< Job 6 >

1 Y RESPONDIÓ Job y dijo:
Kisha Ayubu akajibu:
2 ¡Oh si pesasen al justo mi queja y mi tormento, y se alzasen igualmente en balanza!
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
3 Porque pesaría aquél más que la arena del mar: y por tanto mis palabras son cortadas.
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 Porque las saetas del Todopoderoso están en mí, cuyo veneno bebe mi espíritu; y terrores de Dios me combaten.
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
5 ¿Acaso gime el asno montés junto á la hierba? ¿muge el buey junto á su pasto?
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
6 ¿Comeráse lo desabrido sin sal? ¿ó habrá gusto en la clara del huevo?
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
7 Las cosas que mi alma no quería tocar, por los dolores son mi comida.
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
8 ¡Quién me diera que viniese mi petición, y que Dios [me] otorgase lo que espero;
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
9 Y que pluguiera á Dios quebrantarme; que soltara su mano, y me deshiciera!
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 Y sería aún mi consuelo, si me asaltase con dolor sin dar más tregua, que yo no he escondido las palabras del Santo.
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 ¿Cuál es mi fortaleza para esperar aún? ¿y cuál mi fin para dilatar mi vida?
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 ¿Es mi fortaleza la de las piedras? ¿ó mi carne, es de acero?
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 ¿No me ayudo cuanto puedo, y el poder me falta del todo?
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 El atribulado es consolado de su compañero: mas hase abandonado el temor del Omnipotente.
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 Mis hermanos han mentido cual arroyo: pasáronse como corrientes impetuosas,
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
16 Que están escondidas por la helada, y encubiertas con nieve;
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 Que al tiempo del calor son deshechas, y en calentándose, desaparecen de su lugar;
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 Apártanse de la senda de su rumbo, van menguando y piérdense.
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
19 Miraron los caminantes de Temán, los caminantes de Saba esperaron en ellas:
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
20 [Mas] fueron avergonzados por su esperanza; porque vinieron hasta ellas, y halláronse confusos.
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
21 Ahora ciertamente como ellas sois vosotros: que habéis visto el tormento, y teméis.
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 ¿Os he dicho yo: Traedme, y pagad por mí de vuestra hacienda;
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
23 Y libradme de la mano del opresor, y redimidme del poder de los violentos?
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 Enseñadme, y yo callaré: y hacedme entender en qué he errado.
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
25 ¡Cuán fuertes son las palabras de rectitud! Mas ¿qué reprende el que reprende de vosotros?
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 ¿Pensáis censurar palabras, y los discursos de un desesperado, que son como el viento?
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
27 También os arrojáis sobre el huérfano, y hacéis hoyo delante de vuestro amigo.
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
28 Ahora pues, si queréis, mirad en mí, y [ved] si miento delante de vosotros.
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 Tornad ahora, y no haya iniquidad; volved aún [á considerar] mi justicia en esto.
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 ¿Hay iniquidad en mi lengua? ¿no puede mi paladar discernir las cosas depravadas?
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?

< Job 6 >