< Salmos 50 >

1 El Dios de dioses, Jehová, habló; y convocó la tierra desde el nacimiento del sol hasta donde se pone.
Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
2 De Sión, perfección de hermosura, Dios resplandeció.
Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
3 Vendrá nuestro Dios, y no callará: fuego consumirá de su presencia: y al rededor de él habrá grande tempestad.
Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
4 Convocará a los cielos de arriba: y a la tierra para juzgar a su pueblo.
Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
5 Juntádme mis misericordiosos: los que concertaron mi concierto sobre sacrificio.
Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
6 Y denunciarán los cielos su justicia; porque Dios es juez. (Selah)
Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
7 Oye pueblo mío, y hablaré: Israel, y contestaré contra ti: Yo soy el Dios, el Dios tuyo.
Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
8 No te reprenderé sobre tus sacrificios; porque tus holocaustos delante de mí están siempre.
Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
9 No tomaré de tu casa becerros: ni machos de cabrío de tus apriscos.
Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
10 Porque mía es toda bestia del monte: millares de animales en los montes.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
11 Yo conozco a todas las aves de los montes; y las fieras del campo están conmigo.
Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
12 Si tuviere hambre, no te lo diré a ti; porque mío es el mundo y su plenitud.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
13 ¿Tengo de comer carne de gruesos toros, o, de beber sangre de machos de cabrío?
Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
14 Sacrifica a Dios alabanza: y paga al Altísimo tus votos.
Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
15 Y llámame en el día de la angustia; librarte he, y honrarme has.
Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
16 Y al malo dijo Dios: ¿Qué tienes tú que enarrar mis leyes: y que tomes mi concierto por tu boca:
Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
17 Aborreciendo tú el castigo, y echando detrás de ti mis palabras?
wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
18 Si veías al ladrón, tu corrías con él: y con los adúlteros era tu parte.
Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.
19 Tu boca metías en mal: y tu lengua componía engaño.
Mwautoa mdomo wenu kwa mabaya, huelezea udanganyifu.
20 Asentábaste, hablabas contra tu hermano: contra el hijo de tu madre ponías infamia.
Mnakaa na kuongea dhidi ya ndugu yenu; na kukashfu mwana wa mama yenu.
21 Estas cosas hiciste, y yo callé: ¿pensabas por eso que de cierto sería yo como tú? argüirte he, y propondré delante de tus ojos.
Mmefanya mambo haya, lakini nimekaa kimya, hivyo mlidhani kuwa ni mtu flani nilliye kama ninyi mlivyo. Lakini nitawakaripia ninyi na kuwafunua, mbele ya macho yenu, mambo yote miliyofanya.
22 Entendéd ahora esto, los que os olvidáis de Dios: porque no arrebate, y no haya quien os escape.
Mlitilie maanani hili, ninyi mnao msahau Mungu, vinginevyo nitawakata ninyi vipande vipande, na hatakuwepo yeyote wakuja kuwasaidia!
23 El que sacrifica alabanza me honrará: y el que ordenare el camino, yo le enseñaré la salud de Dios.
Yule atoaye sadaka ya shukurani hunitukuza, na yeyote apangaye njia zake katika namna iliyo sahihi nitamuonesha wokovu wa Mungu.”

< Salmos 50 >