< Salmos 49 >

1 Oíd esto todos los pueblos: escuchád todos los habitadores del mundo:
Sikieni hili, ninyi watu wote; tegeni masikio, ninyi wenyeji wa dunia,
2 Así los hijos de los hombres como los hijos de los varones: juntamente el rico y el pobre.
wote walio chini na walio juu, tajiri na masikini wote pamoja.
3 Mi boca hablará sabidurías: y el pensamiento de mi corazón inteligencias.
Mdomo wangu utazungumza hekima na tafakari ya moyo wangu itakuwa ya uelewa.
4 Acomodaré a ejemplos mi oído: declararé con la arpa mi enigma.
Nitaelekeza sikio langu kwenye mfano; nitaanza mfano wangu kwa kinubi.
5 ¿Por qué temeré en los días de adversidad, cuando la iniquidad de mis calcañares me cercará?
Kwa nini nilazimike kuziogopa siku za uovu, wakati uovu umenizunguka kwenye visigino vyangu?
6 Los que confían en sus haciendas, y en la multitud de sus riquezas se jactan;
Kwa nini niwaogope wale wanao amini katika mali zao na kujivuna kuhusu utajiri wao?
7 Ninguno redimiendo redimirá al hermano: ni dará a Dios su rescate.
Ni hakika kuwa hakuna yeyote atakaye muokoa ndugu yake au kumpa Mungu pesa kwa ajili yake,
8 Porque la redención de su alma es de gran precio: y no se hará jamás,
Kwa maana ukombozi wa uhai wa mtu ni gharama kubwa, na hakuna awezaye kulipa kile tunacho daiwa.
9 Que viva adelante para siempre: y nunca vea la sepultura.
Hakuna yeyote atakaye ishi milele ili mwili wake usioze.
10 Porque se ve que los sabios mueren juntamente: el insensato y el ignorante perecen, y dejan a otros sus riquezas.
Maana yeye ataona uozo. Watu wenye hekima hufa; wajinga pia huangamia na kuacha mali zao kwa wengine.
11 En su íntimo piensan que sus casas son eternas: sus habitaciones para generación y generación: llamaron sus tierras de sus nombres.
Mawazo yao ya ndani ni kuwa familia zao zitaishi milele, na mahali waishipo, kwa vizazi vyote; wanaita ardhi zao kwa majina yao wenyewe.
12 Mas el hombre no permanecerá en honra: es semejante a las bestias que mueren.
Lakini mtu, kuwa na mali, haimaanishi atabaki hai; kama wanyama walioangamia.
13 Este es su camino, su locura: y sus descendientes corren por el dicho de ellos. (Selah)
Hii ni hatma ya wafanyao ujinga baada ya kufa, .................
14 Como ovejas son puestos en la sepultura, la muerte los pastorea; y los rectos se enseñorearon de ellos por la mañana: y su apariencia se envejece en la sepultura de su morada. (Sheol h7585)
Kama kondoo wamechaguliwa kwa ajili ya kuzimu na kifo kitakuwa mchungaji wao. Nao watatawaliwa na wenye haki ifikapo asubuhi, na miili yao italiwa kuzimuni, wakiwa hawana afasi ya kuishi kwa ajili yao. (Sheol h7585)
15 Ciertamente Dios redimirá mi vida del poder de la sepultura, cuando me tomará. (Selah) (Sheol h7585)
Bali Mungu ataufufua uhai wangu kutoka katika nguvu ya kuzimu; naye atanipokea. (Selah) (Sheol h7585)
16 No temas cuando se enriquece alguno: cuando aumenta la gloria de su casa.
Msifadhaike mtu awapo tajiri, utukufu wa nyumba yake uongezekapo.
17 Porque en su muerte no tomará nada: ni su gloria descenderá en pos de él.
Maana atakapo kufa hataondoka na chochote; utukufu wake hautamfuata yeye.
18 Porque mientras viviere, será su vida bendita: y tú serás loado cuando fueres bueno.
Yeye huifurahisha nafsi yake awapo hai na watu hukusifu wewe uishipo maisha yako mwenyewe-
19 El entrará a la generación de sus padres: para siempre no verán luz.
naye atakwenda kwenye ukoo wa baba zake naye kamwe hataiona nuru tena.
20 El hombre en honra que no entiende, semejante es a las bestias que mueren.
Yule ambaye ana mali lakini hana ufahamu ni kama wanyama, ambao wataangamia.

< Salmos 49 >