< Salmos 141 >

1 Jehová, a ti he llamado, apresúrate a mí: escucha mi voz, cuando te llamare.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima. Sikia sauti yangu ninapokuita.
2 Sea enderezada mi oración delante de ti como un perfume: el don de mis manos como un presente de la tarde.
Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba; kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.
3 Pon, o! Jehová, guarda a mi boca: guarda la puerta de mis labios.
Ee Bwana, weka mlinzi kinywani mwangu, weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
4 No inclines mi corazón a cosa mala: a hacer obras con impiedad con los varones que obran iniquidad; y no coma yo de sus delicias.
Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, nisije nikashiriki katika matendo maovu pamoja na watu watendao mabaya, wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
5 Hiérame el justo con misericordia, y repréndame; y aceite de cabeza no unte mi cabeza: porque aun también mi oración será contra sus males.
Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda mabaya,
6 Sean derribados en lugares peñascosos sus jueces; y oigan mis palabras que son suaves.
watawala wao watatupwa chini kutoka kwenye majabali, waovu watajifunza kwamba maneno yangu yalikuwa kweli.
7 Como quien parte e hiende leños en tierra, son esparcidos nuestros huesos a la boca de la sepultura: (Sheol h7585)
Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” (Sheol h7585)
8 Por tanto a ti, o! Jehová, Señor, miran mis ojos, en ti he confiado: no tengas en poco a mi alma.
Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mwenyezi, ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.
9 Guárdame de las manos del lazo que me han tendido; y de los lazos de los que obran iniquidad.
Niepushe na mitego waliyonitegea, kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.
10 Caigan los impíos a una en sus redes, mientras yo pasaré para siempre.
Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, wakati mimi ninapita salama.

< Salmos 141 >