< Job 12 >

1 Y RESPONDIÓ Job, y dijo:
Ndipo Ayubu akajibu:
2 Ciertamente que vosotros sois el pueblo; y con vosotros morirá la sabiduría.
“Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
3 También tengo yo seso como vosotros; no soy yo menos que vosotros: ¿y quién habrá que no pueda decir otro tanto?
Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
4 Yo soy uno de quien su amigo se mofa, que invoca á Dios, y él le responde: con todo, el justo y perfecto es escarnecido.
“Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
5 Aquel cuyos pies van á resbalar, [es como] una lámpara despreciada de aquel que está á sus anchuras.
Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
6 Prosperan las tiendas de los ladrones, y los que provocan á Dios viven seguros; en cuyas manos él ha puesto [cuanto tienen].
Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
7 Y en efecto, pregunta ahora á las bestias, que ellas te enseñarán; y á las aves de los cielos, que ellas te lo mostrarán:
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
8 O habla á la tierra, que ella te enseñará; los peces de la mar te [lo] declararán también.
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
9 ¿Qué cosa de todas estas no entiende que la mano de Jehová la hizo?
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
10 En su mano está el alma de todo viviente, y el espíritu de toda carne humana.
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
11 Ciertamente el oído distingue las palabras, y el paladar gusta las viandas.
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
12 En los viejos está la ciencia, y en la larga edad la inteligencia.
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
13 Con Dios está la sabiduría y la fortaleza; suyo es el consejo y la inteligencia.
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
14 He aquí, él derribará, y no será edificado: encerrará al hombre, y no habrá quien le abra.
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
15 He aquí, él detendrá las aguas, y se secarán; él las enviará, y destruirán la tierra.
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
16 Con él está la fortaleza y la existencia; suyo es el que yerra, y el que hace errar.
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
17 El hace andar á los consejeros desnudos [de consejo], y hace enloquecer á los jueces.
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
18 El suelta la atadura de los tiranos, y ata el cinto á sus lomos.
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
19 El lleva despojados á los príncipes, y trastorna á los poderosos.
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
20 El impide el labio á los que dicen verdad, y quita á los ancianos el consejo.
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
21 El derrama menosprecio sobre los príncipes, y enflaquece la fuerza de los esforzados.
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
22 El descubre las profundidades de las tinieblas, y saca á luz la sombra de muerte.
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
23 El multiplica las gentes, y él las destruye: él esparce las gentes, y las torna á recoger.
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
24 El quita el seso de las cabezas del pueblo de la tierra, y háceles que se pierdan vagueando sin camino:
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
25 Van á tientas como en tinieblas y sin luz, y los hace errar como borrachos.
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.

< Job 12 >