< Job 21 >

1 Y RESPONDIÓ Job, y dijo:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Oid atentamente mi palabra, y sea esto vuestros consuelos.
“Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
3 Soportadme, y yo hablaré; y después que hubiere hablado, escarneced.
Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
4 ¿Hablo yo á algún hombre? y ¿por qué no se ha de angustiar mi espíritu?
Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
5 Miradme, y espantaos, y poned la mano sobre la boca.
Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
6 Aun yo mismo, cuando me acuerdo, me asombro, y toma temblor mi carne.
Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
7 ¿Por qué viven los impíos, y se envejecen, y aun crecen en riquezas?
Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
8 Su simiente con ellos, compuesta delante de ellos; y sus renuevos delante de sus ojos.
Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
9 Sus casas seguras de temor, ni hay azote de Dios sobre ellos.
Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
10 Sus vacas conciben, no abortan; paren sus vacas, y no malogran su cría.
Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
11 Salen sus chiquitos como manada, y sus hijos andan saltando.
Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
12 Al son de tamboril y de cítara saltan, y se huelgan al son del órgano.
Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
13 Gastan sus días en bien, y en un momento descienden á la sepultura. (Sheol h7585)
Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol h7585)
14 Dicen pues á Dios: Apártate de nosotros, que no queremos el conocimiento de tus caminos.
Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
15 ¿Quién es el Todopoderoso, para que le sirvamos? ¿y de qué nos aprovechará que oremos á él?
Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
16 He aquí que su bien no está en manos de ellos: el consejo de los impíos lejos esté de mí.
Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
17 ¡Oh cuántas veces la lámpara de los impíos es apagada, y viene sobre ellos su quebranto, [y Dios] en su ira les reparte dolores!
Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
18 Serán como la paja delante del viento, y como el tamo que arrebata el torbellino.
Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
19 Dios guardará para sus hijos su violencia; y le dará su pago, para que conozca.
Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
20 Verán sus ojos su quebranto, y beberá de la ira del Todopoderoso.
Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
21 Porque ¿qué deleite tendrá él de su casa después de sí, siendo cortado el número de sus meses?
Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
22 ¿Enseñará alguien á Dios sabiduría, juzgando él á los que están elevados?
Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
23 Este morirá en el vigor de su hermosura, todo quieto y pacífico.
Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
24 Sus colodras están llenas de leche, y sus huesos serán regados de tuétano.
Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
25 Y estotro morirá en amargura de ánimo, y no habiendo comido jamás con gusto.
Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
26 Igualmente yacerán ellos en el polvo, y gusanos los cubrirán.
Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
27 He aquí, yo conozco vuestros pensamientos, y las imaginaciones que contra mí forjáis.
Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
28 Porque decís: ¿Qué es de la casa del príncipe, y qué de la tienda de las moradas de los impíos?
Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
29 ¿No habéis preguntado á los que pasan por los caminos, por cuyas señas no negaréis,
Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
30 Que el malo es reservado para el día de la destrucción? Presentados serán en el día de las iras.
kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
31 ¿Quién le denunciará en su cara su camino? Y de lo que él hizo, ¿quién le dará el pago?
Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
32 Porque llevado será él á los sepulcros, y en el montón permanecerá.
Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
33 Los terrones del valle le serán dulces; y tras de él será llevado todo hombre, y antes de él [han ido] innumerables.
Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
34 ¿Cómo pues me consoláis en vano, viniendo á parar vuestras respuestas en falacia?
Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”

< Job 21 >