< Job 30 >

1 MAS ahora los más mozos de días que yo, se ríen de mí; cuyos padres yo desdeñara ponerlos con los perros de mi ganado.
Sasa vijana wananidhihaki - vijana ambao baba zao wasingeweza hata kuwahudumia mbwa wa kundi langu.
2 Porque ¿para qué yo habría menester la fuerza de sus manos, en los cuales había perecido con el tiempo?
Kwa kweli, nguvu za mikono ya baba zao, zingenisaidia nini - watu ambao hawakuwa na nguvu wakati wa kukua kwao?
3 Por causa de la pobreza y del hambre [andaban] solos; huían á la soledad, á lugar tenebroso, asolado y desierto.
Walidhoofishwa na umasikini na njaa; walisaga nchi kavu mafichoni.
4 Que cogían malvas entre los arbustos, y raíces de enebro para calentarse.
Walichuma mche chumvi na majani ya vichaka; mizizi ya mti wa ufagio ilikuwa ndiyo chakula chao.
5 Eran echados de entre [las gentes], y todos les daban grita como al ladrón.
Waliondolewa miongoni mwa watu waliopiga kelele nyuma yao kama ambavyo mtu angempigia kelele mwizi.
6 Habitaban en las barrancas de los arroyos, en las cavernas de la tierra, y en las rocas.
Hivyo walipaswa kuishi katika mabonde ya mto, katika mashimo ya ardhi na miamba.
7 Bramaban entre las matas, y se reunían debajo de las espinas.
Walilia kwa uchungu porini kama punda; chini ya vichaka walikutana.
8 Hijos de viles, y hombres sin nombre, más bajos que la misma tierra.
Walikuwa uzao wa wapumbavu, hakika, wa watu wasiofaa; waliondolewa duniani kama waarifu.
9 Y ahora yo soy su canción, y he sido hecho su refrán.
Lakini sasa, nimekua sababu ya wimbo wa dhihaka kwa wana wao; hakika, nimekuwa mzaa kwao.
10 Abomínanme, aléjanse de mí, y aun de mi rostro no detuvieron su saliva.
Wananichukia na kusimama mbali nami; hawaachi kunitemea usoni.
11 Porque [Dios] desató mi cuerda, y me afligió, por eso se desenfrenaron delante de mi rostro.
Kwa maana Mungu ameondoa kamba katika upinde wangu na amenipiga, na hivyo watu hawa wanashindwa kujizuia mbele yangu.
12 A la mano derecha se levantaron los jóvenes; empujaron mis pies, y sentaron contra mí las vías de su ruina.
Kundi la vijana wabaya wanashambulia nguvu zangu; wananiondolea mbali na kukusanya kinyume changu rundo la kuhusuru.
13 Mi senda desbarataron, aprovecháronse de mi quebrantamiento, contra los cuales no hubo ayudador.
Wanaharibu maisha yangu; wanapeleka mbele maangamizi yangu, watu wasio na wakuwazuia.
14 Vinieron como por portillo ancho, revolviéronse á [mi] calamidad.
Wanakuja kinyume changu kama jeshi katika tundu pana katika ukuta wa mji; katikati ya maangamizi wanajizungusha juu yangu.
15 Hanse revuelto turbaciones sobre mí; combatieron como viento mi alma, y mi salud pasó como nube.
Hofu zimeniandama; heshima yangu imeondolewa mbali nami kama kwa upepo; mafanikio yangu yameondolewa kama wingu.
16 Y ahora mi alma está derramada en mí; días de aflicción me han aprehendido.
Sasa uhai wangu umeondolewa ndani yangu; siku nyingi za maumivu zimenipita.
17 De noche taladra sobre mí mis huesos, y mis pulsos no reposan.
Mifupa inauma ndani yangu wakati wa usiku; maumivu yanayonisaga hayaishi.
18 Con la grande copia [de materia] mi vestidura está demudada; cíñeme como el cuello de mi túnica.
Nguvu kuu ya Mungu imeshika mavazi yangu; yananizunguka kama kala ya vazi langu.
19 Derribóme en el lodo, y soy semejante al polvo y á la ceniza.
Amenitupa matopeni; nimekuwa kama vumbi na majivu.
20 Clamo á ti, y no me oyes; preséntome, y no me atiendes.
Nakulilia wewe, Mungu, lakini haunijibu; ninasimama, nawe unaniangalia tu.
21 Haste tornado cruel para mí: con la fortaleza de tu mano me amenazas.
Umegeuka na kuwa mkali kwangu; kwa nguvu za mkono wako umenitesa.
22 Levantásteme, é hicísteme cabalgar sobre el viento, y disolviste mi sustancia.
Unaniinua katika upepo na kuufanya unikokote; unanirusha huku na kule katika dhoruba.
23 Porque yo conozco que me reduces á la muerte; y á la casa determinada á todo viviente.
Kwa maana najua ya kwamba utanipeleka mautini, nyumba ya hatima kwa viumbe vyote.
24 Mas él no extenderá la mano contra el sepulcro; ¿clamarán [los sepultados] cuando él los quebrantare?
Lakini, je hakuna ainuaye mkono wake kuomba msaada aangukapo? Je hakuna aombaye msaada akiwa tabuni?
25 ¿No lloré yo al afligido? Y mi alma ¿no se entristeció sobre el menesteroso?
Je sikulia kwa ajili yake aliyekuwa tabuni? Je sijahuzunika kwa ajili ya mwitaji?
26 Cuando esperaba yo el bien, entonces vino el mal; y cuando esperaba luz, la oscuridad vino.
Nilipotazamia mema, ndipo yalipokuja mabaya; niliposubiri nuru, giza lilikuja badala yake.
27 Mis entrañas hierven, y no reposan; días de aflicción me han sobrecogido.
Moyo wangu umetaabika na hautulii; siku za mateso zimenipata.
28 Denegrido ando, y no por el sol: levantádome he en la congregación, y clamado.
Nimekuwa na ngozi nyeusi lakini si kwa sababu ya jua; nasimama katika kusanyiko na kulilia msaada.
29 He venido á ser hermano de los dragones, y compañero de los buhos.
Nimekuwa ndugu kwa mbwea, mshirika wa mbuni.
30 Mi piel está denegrida sobre mí, y mis huesos se secaron con ardentía.
Ngozi yangu imekuwa nyeusi na inapukutika; mifupa yangu imeunguzwa na joto.
31 Y hase tornado mi arpa en luto, y mi órgano en voz de lamentadores.
Kwa hiyo kinubi changu kimefunguliwa kwa nyimbo za maombolezo, zomari yangu kwa kuimba kwao waombolezao.

< Job 30 >