< Job 33 >

1 POR tanto, Job, oye ahora mis razones, y escucha todas mis palabras.
“Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
2 He aquí yo abriré ahora mi boca, y mi lengua hablará en mi garganta.
Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
3 Mis razones [declararán] la rectitud de mi corazón, y mis labios proferirán pura sabiduría.
Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
4 El espíritu de Dios me hizo, y la inspiración del Omnipotente me dió vida.
Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
5 Si pudieres, respóndeme; dispón [tus palabras], está delante de mí.
Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
6 Heme aquí á mí en lugar de Dios, conforme á tu dicho: de lodo soy yo también formado.
Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
7 He aquí que mi terror no te espantará, ni mi mano se agravará sobre ti.
Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
8 De cierto tú dijiste á oídos míos, y yo oí la voz de tus palabras [que decían]:
“Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
9 Yo soy limpio y sin defecto; y soy inocente, y no hay maldad en mí.
‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
10 He aquí que él buscó achaques contra mí, y me tiene por su enemigo;
Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
11 Puso mis pies en el cepo, y guardó todas mis sendas.
Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
12 He aquí en esto no has hablado justamente: yo te responderé que mayor es Dios que el hombre.
“Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
13 ¿Por qué tomaste pleito contra él? Porque él no da cuenta de ninguna de sus razones.
Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
14 Sin embargo, en una ó en dos [maneras] habla Dios; [mas el hombre] no entiende.
Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
15 Por sueño de visión nocturna, cuando el sueño cae sobre los hombres, cuando se adormecen sobre el lecho;
Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
16 Entonces revela al oído de los hombres, y les señala su consejo;
anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
17 Para quitar al hombre de [su] obra, y apartar del varón la soberbia.
ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
18 Detendrá su alma de corrupción, y su vida de que pase á cuchillo.
kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
19 También sobre su cama es castigado con dolor fuerte en todos sus huesos,
Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
20 Que le hace que su vida aborrezca el pan, y su alma la comida suave.
kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
21 Su carne desfallece sin verse, y sus huesos, que antes no se veían, aparecen.
Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
22 Y su alma se acerca al sepulcro, y su vida á los que causan la muerte.
Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
23 Si tuviera cerca de él [algún] elocuente anunciador muy escogido, que anuncie al hombre su deber;
“Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
24 Que le diga que [Dios] tuvo de él misericordia, que lo libró de descender al sepulcro, que halló redención:
kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
25 Enterneceráse su carne más que de niño, volverá á los días de su mocedad.
ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
26 Orará á Dios, y le amará, y verá su faz con júbilo: y él restituirá al hombre su justicia.
Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
27 El mira sobre los hombres; y [el que] dijere: Pequé, y pervertí lo recto, y no me ha aprovechado;
Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
28 [Dios] redimirá su alma, que no pase al sepulcro, y su vida se verá en luz.
Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
29 He aquí, todas estas cosas hace Dios dos y tres veces con el hombre;
“Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
30 Para apartar su alma del sepulcro, y para iluminarlo con la luz de los vivientes.
ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
31 Escucha, Job, y óyeme; calla, y yo hablaré.
“Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
32 Que si tuvieres razones, respóndeme: habla, porque yo te quiero justificar.
Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
33 Y si no, óyeme tú á mí; calla, y enseñarte he sabiduría.
Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”

< Job 33 >