, y dará al hombre según sus obras.
Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
13 Come, hijo mío, de la miel, porque es buena, y del panal dulce á tu paladar:
Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
14 Tal será el conocimiento de la sabiduría á tu alma: si la hallares tendrá recompensa, y al fin tu esperanza no será cortada.
Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
15 Oh impío, no aceches la tienda del justo, no saquees su cámara;
Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
16 Porque siete veces cae el justo, y se torna á levantar; mas los impíos caerán en el mal.
Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
17 Cuando cayere tu enemigo, no te huelgues; y cuando tropezare, no se alegre tu corazón:
Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
18 Porque Jehová no lo mire, y le desagrade, y aparte de sobre él su enojo.
Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
19 No te entrometas con los malignos, ni tengas envidia de los impíos;
Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
20 Porque para el malo no habrá [buen] fin, y la candela de los impíos será apagada.
kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
21 Teme á Jehová, hijo mío, y al rey; no te entrometas con los veleidosos:
Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
22 Porque su quebrantamiento se levantará de repente; y el quebrantamiento de ambos, ¿quién lo comprende?
kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
23 También estas cosas [pertenecen] á los sabios. Tener respeto á personas en el juicio no es bueno.
Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
24 El que dijere al malo, Justo eres, los pueblos lo maldecirán, y le detestarán las naciones:
Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
25 Mas los que [lo] reprenden, serán agradables, y sobre ellos vendrá bendición de bien.
Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
26 Besados serán los labios del que responde palabras rectas.
Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
27 Apresta tu obra de afuera, y disponla en tu heredad; y después edificarás tu casa.
Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
28 No seas sin causa testigo contra tu prójimo; y no lisonjees con tus labios.
Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
29 No digas: Como me hizo, así le haré; daré el pago al hombre según su obra.
Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
30 Pasé junto á la heredad del hombre perezoso, y junto á la viña del hombre falto de entendimiento;
Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
31 Y he aquí que por toda ella habían ya crecido espinas, ortigas habían ya cubierto su haz, y su cerca de piedra estaba ya destruída.
miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
32 Y yo miré, y púse[lo] en mi corazón: vi[lo], y tomé consejo.
Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
33 Un poco de sueño, cabeceando otro poco, poniendo mano sobre mano otro poco para dormir;
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
34 Así vendrá como caminante tu necesidad, y tu pobreza como hombre de escudo.
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.

< Proverbios 24 >